Western Propaganda Turns Mugabe into a Tyrant

Kina Morgan katika nchi za kiafrika wamejaa wengi mpaka wanamwagika! hata Bongo tunao. Yaani ukiwahakikishia support na umaarufu, basi wako tayari kuuza hata utu wao. HIvi tujiulize, kuna siri gani ambayo Mbeki anayo na inamfanya amdharau sana Morgan?
 
Kama US na UK hawataki kumweka Tsivangira...Then ni nani huyo wanayetaka kumuweka?

Ama sijakuelewa?

Be specific unaposema hawataki kumweka!

Je ni kwanini hawajafanya lolote kule Darfur?

AMA ZIMBABWE TU NDO WENYE SHIDA?

SISI WENYEWE WENYE SHIDA AMBAYO WAO WENYEWE WANAIJUA KUTOKANA NA KASHFA ZOTE NA HATA BALLALI KUKIMBILIA KWAO...Kama hii ndio demokrasia na haki....! Then...

WAPI BALLALI?

Waache haya mambo mapema la sivyo nitawatoa nishai na wataumbuka!

Pengine uwezo wako wa kuelewa na kuchambua mambo ni mdogo.
Kama Britain na USA wanafanya mapinduzi ya kijeshi au wamehamisha Waingereza kwenda kupiga kura hapo nitakuelewa. Lakini kama ni Wazimbabwe ndo wanapiga kura ya kuamua nani awe rais, then SIO Britain na USA wanaomuweka Tsvangirai madarakani.

Kuhusu Darful sema sielewi chochote. Britain na USA wamefanya kama walivyofanya Zimbabwe, vikwazo, pesa na vifaa kwa jeshi la kulinda amani na baadhi ya maazimio yamekwamishwa na Mchina.

Au ulitaka wapeleke wanajeshi wao? Hivi wangepeleka wanajeshi wao Zimbabwe ungesemaje? Hilo jibu ni mojawapo ya sababu zinazowafanya wasipeleke jeshi huko Darful.
 
Wachina na wamarekani wanasubiri kuona ni silaha za nani zitafanya kazi zaidi!
Na tz mkirogwa mkaanzisha hivyo vita basi mujue havitakwisha!
Na Zimbabwe watakuwa na haki ya kushambulia bongo wanavyoweza!
Na mkishaanza vita...Sahau hata chakula!
Ni silaa tu!
Kwani Chenney ataziuza huku Bush na wengineo wakinyonya mafuta na madini!
Na baada ya kuhakikisha vita vinadumu kwa muda...Then wanaitisha mkutano mwingine wa G8 na kugawana!
Kuna aliyepanua mdomo Iraq kuvamiwa zaidi ya Mandela huko Afrika?
Akadiriki kusema hataki kukutana na Bush kwani ni kichaa!
Sisi tukapandisha bendera zao tukashusha zetu...Tukauza UHURU!
Dawa ya kuepukana na haya ni kuupiga vita ufisadi ili wasipate nafasi ya kuwabana viongozi mafisadi kwa vitisho vya kuwaondoa madarakani.
 
Pengine uwezo wako wa kuelewa na kuchambua mambo ni mdogo.
Kama Britain na USA wanafanya mapinduzi ya kijeshi au wamehamisha Waingereza kwenda kupiga kura hapo nitakuelewa. Lakini kama ni Wazimbabwe ndo wanapiga kura ya kuamua nani awe rais, then SIO Britain na USA wanaomuweka Tsvangirai madarakani.

Kuhusu Darful sema sielewi chochote. Britain na USA wamefanya kama walivyofanya Zimbabwe, vikwazo, pesa na vifaa kwa jeshi la kulinda amani na baadhi ya maazimio yamekwamishwa na Mchina.

Au ulitaka wapeleke wanajeshi wao? Hivi wangepeleka wanajeshi wao Zimbabwe ungesemaje? Hilo jibu ni mojawapo ya sababu zinazowafanya wasipeleke jeshi huko Darful.
Tusiharibu hii thread.
Twende tu hoja kwa hoja.
Umesema Bush hataki Tsivangirai awe raisi.
Sasa wanataka nani ndio awe raisi?
 
Kina Morgan katika nchi za kiafrika wamejaa wengi mpaka wanamwagika! hata Bongo tunao. Yaani ukiwahakikishia support na umaarufu, basi wako tayari kuuza hata utu wao. HIvi tujiulize, kuna siri gani ambayo Mbeki anayo na inamfanya amdharau sana Morgan?

Mie mbona namdharau Mbeki. Kiongozi gani huyo! Viongozi wengine wajinga tu,wakitokea kutoelewana na Westeners wanafanya ugovi huo personal bila kujali madhara kwa wananchi wao. Mbeki haelewani na Uingereza na USA. Sasa akipata mtu kama Mugabe lazima aside.
 
Kwa matokeo ya kura yaliyotangazwa na Mugabe na tume yake ya uchaguzi hata baada ya kuchelewesha kwa siku kibao yalionesha kuwa Mugabe kashindwa na Mzee Tsa..

Hii inaonesha kuwa wananchi wa Zimbabwe hawamtaki Mugabe...
 
JMushi you are indeed a son of Afrika and a true Tanzanian patriot. Keep burning them with the truth!! Wazalendo tafadhali someni kitabu kinachoitwa "Confessions of an Economic Hitman" by John Perkins ili kuelewa haya mambo ya Ufisadi Zimbabwe etc...

Aluta Continua!!
 
Kama wachina na Wamarekani wanapimana silaha zao kama ilivyo kwa mataifa makubwa...Then washambuliane wenyewe kwa wenyewe ili wananchiwao wajue machungu ya vita!
Marekani na wachina wanagombania dunia kama ilivyokuwa kwa USSR before!
Waliitumia AFRIKA PIA KAMA BATTLE GROUND YA KUZIPIMA SILAHA ZAO!
AKISHINDA MUGABE..China ana influence!
Na vita ikipamba moto..Silaha ndio dili...Tena watatupa silaha kwa kusaini mikataba ya migodi yetu na mafuta!
Kwa wakati huo hata rasilimali zetu hazitakuwa na umuhimu kwetu kama silaha za kuendelea kujilinda ili kuendelea kumtumikia bwana tuliyemchagua!
NASEMA NO NO NO KWENDA VITANI!
 
Obama anazungumzia ZIMBABWE NA ANASEMA SOUTH AFRIKA IACHIWE KAZI!
MAMBO YAMEANZA!
 
We should not blame western coutries for anything in Zimbabwe while we are doing nothing!. If we all care then lets us do something to fix the problem instead of blaming western coutries everyday, if Mugabe real care about blacks farmers where are they now? In south Africa and treated like animals. We should stop blaming western coutries and step up as Africans.

Basi kama usemayo ni kweli hiyo barua ya wazi mliyoandika kwa Sinclair ni Ujinga?

Brainwashing if prologed can be successful especially for pepole who usually move with western winds.
 
Yani nilitoka kuzungumza na kampeni ya OBAMA na issue a ZIM inakwenda kama wazalendo tunavyotaka at least kuhusu vita!
Angalieni CCN hapa!
ANASEMA SA WAPEWE NAFASI KWENYE MGOGORO NA NINAVYOJUA SA HAWATAKI VITA!
 
I really do not care much na ya Zimbabwe, kwa sababu utakuwa ni unafiki wa hali ya juu sana kujali ya huko Zimbabwe, wakati na hapa yapo hayo hayo,

Yaani mnasema kina Serukamba wana tofauti kubwa na kina Mugabe? Hiki kimbele mbele na mabo ya nchi zingine wa-Tanzania kiytatuisha lini? Yanatuhusu nini ya huko? Kwani Pemba wananchi hawakufa nani aliyekuja kutuingilia?

Kenya wamekufa wangapi? Mbona hatukusikia wazungu wakisema sana au kuingilia kama huku kwa Mugabe? Huu unafiki utatuponza sana Tanzania!
 
Field Marshall Es,

Mkuu shukran sana maanake sintapenda kurudia yale yaliyokwisha tangulia..
Mugabe ni kiongozi Mbovu kama walivyo wengine wa Afrika....Hana tofauti kabisa na kiongozi mwingine yoyote wa kiafrika ambaye anaona utawala wake unafikia hatma!...

Binafsi nitaendelea kuwachukia Westerners kwa kile walichokifanya- Kuwaweka vikwazo wananchi wa Zimbabwe kwa sababu ya mtu mmoja tu..
Now tujiulize ni sababu gani hasa iliyosababishwa vikwazo viwekwe mwaka 2001/2 ikiwa Mugabe alishinda uchaguzi uliotangulia na mwingine 2004.
Ubaya wa Mugabe haukuanza jana baada ya mauaji haya... ubaya wa Mugabe ulianza toka siku alochukua ardhi ya wazungu na kusema ati Mugabe alikuwa na wapinzani wakubwa toka 1997 ni uzushi mtupu!...Upinzani wa kisiasa ndio ulikuwepo kama ilivyo leo hii nchi zote..
Mubarak ameongoza Egypt kwa miaka mingapi na wamekufa wangapi huko, Algeria, Gabon na kwingineko ambako hadi leo hawakuweka vikwazo vya kiuchumi dhidi ya serikali hizo!..

Yes the guy is bad lakini sio kulingana na lugha ya mzungu ambaye hajali kabisa maisha ya mtu mweusi.. Tumeyaona Rwanda, Kongo, Somalia na Sudan ambako walipiga sana kampeni kuondoia utawala wa mwarabu.. Mwarabu kaweka mkataba wa mafuta na Marekani kelele zote zimekwisha!.. watu bado wanakufa kila siku na sijaona coverage ya maana tena sio CCN wala BBC zaidi ya matukio ya hapa na pale!..Je, mambo Sudan shwari kweli? if not why hawazungumzii tena.. ebu jiulizeni kama kweli hawa watu wanamjali mtu mweusi na sio maslahi yao.
 
Maneno ya muhimu ni mpaka waseme watu flan flan!
Lakini jf mbele!
Lengo ni moja!
UKOMBOZI WA AFRIKA!
TUKIANZIA NA TANZANIA KWANZA!
 
Sasa kina TSIVANGIRAI washajua kuwa hakuna vita na sasa kauli ni kusitisha uchaguzi ili ajiingize tena!

Mzalendo gani huyo anaongozwa kama tiara?

Sasa...Mark ma words..Mugabe will be victorious hata kama hatukutaka..Watayamaliza matatizo yao huko kwa kuwatumia SA kama inavyotakiwa...BUSH NA WENZAO WAME FAIL kwasababu ya resolve ya wazalendo!

HAYA...ZITTO RUDI ULIZIA EPA,RICHMOND,KAGODA ETC ETC.
Na pia ripoti yenu ya madini tunaitaka sasa hivi.

HALAFU WAAMBIE WAACHIE MATANGAZO KWA UHURU ILI TUWASIKE KINA SLAA NA MWAKYEMBE!
 
Bila kujali motive ya westernes, mtu anayesababisha mamilioni ya raia wake kukimbia nchi kwa njaa na matatizo mengi hastahili kuwa kiongozi Afrika.

Hawa ndio wanaipa nguvu dhana ya Ngabu....wanaabisha Afrika.

Pia mmegundua kwamba JK hana respect katika SADCC? Kama Mwenyekiti wa AU ameitisha kikao cha Marais wote wameingia mitini na kutuma maofisa wao wa chini with exception ya mwenyeji wa mkutano Ris wa Swaziland. Mbeki na Jk naona ndiyo hawawivi kabisaaaa! Enzi za Mwalimu akiitisha kikao kama hiki Marais wote wanahudhuria bila kukosa.
 
Nilimwambia zitto aachane na kikwete atammaliza kisiasa akabisha.

Nilmwambia credibility ya Kikwete Afrika hakuna tena kwani TAIFA LIMEUZWA!Mwenzio anapiga ngoma na wewe ndiye mchezaji!

Sasa haya mambo ya kutetea issue za kimataifa bila kusikiliza ushauri....Mambo yake ndiyo haya!

Kikwete alijidai kukupa majukumu hayo ili kukufanya uliwakilishe TAIFA na yeye kila siku kiguu na njia huku mkiwa hata hamuijui WORLD HOSTORY...Let it alone African History!

Sasa rudini muhakikishe mafisadi wanakamatwa ili imani ya wananchi irudi!

Na ninakushauri zitto uombe msamaha!
 
Jmushi1,
Mkuu usinielewe vibaya kwa sababu sikulitaja jina lako lakini kama umesoma vizuri nimesema sintapenda kurudia yale yaliyotangulia...sikumtaja mtu jina isipokuwa ujumbe wangu ulikuwa kwa Field Marshall Es ambaye alizungumzia zaidi mauaji yanayotokea Afrika.
Swala lako limesimama zaidi ktk siasa za Bongo ambazo binafsi sina ufahamu sana, na sielewi Kitwete na CCM wamesimama wapi zaidi ya kukisia..swala la Taifa kuuzwa letu na matukio ya Zimbabwe nashindwa kuyaunganisha kama unavyofanya wewe unayefahamu..
Kifupi waswahili wanasema ukiona watu kimya ujue wanajaribu kutafuna kabla hawajameza! kisha ndio uunaweza kuzungumza ndio ustaarabu wetu...
 
Jmushi1,
Mkuu usinielewe vibaya kwa sababu sikulitaja jina lako lakini kama umesoma vizuri nimesema sintapenda kurudia yale yaliyotangulia...sikumtaja mtu jina isipokuwa ujumbe wangu ulikuwa kwa Field Marshall Es ambaye alizungumzia zaidi mauaji yanayotokea Afrika.
Swala lako limesimama zaidi ktk siasa za Bongo ambazo binafsi sina ufahamu sana, na sielewi Kitwete na CCM wamesimama wapi zaidi ya kukisia..swala la Taifa kuuzwa letu na matukio ya Zimbabwe nashindwa kuyaunganisha kama unavyofanya wewe unayefahamu..
Kifupi waswahili wanasema ukiona watu kimya ujue wanajaribu kutafuna kabla hawajameza! kisha ndio uunaweza kuzungumza ndio ustaarabu wetu...

Haya tusubiri utaona!
Ila kuna ambao washaona...!
Kwani hakuna tena story za vita bungeni!
Sasa ni EPA,RICHOMONDULI,KIGODA ETC ETC...
Niliwaambia waje na PLAN B Mpema wakagoma...Wakagangamala kunifanya kichaa!
Soma thread zangu zote utajua tunaona mbali na UKOMBOZI NI SASA!
 
Watu Wenye Mtazamo Wa Wazungu Wanamuona Morgan Mshindi......!
Wenye Mtazamo Wa Kiafrika tunamuona mugabe Mshindi........!
mugabe Fight For Your Land....! Dont Let Vibaraka Wachukue Ardhi Huku Wewe Ukiangalia.....!
anachofanya Mugabe Sasa Ndicho Ilichofanya Tanzania Miaka Ya Nyuma.....! mugabe Uzi Huo Huo, Mpaka Kieleweke......!
 
Back
Top Bottom