Western Propaganda Turns Mugabe into a Tyrant

Western Propaganda Turns Mugabe into a Tyrant

Mkandara.
Kuwa ni mswahili hilo halina shaka. Umekiri kuwa Mugabe ni muuaji na ni kiongozi mbovu. Waliokuwa wakigombea urais huko Zimbabwe ni wawili, Robert na Morgan. Mada hii inadai kuwa watu wa magharibi wanafanya propaganda kumfanya Robert aonekane mbaya bila shaka ili Morgan, unayemuona kuwa ni puppet wao, ashinde. Hili unaona halikubaliki ndio maana tumekesha hapa tukipingana hoja. Mimi nasema Robert kutokana na uovu wake lazima atoke ( by implication si propaganda za watu wa magharibi zinazompakazia bali yeye ni mtu muovu) na ampishe mwingine, hata kama ni Morgan. Wewe unasema Morgan ni kibaraka kwa hiyo kwa vyo vyote vile asipewe urais. Kwa mantik yako mwenyewe ni kuwa kama ni choice kati ya Robert, muuaji na Morgan kibaraka, heri Robert aendelee. Katika hali ya Zimbabwe ilivyo sasa, huku ni kumshabikia Robert. Alternative uliyoitoa ni mwanamke ambaye hata jina humkumbuki! Huyu ambaye hata hajawahi kusimama hadharani kugombea urais. Hata Makoni humzungumzii. Kwa vile unadai mimi napindisha maneno yako, swali rahisi. Kati ya Robert Mugabe na Morgan Tsvangirai, ambao ndio walikuwa wagombea pekee wa urais katika raundi ya pili ya uchaguzi, ni nani unadhani anafaa kuwa rais wa Zimbabwe? mimi nasema Morgan Tsvangirai, kwa sababu kuna kila dalili alishinda ngwe ya kwanza na hata damu mikononi mwake. Mwenzangu unasemaje? Robert au Morgan?
 
Joshua Nkomo, Ndabaningi Sithole, Abel Muzorewa waliongoza mapambano dhidi ya utawala dhalimu wa Ian Smith. Sithole, Chitepo na Tekere ndiyo walioanzisha ZANU pamoja na Mugabe. ZANU baadae iligawanyika na Joshua Nkomo kuanzisha ZAPU. ZANU iliyobaki ikagawanyika tena na Mugabe na Tekere wakaanzisha ZANU-PF wakati Sithole akabaki na ZANU. Hawa wote hawakuwa active wakati wa kuchukua ardhi. Joshua Nkomo alishakata tamaa baada ya Robert Mugabe akiwatumia 5th brigade, kufanya mauaji dhidi ya base yake ya wandebele. Alifariki 1999. Ndabaningi Sithole alikuwa uhamishoni Marekani ambako alifariki tarehe 12 Desemba 2000. Huyu aliisha shitakiwa kwa kutaka kumuua Mugabe. Shamba lake limechukuliwa. Abel Muzorewa baada ya kuwa Waziri Mkuu katika serikali ya Zimbabwe-Rhodesia amepoteza umaarufu na hasikiki tena. Hawa wote walihusikaje katika kunyang'anywa ardhi wazungu? Uko kwenye www, kabla ya kuandika angalau google!
 
Yote aliyoyafamnya Morgan yanapitia kwa mzungu kwanza na ndio maana kajichimbia ubalozi wa M Dutch -Kaburu. Huyu mkuu ni MNYAPALA....pupet wa Muingereza.

Misinformation tena. Mdachi anauhusiano gani na kaburu? Au kwa vile boers walitokea huko miaka 400 iliyopita? Ulitaka Morgan akimbilie wapi? Waafrika wote wako upande wa Mugabe na unadhani Robert angesita kumfuata huko huko? Au ulitakaakimbilie kwa waingereza au wamarekani ili athibitishe hoja yenu kuwa yeye ni kibaraka wao? Amekimbilia kwa wadachi wewe bado umeona mkono wa muingereza!
 
Hapa kuna cheap politics za kiafrika nyingi sana. Tunaleta siasa za kaya kwenye siasa za kitaifa. Binafsi ninaelewa kuwa kwenye kaya yetu siwezi kumrushia madongo baba au babu yangu hata kama najua kuwa wanafanya makosa ya wazi kabisa. Hayo ndiyo tunataka kulazimisha katika kiwango cya kitaifa, kuwa baba au babu hafanyi makosa. Tanzania tulikuwa na bahati sana kuwa Nyerere alijuwa unyonge wetu na makosa yake hivyo akaamua kuachia ngazi kwa hiari yake. Kama angeamua kung'ang'ania madaraka kama babu hyu na sisi tungekuwa huko huko waliko wazimbabwe leo hii.
 
Sasa mbona mnatumia rangi kujenga hoja yenu? Au hao wazungu mnamaanisha na wengine walioamua kuhamia ulaya na marekani?

Usijifanye naive, Mkuu. Mjadala wote umesimamia rangi na post colonial rhetoric. Rangi in the racial context. Sasa katika postcolonial rhetoric moja ya nguzo ni kuziandika upya association zote zilizohusishwa na rangi nyeupe na waliotutawala. Ambazo nyingi ni negative. Blackmarket, Black plague, Black mail, dark as sin, black deeds etc etc. Na mitazamo kama hii ikapelekwa kwenye race relations; kama mambo yote maovu ni meusi basi wenye rangi hiyo ni waovu na lesser than walio weupe, rangi ya mbinguni! Makovu yaliyoachwa na hizi associations tunayo mpaka sasa. Dada zetu kutumia mkorogo kwa sababu the ideal ya uzuri katika western media ni weupe. Sasa leo nakushangaa armchair revolutionary unaposimama na kusema umechagua rangi nyeupe kukuonyesha usafi wa matendo yako. Kwa mtazamo huo una maana kuwa weusi hauwezi kuwa msafi?

Haujui unachokisema.

Kweli u-mugumu wa kuelewa! Pole!
 
Fundi Mchundo,

Mkuu ama kweli una cheap politics... Sasa unataka kusema uchaguzi wa rais Zimbabwe ni kati ya Mugabe na Morgan?... hii imenza lini ama unazungumzia kurudiwa kwa upigaji kura..Je, hizi mbinu za wazungu wamezianza majuzi baada ya uchaguzi?..ama nimesema wamezianza toka mwaka 2000 baada ya Mugabe kuchukua ardhi..na ndio sababu ya hapa tulipofika..wapo viongozi wengine kibao kwa nini usiwataje wale isipokuwa Mugabe tuuu umemshupalia kama vile ndio neno lilowekewa ubani. Hoja hujibiwa na hoja, wee sema mazuri ya Morgan kisha dhidi ya maneno yangu tutaendelea...
Hivi kweli unasoma nayoandika mkuu.
Ebu nikuulize tena kwa wale wanaosema Chadema haifai kuongoza ama Mbowe hafai wana maana kuwa wanampendekeza Kikwete kuwa ni bora na wanampigia debe..Haya nambie sisi tunaompinga Kikwete hivi sasa tunampigia debe nani maanake kuna watu wawili ktk ufahamu wako.... wapi na wapi mkuu!
Wee vipi soma maandishi ya watu na jaribu kuyaelewa kwanza.

Mkuu kama Kikwete na Lowassa ndio watabakia ktk uchaguzi wa rais Tanzania nitawapinga wote!.. nitayasema mabaya ya Lowassa kama atakuwa ktk nafasi ya Morgan na nitaendelea kumpinga Kikwete (Mugabe) kwa yale alokwisha yafanya!.. Hii ndio lugha yangu.. bado tu!
 
Fundi Mchundo,

Mkuu ama kweli una cheap politics... Sasa unataka kusema uchaguzi wa rais Zimbabwe ni kati ya Mugabe na Morgan?... hii imenza lini ama unazungumzia kurudiwa kwa upigaji kura..Je, hizi mbinu za wazungu wamezianza majuzi baada ya uchaguzi?..ama nimesema wamezianza toka mwaka 2000 baada ya Mugabe kuchukua ardhi..na ndio sababu ya hapa tulipofika..wapo viongozi wengine kibao kwa nini usiwataje wale isipokuwa Mugabe tuuu umemshupalia kama vile ndio neno lilowekewa ubani. Hoja hujibiwa na hoja, wee sema mazuri ya Morgan kisha dhidi ya maneno yangu tutaendelea...
Hivi kweli unasoma nayoandika mkuu.
Ebu nikuulize tena kwa wale wanaosema Chadema haifai kuongoza ama Mbowe hafai wana maana kuwa wanampendekeza Kikwete kuwa ni bora na wanampigia debe..Haya nambie sisi tunaompinga Kikwete hivi sasa tunampigia debe nani maanake kuna watu wawili ktk ufahamu wako.... wapi na wapi mkuu!
Wee vipi soma maandishi ya watu na jaribu kuyaelewa kwanza.

Mkuu kama Kikwete na Lowassa ndio watabakia ktk uchaguzi wa rais Tanzania nitawapinga wote!.. nitayasema mabaya ya Lowassa kama atakuwa ktk nafasi ya Morgan na nitaendelea kumpinga Kikwete (Mugabe) kwa yale alokwisha yafanya!.. Hii ndio lugha yangu.. bado tu!

Exactly Bob hapo ndipo unashindwa kumuelewa Fundi na wengine wenye mawazo yanayofanana fanana na ya kwake kama sisi. Hapa hakuna anayemtetea Morgan au ambaye anasema kwamba wazungu hawako culpable kwa matatizo ya Zimbabwe. No. Hapa tunaongelea ni jinsi gani Mugabe anavyowatreat wale wasiokubaliana na sera zake! wanaochomwa matako na kuuawa..siyo wazungu hata kidogo, na anayewachoma siyo Bush ni Mugabe na utawala wake.

Hili swala kitu ambacho Fundi amejaribu kukielezea hapa na wengine ni kwamba tunaangalia hali ilivyo kwa sasa. Ukiingiza uporaji wa mashamba sijui na mambo gani ya kihistoria we LOSE FOCUS of our arguments na Mugabe anataka topoteze mwelekeo wa arguments. Ndo maana wote wanaomtetea Mugabe..hawaongelei violence dhidi ya wananchi, bali wamejikita kwenye madhambi ya wazungu na mashamba! Kitu ambacho hakimsaidii mwananchi aliyechomwa moto na hana pesa ya kwenda hospitali!

Exactly thats what Mugabe wants. To cover his evil and terror against his opponents kwa kutumia historia!.. Kwa hiyo Mugabe anawachoma moto na kuwaua raia wake kwa kulipiza kisasi kwa wazungu? Hapana hili swala tuliangalie kama lilivyo. Huwezi kuua watu na kusponsor terror dhidi ya wapinzani wako kwa pretext ya HISTORIA jinsi ulivyonyanyaswa na wazungu. Sijui ni kitu gani BOB usichokielewa hapa.

Lastly, unaweza kumhukumu Morgan ambaye hata ikulu hajaingia? kwa nini tusiheshimu mawazo ya wazimbabwe..kumuingiza Morgan au Mugabe madarakani?..asipotimiza matarajio ya wazimbabwe ataondolewa after five years in a fair and periodic election! Thats our concern. Tumeyaona Malawi Muluzi aliingia kama hero after Kamuzu Banda but we have seen how HIS people have pushed him out. Zambia Chiluba aliingia baada ya Kaunda kama hero..but we have seen how people have kicked him out. So hata Zim, Morgan akipewa mandate na wananchi..akavurunda, basi watamtoa kwa amani....kwa hiyo wale waliompigia kura walitumwa na wazungu kwamba wampigie kura Morgan? si ni wazimbabwe kama walivyo wengine? Sasa kwa nini leo tumhukumu Morgan kama kibaraka wa wazungu? Simply because ame-elicit support ya wazungu na waafrika wengine kama akina Fundi na Masanja?

People, politics za Africa ni ngumu sana. Usipokuwa makini..utaona kwamba kila kitu ni conspiracy ya wazungu. Kitu ambacho siyo kweli! Leo tunaambiwa pesa za EPA, MEREMETA nk..ZILIMSAIDIA Muungwana kushinda..now hiyo pesa Mbowe, Mrema, Lipumba..wataitoa wapi? Think about it! Na hatuna hata sheria makini ya kuweka playing level field kati ya wagombea..sasa leo tunaambiwa kwamba wapinzani..ni vibaraka wa wazungu, bila kuhoja maneno ya wale wanaotwambia hivyo!

Kwa Tanzania, its perfect example..kama JK is screwing up..then lets Tanzanians decide in 2010 to let him pack. Simple. Lakini huu mtego wa kuwa-crucify wapinzani eti wanakuwa sponsored na outsiders, wakati incumbents walioko madarakani wanatumia resources za SERIKALI ni kutowatendea haki. Zanzibar..mpaka leo CUF inaonewa kwa BRAND YA UARABU maana kwa hoja CCM hawawezi kuwashinda. Kitu ambacho Fundi, mimi na wengine tumekataa kuingia kwenye huo mtego wa viongozi wetu wanafiki ambao wameishiwa hoja na baadala yake wameamua name calling ndo iwe silaha badala ya hoja.

Masanja,
 
Fundi Mchundo,

Mkuu ama kweli una cheap politics... Sasa unataka kusema uchaguzi wa rais Zimbabwe ni kati ya Mugabe na Morgan?... hii imenza lini ama unazungumzia kurudiwa kwa upigaji kura..Je, hizi mbinu za wazungu wamezianza majuzi baada ya uchaguzi?..ama nimesema wamezianza toka mwaka 2000 baada ya Mugabe kuchukua ardhi..na ndio sababu ya hapa tulipofika..wapo viongozi wengine kibao kwa nini usiwataje wale isipokuwa Mugabe tuuu umemshupalia kama vile ndio neno lilowekewa ubani. Hoja hujibiwa na hoja, wee sema mazuri ya Morgan kisha dhidi ya maneno yangu tutaendelea...
Hivi kweli unasoma nayoandika mkuu.
Ebu nikuulize tena kwa wale wanaosema Chadema haifai kuongoza ama Mbowe hafai wana maana kuwa wanampendekeza Kikwete kuwa ni bora na wanampigia debe..Haya nambie sisi tunaompinga Kikwete hivi sasa tunampigia debe nani maanake kuna watu wawili ktk ufahamu wako.... wapi na wapi mkuu!
Wee vipi soma maandishi ya watu na jaribu kuyaelewa kwanza.

Mkuu kama Kikwete na Lowassa ndio watabakia ktk uchaguzi wa rais Tanzania nitawapinga wote!.. nitayasema mabaya ya Lowassa kama atakuwa ktk nafasi ya Morgan na nitaendelea kumpinga Kikwete (Mugabe) kwa yale alokwisha yafanya!.. Hii ndio lugha yangu.. bado tu!

You make my day kila nikikusoma!
Haya sasa, Mkuu, niambie nani mwingine yuko kwenye kinyang'anyiro cha urais huko Zimbabwe zaidi ya Robert na Morgan? Ninachojua mimi, alikuweko makoni akatoka katika raundi ya kwanza! Sasa wewe usie na cheap politics, nieleze nani mwingine aliyebaki kushindana na Mugabe baada ya Morgan kujitoa? Mimi si mZimbabwe kwa hiyo ninaojua wanawafuasi wengi kule ni Morgan na Mugabe. Najua Mugabe ameua wengi. Sina taarifa ya Morgan kufanya hivyo. Kama wewe una taarifa nyingine, basi nifahamishe.

Rais wa Zimbabwe ninavyojua mimi ni mmoja (hapa tena unaweza kunisahihisha , oh most omniscient one), nae ni Robert Mugabe. As far as I am concerned the buck stops there when it comes to all the udhalimu na ukatili uliofanyika na dola wakati wa utawala wake dhidi ya raia wa Zimbabwe. Raia wa Zimbabwe kwa mtazamo mimi unajumuisha wale wenye rangi nyeupe, nyeusi, bluu na yeyote nyingine.

Unazidi kusogeza magoli. Haya ya Chadema yametoka wapi? Mfano sahihi ungekuwa CUF na CCM, Zanzibar. Kule kwa wenzetu ukisema hautaki Maalim aongoze maana yake ni kuwa wewe unataka CCM iendelee. Hauwezi ukamkataa Maalim, ukidai kuwa Mtikila anaweza kwenda kuongoza! Au mtu mwingine yeyote ambaye hayumo katika vyama hivyo viwili, CUF na CCM. Bara, suala la uongozi ni complicated maana wigo ni mkubwa zaidi, sio kama Zimbabwe au Zanzibar. Ndani ya hivyo vyama vyenyewe kuna watu kibao wameishaonyesha dhahiri nia yao ya kuchukua uongozi. Kwa hiyo unaweza ukasema haumtaki Mbowe heri Chacha, Zitto, Slaa na kadhalika na watu wasishangae.

Utalinganishe Kikwete na Lowassa na Robert na Morgan? Au, mkuu, una za ndani zinazosema kuwa Lowassa ametoka CCM? Au Kikwete?

Naona kuna haja ya kwenda kutafuta maana ya neno convoluted maana naona haulielewi. Ubishi unaoleta ni wa kijiweni, nani mwenye sauti ya juu au kusema sana ndiye anaonekana mjuzi.

Nimekuuliza swali dogo, kwa vile waliobaki kwenye ballot ni Mugabe na Morgan, ungekuwa wewe ungempigia kura nani? Mugabe ambaye umemwita ni muuaji au Morgan ambaye ni kibaraka? Mimi ningempigia Morgan. Mwenzangu mbona unapata kigugumizi? kwangu mimi Uzuri wa Morganni mmoja tu, kuwa yeye siye Mugabe!

Amandla.....
 

Mkuu hapa tuko pamoja. Ndo hapo tunapoona kwamba the current system we have is not working, lakini wale wanaojaribu kuibadilisha ndo tunawacrucify kama vibaraka.. Jamani ni nchi gani mpinzani atashindana na incumbent asionekane msaliti na kibaraka wa wazungu? Thats exactly what our leaders want us to believe. Sasa tusilaumu tuu, lets give alternative basi! Nani atatukomboa? au kila mtu mwenye mapenzi mema na Africa lazima aje kwenye platform ya ant western? ndo atakubalika?

Hapana, Nimekataa na nimechoka kudanganywa!
 
..hivi hiyo resentment ya Mugabe kwa Tsvangarai inayoonekana kuungwa mkono na wengi kwamba hakuwa mpigania uhuru, ndio sababu tosha ya kutokubalika Morgan kuwa raisi Zimbabwe? au ni hili;

...But his break with Mr Mugabe came over an issue that he may now prefer to forget. The president reluctantly embraced the free market in 1991 by accepting a structural adjustment programme from the International Monetary Fund.

Mr Tsvangirai accused him of using workers as "sacrificial lambs" and led a series of protests. He was jailed for six weeks on trumped-up charges of being a South African spy. This intense, personal duel helps to explain Mr Mugabe's loathing for Mr Tsvangirai.

A man 28 years his junior who played no part in the liberation war took on the president for six crucial months in 1997-98 and forced him to retreat.

...isije ikawa kama msemo wa 'balahau' hatakuja tawala unguja sababu 'wao' (wapemba...aka waarabu!) habari ya mapinduzi walipelekewa tu asubuhi kumekucha.

Yale yale...'suspicious minds', unajitisha mpaka unaogopa kivuli chako!
 
Masanja,
Hapa mkuu na wewe unapindisha issue,
Ni wapi nilipopinga hoja ya Fundi Mchundo inayohusiana na Mugabe?.. na kama hakuna imekuwaje tuendelee kubishana ikiwa kweli huyu mtu hafikirii kuwa mimi namtetea Mugabe naposema mabaya ya Morgan na uhusiano wake na wazungu..
Pili, nimesema toka mwanzo kuwa Zimbabwe singekuwa hii leo kama sio swala la Ardhi na nimewatajia kuwa MDC ilianzishwa toka swala hili lilipofikia hatma yake kuwa Mugabe angechukua ardhi hiyo.. Ni lazima tutazame source ya mambo yote haya ili niweze kujenga hoja kuhusiana na wazungu/Morgan. Mada hii inawahusu wazungu na kampeni zao kuhakikisha Morgan ndiye chaguo la wananchi.
Na laukama Morgan atachukua nchi basi kitu cha kwanza ni kurudisha ardhi ya wazungu jambo ambalo litaleta mgogoro zaidi na pengine vita ya wenyewe kwa wenyewe kama inavyotokea nchi nyinginezo, na mifano kibao nimetoa lakini bado mmeshupalia mapenzi yenu kwa wazungu..

Hakuna hata sehemu moja ambayo sikufahamu Fundi Mchundo alichosimamia, na wala sidhani kuna mtu humu anapenda kile kinachotokea leo huko Zimbabwe isipokuwa mimi natazama nyuma, hapa tulipo na mbele jambo ambalo kwenu halina msingi isipokuwa kumtetea Morgan, Na hakuna hata sehemu moja sii Fundi Mchundo ama wote wanaompinga Mugabe wamesema wazi kuwa Morgan pia hafai kwa sababu wao wana ona watu wawili tu hapa!..Na wanasisitiza mzungu awekwe nje ya swala hili kama vile dhambi kuwahusisha Marekani na Iraq!.
Bila shaka Mugabe anasema ukweli pamoja na kwamba yeye mwenyewe ni mshenzi, ukweli ambao nyie hamtaki kuukubali kwa sababu unamhusu mzungu - Mtawala wenu. hapa issue ni mzungu tu na ndio kichwa cha mada hii hakuna jingine, kwani zipo mada zinazozungumzia Zimbabwe nje ya mchango wa mzungu... hunioni kule kwa sababu nakubaliana na hoja za wachangiaji..

Na kama unabisha maneno yangu nionyeshe wewe wapi umezungumzia mapungufu ya Morgan na kama unakubali mchango wa Muingereza ktk nchi huru ya Zimbabwe - if not why?
Acheni ushabiki wenu wa Yanga na Simba mimi natazama mpira huu unavyokwenda na sizipendi timu zote!...
 
Ladies and Gentlemen...our episode today...after that of Charles Taylor....hahahahah...it's non other than Robert Mugabeeeeeeeee....clap clap clap....A superstar from Zimbabweee.....
Welcome to The Hague...
 
Mchongoma,
Mimi nilikataa hata kuwepo kwa Muafaka kati ya Mugabe na Morgan kwa sababu hawa jamaa wote ni bomu!..Never make a deal with a devil! labda wewe pia uwe ni mfano wake.. Na ndicho nachokiona hapa.. trust maneo yangu UK hawatakubali kabisa muafaka kati ya Mugabe na Morgan kwanza wamekwisha kumpoa warning siku za nyuma - Ushindi wa Morgan ni lazima...
Kwa kutazama mbele nchi hiyo imekwisha! huu ni mwanzo tu!..Mtakuja nambia.... Oooh bila shaka nitawakumbusha iwe kijiwe hiki ama chochote..
 
Masanja,
Hapa mkuu na wewe unapindisha issue,
Ni wapi nilipopinga hoja ya Fundi Mchundo inayohusiana na Mugabe?.. na kama hakuna imekuwaje tuendelee kubishana ikiwa kweli huyu mtu hafikirii kuwa mimi namtetea Mugabe naposema mabaya ya Morgan na uhusiano wake na wazungu..
Pili, nimesema toka mwanzo kuwa Zimbabwe singekuwa hii leo kama sio swala la Ardhi na nimewatajia kuwa MDC ilianzishwa toka swala hili lilipofikia hatma yake kuwa Mugabe angechukua ardhi hiyo.. Ni lazima tutazame source ya mambo yote haya ili niweze kujenga hoja kuhusiana na wazungu/Morgan. Mada hii inawahusu wazungu na kampeni zao kuhakikisha Morgan ndiye chaguo la wananchi.
Na laukama Morgan atachukua nchi basi kitu cha kwanza ni kurudisha ardhi ya wazungu jambo ambalo litaleta mgogoro zaidi na pengine vita ya wenyewe kwa wenyewe kama inavyotokea nchi nyinginezo, na mifano kibao nimetoa lakini bado mmeshupalia mapenzi yenu kwa wazungu..

Hakuna hata sehemu moja ambayo sikufahamu Fundi Mchundo alichosimamia, na wala sidhani kuna mtu humu anapenda kile kinachotokea leo huko Zimbabwe isipokuwa mimi natazama nyuma, hapa tulipo na mbele jambo ambalo kwenu halina msingi isipokuwa kumtetea Morgan, Na hakuna hata sehemu moja sii Fundi Mchundo ama wote wanaompinga Mugabe wamesema wazi kuwa Morgan pia hafai kwa sababu wao wana ona watu wawili tu hapa!..Na wanasisitiza mzungu awekwe nje ya swala hili kama vile dhambi kuwahusisha Marekani na Iraq!.
Bila shaka Mugabe anasema ukweli pamoja na kwamba yeye mwenyewe ni mshenzi, ukweli ambao nyie hamtaki kuukubali kwa sababu unamhusu mzungu - Mtawala wenu. hapa issue ni mzungu tu na ndio kichwa cha mada hii hakuna jingine, kwani zipo mada zinazozungumzia Zimbabwe nje ya mchango wa mzungu... hunioni kule kwa sababu nakubaliana na hoja za wachangiaji..

Na kama unabisha maneno yangu nionyeshe wewe wapi umezungumzia mapungufu ya Morgan na kama unakubali mchango wa Muingereza ktk nchi huru ya Zimbabwe - if not why?
Acheni ushabiki wenu wa Yanga na Simba mimi natazama mpira huu unavyokwenda na sizipendi timu zote!...

Sasa tuko upande mmoja? Haya, ulishasema wewe ni mswahili!
Mbona hutaki kujibu, wanaogombea uchaguzi huko Zimbabwe ni nani na nani? Morgan, amejitoa, nani mwingine alikuwa kwenye ballot? Morgan ana matatizo yake lakini hata siku moja hauwezi kuyalinganisha na ya Mugabe. Tuhuma zako zote ni kuwa ni kibaraka. Kiongozi gani wa Afrika asiye kibaraka kwa mtazamo huo? Mugabe anabebwa na Afrika Kusini na China, unadhani anaweza kutamka lolote hadharani dhidi ya Mbeki na utawala wa China? Ninachopingana na wewe ni kuendelea kumfananisha muuaji na kibaraka ambaye hata utawala haja uonja.
 
Masanja,
Nimekujibu kipande cha kwanza sasa naingia cha pili na nitakupa mifano hai..
Siku za nyuma kulikuwa na mjadala hapa kuhusiana na Chadema hasa uhusiano wao na Conservative cha Uingereza..Hii ilikuwa big issue kwangu ambayo haitakiwi kusubiri uchaguzi wa wananchi Wadanganyika ati tuwape ushindi Chadema kwa miaka mitano kama unavyofikiria wewe ,No way mkuu, kama Chadema hawafai kwa kujihusisha na mipango ya wazungu inabidi tuwatoe katika hesabu kwa sababu utawala wa nchi sio uwanja wa majaribio..Na lazima tuwalaumu Uingereza kwa kutaka kuingilia Uhuru wa Tanzania kutuwekea vibaraka wao kama Iraq na Afhganstan..

Kwa sababu lilikuwa jambo zito kwangu, nilipata maelezo toka kwa baadhi wanachama viongozi wa chama hicho hapa kijiweni.. na wengine tuliwasiliana kwa PM hadi nikafikia kuamini waliyoyasema mbali na uchunguzi wangu binafsi. Kuna issue za Ukabila na mengine mengi ambayo hayawezi kupita tuu..Leo hii tunaona uongozi wa Kikwete ulivyokamatwa ati tumwache hadi 2010, then hiki kijiwe cha nini?..kwa nini tupo hapa kama hatutazami kote, Na itakuwa ujinga ulioje kama Lowassa atapita kuwa mgombea wa rais tumwache kumhusisha na scandal zote ati kwa sababu ni chaguo la wananchi waliolala...sababu yetu kubwa ati hajawahi kuwa rais!... Huu ni upumbavu mkubwa sana, samahani lakini kwa kutumia lugha hiyo..yaani inanipa ile luigha ya Ndivyo tulivyo!..sisi hapa tumeamua kuwa tofauti na wengi wadanganyika na tunapashana mabaya yote yanayotufika na kuangalia mbele ya safari yetu.. future ya nchi yetu ndio muhimu kwanio kinachotokea leo na kesho ndicho kitakachotuhumu..
Kikwete anatumiwa na kina Sinclair na inazungumzwa hapa hakuna mtu anayemtetea Sinclair hata kidogo, tunazungumzia uwekeshaji na jinsi wageni wanavyopora mali zetu, hili ni funzo kwetu sote na hatutapenda kiongozi mwingine atakaye tupeleka pabaya zaidi ati kwa sababu tu anapata support kubwa...

Fundi Mchundo,
Mada hii haizungumzii uchaguzi huu, na hatupo hapa kulinganisha wahalifu.. nimesema toka mwanzo hili sio swala la kuruka mkojo kukanyaga mavi.. huko sipo hawa wote ni viongozi wabaya, washenzi na hawawezi kumsaidia Mzimbabwe zaidi ya kuhatarisha zaidi maisha ya Wazimbabwe...Ajabu unasema hakuna kiongozi Afrika ambaye sio kibaraka... so unachosema ni poa tu kuiwa na kibaraka!.. hii kweli sio viongozi wetu kuwa reflection yetu sisi wenyewe?..
 
Mkandara.
Kumkosoa Kikwete ni tofauti na kusema SIKUBALI awe rais mwaka 2010! Vilevile kwa Mbowe. Vile vile kwa Mrema. Ni haki ya wanachi wa Tanzania kuchagua rais wanayemtaka bila kulazimishwa kwa bakora na vinginevyo. Ubabe ukitumiwa,unatia wasiwasi legitimacy ya huyo atakayeshinda. Haya tunayaona Zanzibar.

Sasa wewe kwa kusema HAUTAKUBALI ushindi wa Morgan ni hayo hayo. Pamoja na kutompenda na kumkubali Mugabe mimi binafsi, kama wananchi wa Zimbabwe kupitia uchaguzi ulio wazi na haki, wakiamua ndiye anayewafaa, sitakuwa na ubavu wa kutomtambua kama rais. Nitaendelea kumchukia lakini nitamtambua kama kiongozi halali. Tunachokisikia kutoka kwenu ni dhana ileile ya Mugabe kuwa piga uwe Morgan hawezi kuwa rais wa Zimbabwe. Hicho ndicho ninachokipinga. Kila dalili zinaonyesha kuwa Robert amefanya usanii mkubwa( kucheleweshwa kwa matokeo n.k.) na ukatili dhidi ya wananchi wake kuhakikisha kuwa hilo halitokei. Wewe yote haya hauyaoni, unabaki kung'ang'ania kuwa Morgan ni kibaraka? So what? Mbona wamarekani walimchagua George W mara mbili?
 
Fundi Mchundo,
Haya umerudi kule kuleee! nani anazungumzia kupigwa watu bakora?.. issue ni source na jinsi mzungu anavyoingilia hapa. Sudan wanapigwa, Kenya walipigwa, Tanzania wamepigwa,.. mbona BBC na CNN hazizungumziii huko ama ndio kusema wale ni less evil kuliko Mugabe?.. nachosema mimi mbali na uabay wa Mugabe, wazungu wana interest zao Zimbabwe do you agree?. ukisema ndio tumemaliza..
Na kuhusu swala la Mugabe kuwa kiongozi mbovu muuaji nimesema mara mia kidogo kuwa YES! na mwenyewe huko nyuma ume acknowledge kuelewa lakini bado unarudisha swali lile lile bila kujibu yangu...Mugabe ni mbovu, mshenzi na matusi tumpe lakini kuna mkono wa mzungu ktk haya yote, mzungu hutetea nchi zinazokubaliana naye (kwa maslahi yake) kama ilivyo Sudan ambako kiongozi wao hana tofauti na Mugabe..
 
Fundi Mchundo,
Haya umerudi kule kuleee! nani anazungumzia kupigwa watu bakora?.. issue ni source na jinsi mzungu anavyoingilia hapa. Sudan wanapigwa, Kenya walipigwa, Tanzania wamepigwa,.. mbona BBC na CNN hazizungumziii huko ama ndio kusema wale ni less evil kuliko Mugabe?.. nachosema mimi mbali na uabay wa Mugabe, wazungu wana interest zao Zimbabwe do you agree?. ukisema ndio tumemaliza..
Na kuhusu swala la Mugabe kuwa kiongozi mbovu muuaji nimesema mara mia kidogo kuwa YES! na mwenyewe huko nyuma ume acknowledge kuelewa lakini bado unarudisha swali lile lile bila kujibu yangu...Mugabe ni mbovu, mshenzi na matusi tumpe lakini kuna mkono wa mzungu ktk haya yote, mzungu hutetea nchi zinazokubaliana naye (kwa maslahi yake) kama ilivyo Sudan ambako kiongozi wao hana tofauti na Mugabe..

Bob, now you are getting it...

Sasa kama Sudan, Kenya et al wanakufa..tukae kimya tuu kwa sababu hata kwingine wamekufa na mzungu hakuingilia au CNN haikupiga kelele? Yes, Darfur watu wanakufa kama nzi na mateso ni mengi, so is Congo, so is Somalia so is Chad...the list is endless.....so what? tukubali watu wafe na kwingine simply because hata kwingine wanakufa? and guess what? who is killing people in Darfur? Ila its easy kwa Bashir kusema ni wazungu wanataka mafuta! na sisi wananchi tunakubali. as simple as that! Hatuulizii the other side of the coin...marginalization ya Darfurians, ambavyo wameteswa na tawala mbali mbali za Sudan, ambavyo watoto wao mpaka leo madarasani hawafundhwi anything than Quran! list ya madhambi haiishi! ..lakini tunakubali kuchuka majibu ya mkato kutoka kwa watwala hawa dhalimu wa Afrika...akina BASHIR! Talk of the African solutions for African problems!

Mzungu ana maslahi yake Zimbabwe hilo halina ubishi. Swali letu, je hayo maslahi ndo yanamfanya Mugabe awatreat wananchi na wale wanaompiga namna hii? (to kill, maim..name them..?) na kama sivyo...what should we do? Ni ukweli mzungu ana maslahi yake na hii siyo Zimbabwe tuu..ni Afrika nzima! lakini je sisi kama waafrika, tumeshalijua hilo, sasa tufanye nini? ndo tunaulizana hapa! Au APPROACH Mugabe anayoitumia kuwanyanyasa wapinzani wake ndo sahihi ya kupambana na hawa mabeberu?

Ubeberu ni global issue! Lakini je tukiua watu wetu ndo itasaidia? NA KWA NINI UTUFANYE TUAMINI KWAMBA MORGAN AKIRUDI MADARAKANI ATARUDISHA MASHAMBA KWA WAZUNGU? HIYO THEORY YAKO INA TOFAUTI GANI NA ULE MSEMO WA CCM KWAMBA KUPIGIA KURA UPINZANI TANZANIA NI KUKARIBISHA VITA KAMA BURUNDI AU CONGO? HAPANA MKUU POLITICS OF FEAR HAVE NO PLACE AT LEAST HAPA KWENYE JAMVI LA WASOMI KAMA JF...
 
...Kwa vyovyote Mugabe anaonekana Tyrant!, hayo matamshi ya vitisho alivyowatolea MDC, au kwakuwa yeye amekamata Mpini, MDC wamekamata makali ndio maana inaonekana sio uchochezi?

"We shall never, never accept anything that smells of ... the MDC. These pathetic puppets taking over this country? Let's see. That is not going to happen," Mugabe said in a speech at the burial of a former army general.

"We are prepared to fight for it (Zimbabwe) if we lose it in the same way that our forefathers lost it," he said, referring to British colonial rule.

Tyrant; The term carries modern connotations of a harsh and cruel ruler who places his or her own interests or the interests of a small oligarchy over the best interests of the general population which the tyrant governs or controls (http://en.wikipedia.org/wiki/Tyrant)

...Njia pekee ambayo ingemuokoa Mugabe ni pale tu angekubali kung'atuka. Kinyume na hapo ni kung'ang'ania madaraka, ingawa mbele ya uso wa dunia inaonekana dhahiri utawala wake ni wa kimabavu na wananchi wanaathirika kwa kiwango kikubwa, hasa wale wanao support opposition.
 
Back
Top Bottom