Wenye magari namba (A) tuwe waungwana tuyatoe barabarani ili TRA warudi kusajili (A) tena itakapo jaa namba D

Huu mji unashangaza kuna magari no C na D yamechoka sana na kuna Land cruiser no A na B bado zinawaka sana hasa V8
It's simple, wenye gari kubwa most likely wana magari madogo kwa hiyo hizo V8 hazitembei kila siku, lakini pia ukiendesha gari ya thamani lazima zile rough za barabarani utaachana nazo. Hizi "baby walker" ndio bingwa wa rough..
 
Kuna mtu ana gari namba A na alinunuaga Toyota motors,na mpk leo hizo gari namba D
Haifiki...

Ova
 
Uchakavu unapimwa kwa vitu vingi! Na sioni sababu ya kupaniki kama gari litagundulika linafaa, litabandikwa plate nyekundu ili kutofautisha na (A) mpya!

Lengo pia ni kufunya clean sheet namba A!

Tunahitaji kama inchi kuwa na mkakati wa sheria ya uchakavu, mazingira na usalama wa watu
Unanunua gari yard used unaliona jipya mzee
Wakati ni chakavu bado

Ova
 
Jamaa Nadhan ni ama ana kagari kapya ka number D Sasa anaona kanaenda jusound vibaya ndo maana anapambania karudi

IFIKE HATUA VIONGOZI WATOKE KATIKA LOYALTY FAMILY TU HAWA WATOTO WA MASKIN HAWAFAI HATA KIDOGO AISEE
Ni kweli.

Viongozi waliotoka kwenye familia za kimasikini kama JPM ndo wanaoleta hoja za ajabu ajabu
 
Katika utaratibu wa maisha Africa inabidi tujifunze kujiwekea kikomo!

Ili tuendane na ulimwengu lazima tujifunze kubadilika!

Nikimnukuu bwana Newton mwanasayansi msomi aliwahi kusema kwamba (Kila kitu hubaki kilivyo au kwenye mwendo hadi pale nguvu hasi itakapotumika)

Hii inamaanisha kwamba afrika tutaendelea kuwa hivi hivi hadi pale nguvu nyingine itaamua vinginevyo!

Afrika huwa hatuna mda kabisa wa kuzingatia uchakavu (expire date)!

Hatuzingatii uchakavu kuanzia vyakula, mapenzi na vitu vingine yabisi hadi pale tunakumbana na madhara! (Sitachimba sana huku)

Tukirudi kwenye gari na vyombo vya moto!
Huko yanapotengenezwa magari mfano Japan na kwingineko!

Ziko taratibu walizojikwekea kwamba gari ikifikia kiwango flani cha matumizi iondolewe barabarani!

Na ndiyo maana japani ukiwa na hata laki nane unapata gari kari!

Lakini likifika afrika huwa ni Jipya!

Sasa basi, magari yanayoingia inchini husajiliwa na mamlaka ya TRA kwa alphabet kimahesabu ya probability/possibility!

Magari yaliyotumiwa huko inje miaka hiyo, yakafika Tanzania na kusajiliwa namba TZ na baadae kuhamia usajili mpya wa namba (A) hakika yatakuwa yamezeeka sana!

Kama kweli tunajali afya za watu hayo magari yangeondolewa barabari! TRA wasihamie namba E bali waangalie namna ya kuondoa (A) ili waanze upya!

Tunajaza sever za TRA pasipo sababu ya msingi na minamba kibao!

Utafiti unaonesha kama TRA itahamia namba (E) itachukua karibu miaka 8-10 kufikia kujaa!

Rai yangu kwa serikali, kama ilivyofanya kurudia usajili wa laini za simu!
Basi isione tabu kufuta usajili wa magari namba (A)
Serikali ni afadhali ipunguze ushuru wa kuagiza magari Japan lakini ifute usajili wa magari namba (A) ili kubalance life cycle ya magari Tanzania! Iwe (A to D)

Na kwa Yale namba (A) yatayobainika yanaubora wa kiwango cha kubaki, walipie gharama annually na wabadilishwe rangi ya plate number, isomeke namba (A) lakini plate nyekundu (namba maalum)

Mkishindwa hilo, wekeni hata utaratibu wa kila gari kuwa na umri wake wa kutembea!

Nasema hivi kwasababu zipo gari hapa bongo hata akiiona mjapani atakataa kuwa hakuitengeneza yeye!

Yaani gari Kuanzia injini imebadilishwa, gearbox nyingine, kila kitu kimebadilishwa!

Pia Hii inachangia hadi wizi wa spea kuongezeka!

Sioni sababu ya kuhamia namba (E) na kuiacha (A) ikiteketeza dunia kwa uchakavu!

Huna hoja mkuu. Gari ni modular. Gari ni service.

Kama modular kitu kinachoharibika kinaweza kurejelewa na kipya chenye ubora zaidi.

Gari ni mfuko wako jombi.

Kuna magari registered AAA bora kabisa kuliko DZZ.

Tembea uone.
 
Nguo pia Zina expiry date ni musimu mfano msimu wa baridi ukiisha unapoanza msimu wa joto unatakiwa kutupa wewe mleta mada nguo zako vipi?

Njia nyingine kujua hutakiwi kuendelea kuvaa hiyo nguo Ni je umeifua nguo Mara ngapi ukiifua Mara 20 au ina miezi mitano ya kuwa nayo kizungu shelf life hata Kama umeifua Mara 10 tu unatakiwa uitupe ndio maana huweko kitu kinaitwa sale unanunua nguo iliyokaa muda mrefu kwenye shelf wewe mwenzetu vipi? Kanguo tu ka ndani umekafua au uko nako muda gani Sasa? na bado umekakomalia tu

Ukiondoa mitumba asilimia kubwa ya wananchi watatembea uchi
Kweli saa mbovu pia huwa sahihi mara mbili kwa siku 😂😂😂😂
Hata wewe leo unaonekana kuwa na akili timamu
 
Mke wangu wa kambo (mchepuko wangu) alipopata mimba alichukia sana bukima (ugali) nikamzoesha kula mserebende (samaki ndogondogo). Nahisi mtoa mada nawe upo katika hali hiyo, au umeingia joto hivyo unachukia kitu kinachpitwa "A". Sijui tukuzoeze nini .....
 
mtoa mada huna akili gari zenye namba A nyingi ni nzima na imara utafikiri kanunua leo lakini kuns magari namba D zimechakaa
 
upuuzi kama huu alianzisha zungu......ukatembea weeeeee.....nchemba akauokota......akampelekea sasha......wanaumia ni wale WATANZANIA halisi wenye kipato cha kuunga unga.......namba ni namba.......gari bovu halitembei...ukiliona juwa liko zima.....TANZANIA ni TAJIRI kiasilia....MASKINI kiuhalisia....kaka mkubwa kama wewe uko njema, endelea kufaidi matunda yako...tuachie vigari vyetu vya namba A....... cha kwangu nimenunue 2002......kinapumua vema bro...na bado sana...nimeoa na festi boni anakiendesha mno....na kila kilismasi kinaenda kutalii mjini moshi......
 
Nimeibiwa kifaaa pale dodoma jamaa kaemda na gRi garage kaenda kuchokonoa kwenye mfumo wa maji
Katika utaratibu wa maisha Africa inabidi tujifunze kujiwekea kikomo!

Ili tuendane na ulimwengu lazima tujifunze kubadilika!

Nikimnukuu bwana Newton mwanasayansi msomi aliwahi kusema kwamba (Kila kitu hubaki kilivyo au kwenye mwendo hadi pale nguvu hasi itakapotumika)

Hii inamaanisha kwamba afrika tutaendelea kuwa hivi hivi hadi pale nguvu nyingine itaamua vinginevyo!

Afrika huwa hatuna mda kabisa wa kuzingatia uchakavu (expire date)!

Hatuzingatii uchakavu kuanzia vyakula, mapenzi na vitu vingine yabisi hadi pale tunakumbana na madhara! (Sitachimba sana huku)

Tukirudi kwenye gari na vyombo vya moto!
Huko yanapotengenezwa magari mfano Japan na kwingineko!

Ziko taratibu walizojikwekea kwamba gari ikifikia kiwango flani cha matumizi iondolewe barabarani!

Na ndiyo maana japani ukiwa na hata laki nane unapata gari kari!

Lakini likifika afrika huwa ni Jipya!

Sasa basi, magari yanayoingia inchini husajiliwa na mamlaka ya TRA kwa alphabet kimahesabu ya probability/possibility!

Magari yaliyotumiwa huko inje miaka hiyo, yakafika Tanzania na kusajiliwa namba TZ na baadae kuhamia usajili mpya wa namba (A) hakika yatakuwa yamezeeka sana!

Kama kweli tunajali afya za watu hayo magari yangeondolewa barabari! TRA wasihamie namba E bali waangalie namna ya kuondoa (A) ili waanze upya!

Tunajaza sever za TRA pasipo sababu ya msingi na minamba kibao!

Utafiti unaonesha kama TRA itahamia namba (E) itachukua karibu miaka 8-10 kufikia kujaa!

Rai yangu kwa serikali, kama ilivyofanya kurudia usajili wa laini za simu!
Basi isione tabu kufuta usajili wa magari namba (A)
Serikali ni afadhali ipunguze ushuru wa kuagiza magari Japan lakini ifute usajili wa magari namba (A) ili kubalance life cycle ya magari Tanzania! Iwe (A to D)

Na kwa Yale namba (A) yatayobainika yanaubora wa kiwango cha kubaki, walipie gharama annually na wabadilishwe rangi ya plate number, isomeke namba (A) lakini plate nyekundu (namba maalum)

Mkishindwa hilo, wekeni hata utaratibu wa kila gari kuwa na umri wake wa kutembea!

Nasema hivi kwasababu zipo gari hapa bongo hata akiiona mjapani atakataa kuwa hakuitengeneza yeye!

Yaani gari Kuanzia injini imebadilishwa, gearbox nyingine, kila kitu kimebadilishwa!

Pia Hii inachangia hadi wizi wa spea kuongezeka!

Sioni sababu ya kuhamia namba (E) na kuiacha (A) ikiteketeza dunia kwa uchakavu!
 
Mleta mada atakuwa afisa wa serikali entitled kigari kipya Cha serikali au wake entitled kukopeshwa vigari vipya na serikali .Hai huwa Ni wale akina maskini akipata ma Nani hii hulia mbwata!

Anaiona dunia yoote yake na wengi huwa wale waliezaliwa familia maskini Sana halafu wakafika hizo level za uafisa serikalini .Huwa jeuri na washamba na wajinga jinga fulani hivi .

Wangekuwa sekta binafsi asingeandika hii hoja.Hoja Kama hi inaletwa na malofa wa porini waliopewa vimadaraka serikalini

Ukisoma between the lines unajua kabisa mwandishi anatokea familia maskini Ila kwa Sasa ana ka position koko
Umempa credit ambazo hana. Hawa ndo wale wanaopewa bundle na waume wa dada zao hana cha kuandika cha maana. Hata gari hajui kitu huyu. Ni akina na mimi nimo jf. Plate no na uchakavu wapi na wapi!
Walioko level ya kumiliki magar wanajua matatizo ya msingi kama kodi kubwa, urasimu ukaguzi nchini kupitia tbs, upotevu wa vifaa vya magari bandarin, sheria kuruhusu magari ya umeme na solar,
 
Back
Top Bottom