TRA: Kufuta Usajili wa Vyombo vya Moto

TRA: Kufuta Usajili wa Vyombo vya Moto

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,900
Reaction score
52,051

Kufuta Usajili wa Vyombo vya Moto​


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwajulisha watu wote wanao miliki vyombo vya moto (magari, matrekta, pikipiki na matela) ambavyo havipo tena barabarani au haviwezi tena kurudi barabarani kwa sababu ya uchakavu, kuwasilisha maombi yao TRA ya kuvifuta kwenye usajili.

Kwa mujibu wa Kanuni Namba 177 ya mwaka 2001 ya Sheria ya Usalama Barabarani ya Mwaka 1973 kinamtaka mwenye chombo cha moto ambacho hakifai kuwa barabarani kuomba kufutwa kwenye usajili wa magari

Mwongozo:

1. Mmiliki atatakiwa kwenda Ofisi ya Usalama Barabarani (Polisi) kwa ukaguzi wa chombo cha moto na kupata cheti cha ruhusa ya kufuta usajili

2. Mmiliki atatakiwa kuwasilisha barua ya maombi ya kufuta usajili ofisi ya TRA iliyokaribu ikiambatanishwa na kadi halisi ya gari na cheti kutoka ofisi ya usalama barabarani

3. Baada ya TRA kuridhika na taarifa zilizowasilishwa maombi yatakubaliwa na chombo husika kitafutwa kwenye usajili na mmiliki atapewa cheti kuthibitisha kufutwa kwa chombo husika

Lengo:
Lengo la tangazo hili ni kuwahimiza wenye vyombo vya moto ambavyo haviko barabarani kuwasilisha maombi ya kufuta usajili haraka ili Serikali iwe na kumbukumbu sahihi ya idadi ya vyombo vya moto vinavyotembea barabarani kwa ajili ya kurahisisha mipango yake ya maendeleo ya taifa
 
Naskia Japan kuna ukomo wa kilomita za vyombo vya moto. Zikiisha hizo kilomita basi chombo cha moto hakiruhusiwi barabarani. Lengo la kufanya hivyo ni kuhifadhi mazingira.

Ukija huku kwetu (TZ), mambo ni tofauti. Unakuta gari au pikipiki ya miaka mingi na kilomita kibao ila ipo barabarani.

Sasa, je, kuna ubaya gani kwa hapa Tanzania magari namba A yakaondolewa barabarani?

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 

Kufuta Usajili wa Vyombo vya Moto​


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwajulisha watu wote wanao miliki vyombo vya moto (magari, matrekta, pikipiki na matela) ambavyo havipo tena barabarani au haviwezi tena kurudi barabarani kwa sababu ya uchakavu, kuwasilisha maombi yao TRA ya kuvifuta kwenye usajili.

Kwa mujibu wa Kanuni Namba 177 ya mwaka 2001 ya Sheria ya Usalama Barabarani ya Mwaka 1973 kinamtaka mwenye chombo cha moto ambacho hakifai kuwa barabarani kuomba kufutwa kwenye usajili wa magari

Mwongozo:

1. Mmiliki atatakiwa kwenda Ofisi ya Usalama Barabarani (Polisi) kwa ukaguzi wa chombo cha moto na kupata cheti cha ruhusa ya kufuta usajili

2. Mmiliki atatakiwa kuwasilisha barua ya maombi ya kufuta usajili ofisi ya TRA iliyokaribu ikiambatanishwa na kadi halisi ya gari na cheti kutoka ofisi ya usalama barabarani

3. Baada ya TRA kuridhika na taarifa zilizowasilishwa maombi yatakubaliwa na chombo husika kitafutwa kwenye usajili na mmiliki atapewa cheti kuthibitisha kufutwa kwa chombo husika

Lengo:
Lengo la tangazo hili ni kuwahimiza wenye vyombo vya moto ambavyo haviko barabarani kuwasilisha maombi ya kufuta usajili haraka ili Serikali iwe na kumbukumbu sahihi ya idadi ya vyombo vya moto vinavyotembea barabarani kwa ajili ya kurahisisha mipango yake ya maendeleo ya taifa
Sasa kazi, itabidi niwapelekee injinibloki kwani mabati niliuza kwa chuma chakavu.
 
Naskia Japan kuna ukomo wa kilomita za vyombo vya moto. Zikiisha hizo kilomita basi chombo cha moto hakiruhusiwi barabarani. Lengo la kufanya hivyo ni kuhifadhi mazingira.

Ukija huku kwetu (TZ), mambo ni tofauti. Unakuta gari au pikipiki ya miaka mingi na kilomita kibao ila ipo barabarani.

Sasa, je, kuna ubaya gani kwa hapa Tanzania magari namba A yakaondolewa barabarani?

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Kuna ubaya gani namba A zikafutiwa usajili? Je, tutaendelea kuendesha vyombo vya moto chakavu mpaka lini?

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Naskia Japan kuna ukomo wa kilomita za vyombo vya moto. Zikiisha hizo kilomita basi chombo cha moto hakiruhusiwi barabarani. Lengo la kufanya hivyo ni kuhifadhi mazingira.

Ukija huku kwetu (TZ), mambo ni tofauti. Unakuta gari au pikipiki ya miaka mingi na kilomita kibao ila ipo barabarani.

Sasa, je, kuna ubaya gani kwa hapa Tanzania magari namba A yakaondolewa barabarani?

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Kuna gari zinaundwa Tanzania mpaka unataka tulingene, Wajapani wananunua gari za mtumba kwa uwingi kama Tanzania.
 
Kuna ubaya gani namba A zikafutiwa usajili? Je, tutaendelea kuendesha vyombo vya moto chakavu mpaka lini?

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Namba ya gari siyo ubovu wake, kuna watu wanamiliki magari zaidi ya kumi, unaweza kuna kuna Gari No A. lakini halitumii sana kuliko No D, hivyo No D linachoka na kuhitaji matengenezo kuliko lile A.
 
Naskia Japan kuna ukomo wa kilomita za vyombo vya moto. Zikiisha hizo kilomita basi chombo cha moto hakiruhusiwi barabarani. Lengo la kufanya hivyo ni kuhifadhi mazingira.

Ukija huku kwetu (TZ), mambo ni tofauti. Unakuta gari au pikipiki ya miaka mingi na kilomita kibao ila ipo barabarani.

Sasa, je, kuna ubaya gani kwa hapa Tanzania magari namba A yakaondolewa barabarani?

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Tz gari ya mwaka 2000 unaambiwa ni new model
 
Namba ya gari siyo ubovu wake, kuna watu wanamiliki magari zaidi ya kumi, unaweza kuna kuna Gari No A. lakini halitumii sana kuliko No D, hivyo No D linachoka na kuhitaji matengenezo kuliko lile A.
Basi tuangalie hata km. Magari yenye kilomita nyingi yaondolewe barabarani.

Mbona Japan magari ni mazima ila yanaondolewa barabarani kwa sababu ya km nyinhi?

Unajua sisi TZ hatujali kabisa afya. Unakuta gari linatoa moshi mweusi na lipo barabarani tu!

Nimejaribu kufanya utafiti. Magari mengi namba "AAA" ni ya zamani sana, na tena yana kilomita nyingi sana, hivyo yaondolewe kwani yanazalisha kiwango kikubwa cha hewa chafu!

Wachache sana wenye magari kumi mchanganyiko yaani namba "AAA" na namba "D". Wengi wenye namba "AAA" wanalo moja wanajikongoja nalo!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
L
Basi tuangalie hata km. Magari yenye kilomita nyingi yaondolewe barabarani.

Mbona Japan magari ni mazima ila yanaondolewa barabarani kwa sababu ya km nyinhi?

Unajua sisi TZ hatujali kabisa afya. Unakuta gari linatoa moshi mweusi na lipo barabarani tu!

Nimejaribu kufanya utafiti. Magari mengi namba "AAA" ni ya zamani sana, na tena yana kilomita nyingi sana, hivyo yaondolewe kwani yanazalisha kiwango kikubwa cha hewa chafu!

Wachache sana wenye magari kumi mchanganyiko yaani namba "AAA" na namba "D". Wengi wenye namba "AAA" wanalo moja wanajikongoja nalo!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Japan hawaindoi magari sababu ya KM nyingi wao wanaondoa gari barababrani sababu ni expensive ku maintain gari gharama za parking space lot, inspection ya gari kwa mwaka au miaka, etc
 
Back
Top Bottom