Napendekeza mfumo wa ‘Randomizer’ kwenye usajili wa ‘plate number’ za magari nchini

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,052
40,715
7E29CDF3-3DAD-4922-8216-F8CA046E4BED.jpeg

==========================

Badala ya mfumo wa sasa wa ‘TxxxAyy> TxxxByy > TxxxCyy > TxxxDyy , na sasa karibia tunaingia namba ‘E’ , ambapo mtu anakuwa anajua kabisa kwamba gari hii imesajili ya zamani au ni mpya.

Napendekeza namba zinazofuata baada ya kuisha kwa namba ‘D’ ziwe katika mfumo wa ku-‘Randomize’ ambapo panakuwa hakuna mtitiririko maalum katika usajili wa namba za magari, hii itasaidia mtu kuuza gari lake kulingana na hali iliyonayo, na sio kuangalia namba, unakuta gari zuri lina hali nzuri ila linakosa soko kisa ni namba A.

=================================

Watu wengi hununua gari toka Japan ili tu aweze kupata usajili mpya kwenye gari lake, na hivyo tunatumia pesa nyingi mno za kigeni kuagiza magari kama taifa, wakati huo huo kuna gari nyingi nchini zina hali nzuri kuliko hata hizo za kutoka japan (imefungwa engine mpya, gearbox mpya, matairi mapya, body halina accident damage, low mileage); ila linakosa soko kisa ni namba C, au B au A, ila kuna watu wanaagiza mikangafu toka Japan kisa tu itapata usajili mpya.

Hii itatoa fursa ya kuanzishwa kwa ‘Car restoration facilities’ ambazo zinalorudisha gari katika hali ya upya kama ilivyokuwa kiwandani, hata hao Japan ndivyo wanavofanya kiasi wakituuzia mkangafu sisi tunaona kama jipya, hii itatengeneza ajira nyingi sana!!!!

Pia itaokoa fedha nyingi tunazotumia kuagiza magari toka Japan, maana mtu ataona anunue hapa hapa nchini restored car ambayo haitamwaibisha barabarani kwa kuwa na plate number ya zamani...


===========================
Update: 08/09/2022

Ajira nje nje



==========================
Update: 25/10/2022

===========================Update: 14/05/2023

 
wewe unaona kuuza gari lake tu ndicho kitu muhimu sana mpaka kuvuruga system nzima.

Mbona miaka yote toka tunapata uhuru namba zinaenda kwa mtiririko huo huo wa TZA ikiisha ndiyo inafata TZB, na bado watu waliuziana magari tu
 
wewe unaona kuuza gari lake tu ndicho kitu muhimu sana mpaka kuvuruga system
Thamani ya jumla ya magari nchini itapanda sana, pia itaondoa unyonge barabarani kwa wale wanaokuwa na namba za zamani, ila gari kafunga engine mpya, gearbox mpya, body halina accident kabisa, tairi mpya, ila mtu unashindwa kuuza kwa bei nzuri, kisa namba ‘C’
 
wewe unaona kuuza gari lake tu ndicho kitu muhimu sana mpaka kuvuruga system nzima.

Mbona miaka yote toka tunapata uhuru namba zinaenda kwa mtiririko huo huo wa TZA ikiisha ndiyo inafata TZB, na bado watu waliuziana magari tu
Kwani maendeleo maana yake nini? Tukisema tufanye vitu vile vile kama tulivyokuwa tunafanya miaka yote tutapiga hatua kusonga mbele kweli?
 
Mkuu wazo lako ni too personal...

Kama haliingizii kipato taifa basi kwao hali make sense.
 
Binafsi nadhani tungerudi kwenye utaratibu wa kusajili magari kutokana na mikoa yanapotoka na mwishoni herufi mbili zozote.Mfano wale wa Iringa,gari inaweza kuwa IR 2345 GN.Pia hata uhalifu wa kutumia magari ungepungua.
kwahiyo kila mkoa upewe mamlaka ya kufanya hivyo... tuunde vyombo kama mamlaka zamaji?
 
Binafsi napenda sana mfumo huu unaonesha gar n la lini.
Swala la kuuza mie naona hali ya gari ndio ifanya kiuzwe kwa bei gan na si namba japo namba nayo inamchango wake
 
Back
Top Bottom