Habarini!
Wenye ujuzi tupeane maarifa kidogo tafadhali.
Msingi wa swali langu unaegemea zaidi maisha ya wanyama hawa wala nyasi. Naona maisha yao yamejaa tabu na mateso na wasiwasi mtupu.
Wakikoswa kupigwa meno ya shingo na kunyonywa damu na simba au chui basi huishia kuliwa kwa kumegwa vipandevipande huku wakiwa hai na kujiona na mbwa mwitu, fisi n.k. Maumivu makali kiasi gani! Akili au uwezo wa maana wa kujitetea hata hawajapewa, unaona kabisa kuna sehemu kuna ambalo wangeweza kufanya kujiokoa na kukomesha uonevu lakini wapi. Mwenzao anachunwa ngozi hapa na fisi akiwa hai wao wapo pembeni wanaangalia tu. Angalau kidogo nyati wanajitahidi kupambana lakini bado sana, wazito na tegemeo lipo kwenye pembe tu ambazo simba na chui huwa wanazikwepa kiurahisi tu.
Unakuta mama twiga mtoto wake ameshambuliwa na chui au simba anajitahidi kumtetea lakini pekee anachoweza kufanya ni kumlambalamba tu huku akishindwa hata kumnyanyua (kutokana na kukosa maarifa) aondoke nae na kumshuhudia akifa kwa uchungu. Mateso ya kiasi gani ya kisaikolojia. Kuna wakati nashindwa kabisa kuangalia documentaries za wanyama.
Yapo mengi yanayowakuta, hapo sijazungumzia mateso kutoka kwa binadamu. Kule China samaki anakaangwa upande mmoja taratiibu bila kumuua na kuanza kumla upande huo huku akiwa hai, baadae (akiwa ameshateseka sana, bila shaka) ndo anakaangwa na upande mwingine na kufa kabisa. Jambo hili hufanyika kwa furaha kuu!
Hapa kwetu, kule umasaini kwa mfano, ng'ombe anaweza kuchomwa sijui kukatwa mshipa fulani na damu kutoka kwa wingi. Damu hiyo hukingwa na kunywewa. Maumivu anayapatayo ng'ombe huyu bila shaka unaweza kuyahisi. Sijazungumzia uchinjaji wa nguruwe ambapo anapigwa magongo ya kichwa kwanza na ule wa kisasa. Hatari tupu, wanyama wanaterezeshwa kwenye sakafu lainiii na kujichinja wenyewe katika kifaa kimoja kikali sana kilichowekwa hapo.
Ndege wanafungiwa kwenye matundu, hawana uhuru wa kujichanganya maisha yao yoote huku wengine wakifungiwa mazizini.
Swali langu, ni nini hekima ya Muumba iliyopo nyuma ya haya?
Swali la nyongeza; kuna hekima gani juu ya mfanano wa damu ya binadamu, wanyama na ndege? Mdada angalia anavyomkimbia mtu aliyejeruhiwa kidogo kwenye gari (hata kama ni kidole tu) kwa kuogopa damu, lakini ajabu mwangalie anavyokimbilia kumchaangachaanga ng'ombe au mbuzi mwenye damu yenye mfanano tu na ya binadamu.
Wenye ujuzi tupeane maarifa kidogo tafadhali.
Msingi wa swali langu unaegemea zaidi maisha ya wanyama hawa wala nyasi. Naona maisha yao yamejaa tabu na mateso na wasiwasi mtupu.
Wakikoswa kupigwa meno ya shingo na kunyonywa damu na simba au chui basi huishia kuliwa kwa kumegwa vipandevipande huku wakiwa hai na kujiona na mbwa mwitu, fisi n.k. Maumivu makali kiasi gani! Akili au uwezo wa maana wa kujitetea hata hawajapewa, unaona kabisa kuna sehemu kuna ambalo wangeweza kufanya kujiokoa na kukomesha uonevu lakini wapi. Mwenzao anachunwa ngozi hapa na fisi akiwa hai wao wapo pembeni wanaangalia tu. Angalau kidogo nyati wanajitahidi kupambana lakini bado sana, wazito na tegemeo lipo kwenye pembe tu ambazo simba na chui huwa wanazikwepa kiurahisi tu.
Unakuta mama twiga mtoto wake ameshambuliwa na chui au simba anajitahidi kumtetea lakini pekee anachoweza kufanya ni kumlambalamba tu huku akishindwa hata kumnyanyua (kutokana na kukosa maarifa) aondoke nae na kumshuhudia akifa kwa uchungu. Mateso ya kiasi gani ya kisaikolojia. Kuna wakati nashindwa kabisa kuangalia documentaries za wanyama.
Yapo mengi yanayowakuta, hapo sijazungumzia mateso kutoka kwa binadamu. Kule China samaki anakaangwa upande mmoja taratiibu bila kumuua na kuanza kumla upande huo huku akiwa hai, baadae (akiwa ameshateseka sana, bila shaka) ndo anakaangwa na upande mwingine na kufa kabisa. Jambo hili hufanyika kwa furaha kuu!
Hapa kwetu, kule umasaini kwa mfano, ng'ombe anaweza kuchomwa sijui kukatwa mshipa fulani na damu kutoka kwa wingi. Damu hiyo hukingwa na kunywewa. Maumivu anayapatayo ng'ombe huyu bila shaka unaweza kuyahisi. Sijazungumzia uchinjaji wa nguruwe ambapo anapigwa magongo ya kichwa kwanza na ule wa kisasa. Hatari tupu, wanyama wanaterezeshwa kwenye sakafu lainiii na kujichinja wenyewe katika kifaa kimoja kikali sana kilichowekwa hapo.
Ndege wanafungiwa kwenye matundu, hawana uhuru wa kujichanganya maisha yao yoote huku wengine wakifungiwa mazizini.
Swali langu, ni nini hekima ya Muumba iliyopo nyuma ya haya?
Swali la nyongeza; kuna hekima gani juu ya mfanano wa damu ya binadamu, wanyama na ndege? Mdada angalia anavyomkimbia mtu aliyejeruhiwa kidogo kwenye gari (hata kama ni kidole tu) kwa kuogopa damu, lakini ajabu mwangalie anavyokimbilia kumchaangachaanga ng'ombe au mbuzi mwenye damu yenye mfanano tu na ya binadamu.