![]()
Ngoma ikilia sana ujue inakaribia kupasuka na lisemwalo lipo kama halipo, basi li njiani laja! Hatimaye Wema Isaac Sepetu na Naseeb Abdul Jumaa ‘Diamond', wamemwagana rasmi
Ilikuwa ni Jumanne, saa mbili usiku, Diamond ‘Platinum' aliita vyombo vya habari katika Hoteli ya Lion Sinza jijini Dar es Salaam na kufunguka:
"Washikaji, nimewaita hapa nifunguke mbele yenu kuwa nimemmwaga rasmi yule demu (Wema) kwa sababu hapatani na mama yangu (Sandra Sammy).
"Kwanza Wema amekuwa akinilazimisha nitengane na mama yangu, yaani nimrudishe kule Tandale tulipokuwa tukiishi mwanzo , halafu mimi na yeye tuishi Sinza (Madukani), jambo ambalo sipo tayari kulifanya.
TUKIO ZIMA LA KUPIGANA CHINI LIPO HAPA << WEMA NA DIAMONDI WAACHANA>>
Unajua utoto ni shida sana, alipomtongoza hakuita waandishi wa habari na kudeclare sasa anaingia vitani kumtongoza Wema lakini kuachana anaita waandishi wa habari ili iwaje? Halafu mapenzi yana kurudiana baada ya kuyaweka mambo sawa sasa sijui kama ataita tena waandishi wa habari kuwajuza jamani nimerudiana na Wema! Halafu Wema amshukuru Mungu yule dogo si saizi yake musiki wa kibongo ni kama uganga, mganga fulani anavuma halafu ghafla anapotea hivyo hivyo wanamuziki, yuko wapi Mr Nice, Babu aka Insp Haroon n.kwalitongozana kimyakimya, walioana kimyakimya basi waachane kimyakimya. hayo ni matumizi mabaya ya media. lakini kwa kuwa ni udaku, ndo kazi yao