We mwanamke inakuwaje unatandikiwa kitanda?

We mwanamke inakuwaje unatandikiwa kitanda?

[QU
OTE=Dark City;5450256]Kwa nini hupendi Nyamayao??

Poti wangu Mwita Maranya yeye kasema kuwa bed room kwake kuna siri zao (may be na ule uganga wa kule Poti umefichwa huko..lol:smiling::smiling::whistle🙂 na pia ni defence mechanism dhidi ya house girl asije kupindua gari....I hope I ma right kamanda???

Wewe kwani nini hutaki kusaidiwa na house girl??

Babu DC!![/QUOTE]

sio kwamba sitaki/sipendi, ni wajibu wangu huo, chochote cha chumbani kwangu ni wajibu wangu kukitekeleza kama sipo ninajua nina wa kunisidia, msukuma!
 
kazi kwel kwel! hebu nikae kando kwanza, nione mtanange unaendeleaje??
 
Kiukwel, utaratibu wa chumbani kwangu na wife, japo haujaandikwa ni kwamba wa mwisho kuamka kati yetu ndiye anayetandika kitanda.
Alafu tuna utani kuwa kila anayetandika, mwenzake akija anajitahidi kumkosoa kuwa hakutandika vizuri, anajifanya kutoa kasoro (jokes)
I just enjoy that?
 
Siku zote mke ni mlinzi wa mume wake na mume ni mlinzi wa mke wake. Hapa simaanishi kwamba umlinde kwa maana ya kumfuatilia kila anachokifanya isipokuwa unatakiwa kutambua mazingira hatarishi kwa mkeo/mumeo na kujaribu kumuepusha nayo. Wapo wanaume wachache wanaotoka na mabeki tatu hata kama hawaingii vyumbani mwao lakini believe me wengi wao unakuta kuna mazoea yasiyo ya kawaida baina ya mume na beki tatu ambayo yamesababishwa na mwanamke kutafuta usawa kiasi kwamba kazi zote anamuachia beki tatu.

Kwa kawaida binadamu kadri unavyomtendea wema hata kama ni wajibu wako ndipo anapoanza kukuzingatia na baade kujenga matamanio. Wanaume wengi ni dhaifu kwa wanawake jamani hili kama hamtaki kulikubali siwalazimishi. Beki tatu anakula vizuri anavaa vizuri anajua kupiga vitopu na kubinua chuchu halafu mzee anarudi usiku anafunguliwa nabeki tatu anatengewa chakula na beki tatu, ananawishwa na beki tatu hata kitanda anatandikiwa na eki tatu? mtaishia kulia na kusaga meno sana.

kuna wengine sie waume hawataki kusikia chakula cha kupikiwa na dada, so ni wajibu wangu kama sipo atakula anapopajua ama atapika mwenyewe, kuhusu kitanda ndio kitu ambacho nakipinga milele coz naona ntakuwa sijamtendea dada haki hata kidogo, aisee ni jukumu langu kuanzia mashuka hadi mataulo ya room kwangu,room yangu inafungwa na funguo anazo baba/mama, DC hatufichi hirizi humu ndani but dada anaingia kufanyaje haswa kama mie nafanya wajibu wangu? kwangu mie naona sio haki kabisa kwa dada kufanya usafi room kwa wanandoa,hiyo ni kwa nyamayao.
 
Ahsante sana kaka Mwita Maranya,

Naona Poti mjadala unaanza kunoga kwani hata wakongwe akina Nyamayao wako ndani ya nyumba..

Sababu zako mkee nazielewa... ila kuna nyingine bado zinanipa kigugumizi kidogo....

Una maana kwamba house girls ni hata kiasi hicho kwa ndoa??

Kwa upande wangu mie huwaona kama wanangu basi....

Na kwa vile wanangu wanaingia chumbani kwangu (kama mimi na bibi hatupo), basi hata wasaidizi hao wanaigia tu...

Ni hayo kaka,

Babu DC!!

Mzee mzima sitarajii kama ipo siku unaweza kumtamani mwanao, hata kama mama nanihino amekwenda ulaya for five years.
Lakini ukiwa mkweli utakubali kwamba mara kadhaa unakutana na wanawake wa umri sawa na binti yako na unajikuta umewatamani. Kwahiyo unaweza kuiona hiyo tofauti.
 
WIFE
Washing
Ironing
Food
Etcetera

(Kama ninakumbuka vizuri)

Pole zenu wenye waume wanaotumia hii definition!
 
msichana atafua tena baadhi ya nguo zetu na kazi nyingine lakinj chumba changu haikubaliki kuanzia usafi hadi kutandika

Eti mzee mwenzangu Blaki Womani, bed room kwako umefichamo nini hadi hutaki mtu aingie??

Kwani akikutandikia unakuwaje??

Mjenda Chilo
Ugomvi mwingine ni _______________ mtupu! I'd have sympathazied kama issue ya jamaa ingekuwa kitanda chao hakitandikwi,but not who is making the bed? Duh, kwa kweli siielewi hiyo shame unayoongelea ,kwani kazi ya mke kwenye ndoa ni kutandika kitanda:shut-mouth:!!!!???

Na kama ni hivyo, basi akishindwa kutandika kinachofuata ni talaka...right??

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Mzee mzima sitarajii kama ipo siku unaweza kumtamani mwanao, hata kama mama nanihino amekwenda ulaya for five years.
Lakini ukiwa mkweli utakubali kwamba mara kadhaa unakutana na wanawake wa umri sawa na binti yako na unajikuta umewatamani. Kwahiyo unaweza kuiona hiyo tofauti.

Exactly kaka Mwita Maranya,

Na binti akishaishi chini ya paa langu tayari anakuwa kama mwanangu...that's why siwezi kumtamani...

Sasa inakuwaje house girl aonekane tishio kiasi hicho???

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
WIFE
Washing
Ironing
Food
Etcetera

(Kama ninakumbuka vizuri)

Pole zenu wenye waume wanaotumia hii definition!

Sema neno basi na wewe nyumba kubwa.....

Hapa naona ngoma inogile......

House girl akifanya usafi wa bed room na kutandika kitanda mbingu inapasuka vipande??

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
WIFE
Washing
Ironing
Food
Etcetera

(Kama ninakumbuka vizuri)

Pole zenu wenye waume wanaotumia hii definition!

Washing- beki tatu (isipokuwa vyupi tu)
Ironing-beki tatu
Food-beki tatu
Etcetera-ufafanuzi tafadhali(kuna vitu gani humu kwenye hiki kipengele?)
 
Kumbe kitchen party haina mafunzo yoyote[ni sherehe ya kula mpunga na kutoa zawadi].!!!
 
Umeona eeh hakuna kitu ambacho sijuhi kama ningeweza vumilia kama mwanaume bossy....masheria lukuki...oh siri alichopika hg....ooh nguo zangu lazima ufue; ndio maana japo hg hatandiki chumba changu siwezi shangaa hao wanaotandikiwa na hg kwani ni utaratibu tu kwani kutandika ni kazi ngumu kama kubeba zege mpaka mtu aone ameonewa?

Mi nawajua washkaji zangu fulani (yes si wa tanzania)wanafuliwa hadi kofuli na hg...na wala ha complain kwani anapata mshiko wa nguvu...mbona manesi wanashika vidonda sembuse shuka tuuuu.

Sipendi kweli hizi 'Donts'....sijuhi mke wa fulani this mke wa fulani that...



Kiukwel, utaratibu wa chumbani kwangu na wife, japo haujaandikwa ni kwamba wa mwisho kuamka kati yetu ndiye anayetandika kitanda.
Alafu tuna utani kuwa kila anayetandika, mwenzake akija anajitahidi kumkosoa kuwa hakutandika vizuri, anajifanya kutoa kasoro (jokes)
I just enjoy that?
 
kazi kwel kwel! hebu nikae kando kwanza, nione mtanange unaendeleaje??


Utakuwa hutendi haki kabisa cacico,

Ni sawa na kwenda hotelini ukala halafu usilipe bill....

Hebu changiapo kidogo basi na wewe.....

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Mwita sina maelezo zaidi kwani nime copy toka movie fulani ya vijana marafiki waliooa kipindi kimoja wakawa wanadanganyana....mi mke wangu lazima apike....mi mke wangu lazima afue na kunyoosha nguo....etc....kumbe waongo wakirudi home wanapigishwa deki.


Washing- beki tatu (isipokuwa vyupi tu)
Ironing-beki tatu
Food-beki tatu
Etcetera-ufafanuzi tafadhali(kuna vitu gani humu kwenye hiki kipengele?)
 
Kwani mkiwa hotelini hizo taulo zenu huwa mnaziweka wapi??

Na huko hotelini huwa hampishi watu wakafanya usafi??

Naomba elimu yako Nyamayao..., hata ukitaka nilipe bill nitalipa!!

Babu DC!!

ushasema hotelini, kuna tofautiana sana na kwangu, wale wameajiriwa na moja ya jukumu lao ni hilo, mie nimeajiri na hilo jukumu halimuhusu.
 
Yani nyinyi wake zetu mnatia aibu sana, nimetoka kusuluhisha ugomvi kwa jamaa yangu, ugomvi ulikuwa mkubwa sana ila source mshkaji kachoka kutandikiwa kitanda na beki tatu so akamuuliza mkewe kama huyu dada anafua, ananipikia na bado ananitandikia kitanda hv nikwanini namnyima haki yake ya unyumba? mwanamke almanusura apasuke, ugomvi umesuluhishwa ila vipande nimempa, shame on u na wewe kama ni mmoja wao.

Binafsi sijawahi "kutandika" kitanda tangu nilipofunga pingu za maisha...!

Mke wangu akisafiri huwa anakuta mashuka yale yale aliyoyaacha yakiwa bado yapo kitandani, hata na "net" pia iko vile vile...!

Ni Fedheha na AIBU kubwa kwa mwanaume "anayelala kitanda" kimoja na mwanamke, "kumtandikia" kitanda huyo mwanamke...! Mwanamke akikufikisha hatua hiyo, kwa kisingizio cha "kusaidiana" fahamu fika kuwa kuna siku atakuachia "nguo za ndani" ufue na kukupangia zamu za kupika - SHAME...!
 
Back
Top Bottom