We mwanamke inakuwaje unatandikiwa kitanda?

We mwanamke inakuwaje unatandikiwa kitanda?

Hapa sasa ndipo ninaposhindwa kuwaelewa wadogo zangu...

Mnalilia kusaidiwa kazi, na wakati huo mnaweza mipaka......

Kama kweli mnataka msaada, inakuwaje msaada wa house girl hamuutaki?

Babu DC!!

Si kila kazi inahitaji usaidizi, nyengine unafanya mwenyewe, na hapo ndipo mpaka wa beki tatu unapoanzia na kukomea.
 
Mzee mzima kweli leo kazi ipo kama na wewe umegeuka kuwa denti.
Chumbani kwangu na mke wangu ni mahali petu pa binafsi/maalum (private) kufanyia mambo yetu, huko tunajiachia. Chochote kinachofanyika huko ni chetu wawili mimi na mama rhobi tu ndo tunajua na tunaopaswa kujua. Mzee mzima chumbani kwako ndio mahali pa kujifunga khanga. Tatizo ninyi waswahili wenzangu mnafunga khanga mnatoka nazo kwenda sokoni hapa mtanishangaa.

Si kila unachokifanya kinakuwa ni kwa ajili ya "public consumption" hapa nakusudia public ya familia yako, lile mnalodhani kwamba linaweza kufikishwa kwa wengine ndo mnalitoa. Kama mna jambo lenu huko ndo mnaweka cabinet na kulidadavua, huko ndiko mnakaliana bila wasiwasi wowote manake mko wenyewe (hapa najua wengine wanajifanya wameendelea wanadandiana hata sebuleni mbele ya ndugu jamaa na marafiki)

Na la mwisho, siri yenu wewe na mkeo inakuwa siri ikiwa ni yenu wawili tu lakini mkishamruhusu mtu mwingine kuingia chumba chenu cha siri basi hakuna tena usalama hapo. Tena hawa mabeki tatu tunaowaokota tu mitaani wameshaleta mabalaa kwenye ndoa/familia za watu. Hapa kuna mambo mchanganyiko kama vile mabeki tatu kuwatia kwenye kumi na nane zao wanaume, kuibiwa, kuvujisha siri za familia na mambo mengine kama hayo. Sasa kwa kulitambua hilo ndipo wahenga wetu wakatufundisha kutoruhusu watu wengine kukizoea chumba changu na mke wangu.

Bado bado baba Rhobi,

Hivi huko chumbani kuna siri gani ambazo mnazificha kiasi kwamba kuwe kama jehanamu kwa watu wengine??

Halafu, hata wewe unaogopa kuibiwa na house girl kamanda wangu?

Ila pia sijaelewa kitu hapa, kwani watu wanaongelea watoto au wasaidizi wa kazi kuingia chumbani wakati nyie mpo huko? Na kama hampo, kwa nini wasiingie kwa shughuli maalumu ikiwemo usafi?

Na hujawahi kupata wageni wakaingia hadi chumbani kwako katika yale mambo ya kutegembezana kwenye makazi yetu??

Naomba usichoke mzee mwenzangu Mwita Maranya...!!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Si kila kazi inahitaji usaidizi, nyengine unafanya mwenyewe, na hapo ndipo mpaka wa beki tatu unapoanzia na kukomea.


Bado sijapata msaada kamanda,

Kwanini tunaweka mpaka Poti, wakati wanatupikia chakula tunakula na kutulelea watoto wetu??

Naomba sababu za msingi hasa ili na mimi nikajaribu...ila nadhani nimeshachelewa!!

Babu DC!!
 
Bado sijapata msaada kamanda,

Kwanini tunaweka mpaka Poti, wakati wanatupikia chakula tunakula na kutulelea watoto wetu??

Naomba sababu za msingi hasa ili na mimi nikajaribu...ila nadhani nimeshachelewa!!

Babu DC!!

Sasa mzee mzima suala la kukubaliana na mimi ni gumu sana kama kila sababu unayoambiwa unaiona ndogo. Kila siku hapa JF watu wanalalamika (hasa wanawake) kwamba wameporwa waume na mabeki tatu, ama wamewafumania waume zao na mabeki tatu, ama wanaume wanalalamika kwamba wamenaswa na mapenzi ya mabeki tatu.

Sisi ni binadamu mkuu usisahau hilo kwahiyo ni muhimu sana kuwekeana mipaka ili kupunguza hizo risk badala ya kujiachia mwisho wa siku ni vilio katika ndoa za watu.

Mimi binafsi na mke wangu beki tatu hakanyagi chumbani kwetu kwa kipindi chote cha maisha yetu ya ndoa na hatutegemei kumruhusu aingie chumbani kwetu, eti atusaidie kufanya usafi? no bro., chumba chetu tunakifanyia usafi sisi wenyewe.
 
Hujanisoma vizuri mkuu Stamina, nami pia sitaki kabisa hg aingie chumbani so kwa vyovyote hawezi kunitandikia kitanda. Binafsi sipendi hata kufuliwa nguo zangu na mtu yeyote, ndio iwe za mume wangu! Pia kupika ni hobby yangu. Nimechangia kwa kuzingatia mazingira na hali ya uchumi tu.

kutandikiwa n aibu
 
Last edited by a moderator:
Bado bado baba Rhobi,

Hivi huko chumbani kuna siri gani ambazo mnazificha kiasi kwamba kuwe kama jehanamu kwa watu wengine??

Halafu, hata wewe unaogopa kuibiwa na house girl kamanda wangu?

Ila pia sijaelewa kitu hapa, kwani watu wanaongelea watoto au wasaidizi wa kazi kuingia chumbani wakati nyie mpo huko? Na kama hampo, kwa nini wasiingie kwa shughuli maalumu ikiwemo usafi?

Na hujawahi kupata wageni wakaingia hadi chumbani kwako katika yale mambo ya kutegembezana kwenye makazi yetu??

Naomba usichoke mzee mwenzangu Mwita Maranya...!!

Babu DC!!


Ninachoamini ni kwamba kila familia ina siri zake, na mimi nina siri zangu binafsi za familia yangu, sasa mzee mzima kama wewe hauna siri za familia yako nitashindwa kukuelewa na kukubalia.

La kuibiwa na beki tatu mkuu wala usinishangae mimi ni binadamu tu kama wengine, kwahiyo nina madhaifu yangu. Na ndio maana tumekubaliana na mama rhobi si kila kazi za ndani anafanya beki tatu, kuna kazi nyengine tunafanya sisi wenyewe.

Kinga ni bora kuliko tiba mkuu. Usisahau kwamba wanaume hodari huanguka kirahisi sana kwenye mikono ya wanawake!!
 
nyie ni wanawake mnaojitambua ,nawaombeeni waume zenu wawe ni watu wanaothamini huo uelewa wenu na kudumisha upendo kwenye hizo ndoa zenu.
be blessed all.
asakuta same... kuna baadhi ya watu wanajadili ili kuchangamsha genge tufurahi sie (kwamba wanayoyasema hayapo wala hayawezekani).

pia nachoamini ni kuwa kama mume na mke wanapendana na kila mtu anatimiza wajibu wake kwa kadri ya uwezo wake ..hayo MALUMBANO ya kusaidiana sijui fedha (mke kusaidia mahitaji mbalimbali ya familia) au sijui kazi za ndani (baba kusaidia some stuffs za pale home) hayapo lol.

Msaada unakuja automatically, na usipokuja una uomba akikataa basiiii.. Fanya kwa kadri ya nafasi na afya yako ikishindikana fanya siku inayofuata.

tena now days na hizi digitali zinatusaidia sana (apply na hizi pia) kurahisisha mambo... si mnafanya kazi bana kwa hiyo hamna nafasi ya shughuli za nyumbani .. nunua mashine ya kufua, vimashine vingine vya kurahisisha kazi za nyumbani, weka na beki 3... Alafu nyie mnabaki na yale mambo yenu binafsi ambayo hamtaki kuyaanika hadharani. JUST SIMPLE
 
Last edited by a moderator:
Bado sijapata msaada kamanda,

Kwanini tunaweka mpaka Poti, wakati wanatupikia chakula tunakula na kutulelea watoto wetu??

Naomba sababu za msingi hasa ili na mimi nikajaribu...ila nadhani nimeshachelewa!!

Babu DC!!


tena sana, ulitembea kabla ya kutambaa, mie ni mmojawapo, dada hajui room kwangu kunafananaje, na sio kwamba nahofu atanikwapulia sijui nini na nini but huwa sipendi, kule ni pangu na mume wangu basi,mengine afanye but kama mama nimeamua kwamba hilo aliache kama lilivyo.
 
Sasa hapo mbona hakuna hata moja iliyo men specific? Zote zafanywa na modern women ....afu kupenda, kuheshimu nazo ni kazi lol! Men put uncooked food on the table lol!

What if a man can't provide for the family needs?!

hizi ni part ya kazi zake bwana wewe....kugegedwa pia kazi ati lol.
mwanaume kazi zake ni; kugegeda, kuput food on the table, provide the wife's wants and needs, kumpenda mke unconditionaly na kumuheshimu
 
Nadahani ifike mahali wanawake mjitambue,swala la kulalama mara oooh wanatufanya maroboti,mara ooh kwanini nao wasifanye.........kuwa mjanja,hapa kuna wanawake wanatoa comments za kipuuzi kabisa,kisa kutaka usawa.Kusaidiana kupo ila isiwe ndio mazoea.
 
Vitu vidogo kama hivyo ni chachu kubwa ya ndoa.Haya makelele ya haki na usawa unawatia ujeuri hata kwenye mambo ya kijamii-mambo ya chumbani.Halafu baadae unalalamika housegirl akikusaidia unyumba-halafu unakuta anautoa unyumba bil kinyongo zaidi yako mke unayejifanya uko busy.Badilikeni,tendo moja linabadilisha ladha yote uliyoijenga kwa miaka mingi.Wanaume hatupendi kufanya lakini mnatutengenezea mazingira wenyewe.
 
Si kila kazi inahitaji usaidizi, nyengine unafanya mwenyewe, na hapo ndipo mpaka wa beki tatu unapoanzia na kukomea.

hivi kiukweli huyo dada anaingia chumbani kufanya nini, usafi ama?yaani anahusikaje na chumbani kwangu,hizo habari za kupika sijui nini ndio wajibu wake, za room kwangu ni wajibu wangu.
 
Sasa mzee mzima suala la kukubaliana na mimi ni gumu sana kama kila sababu unayoambiwa unaiona ndogo. Kila siku hapa JF watu wanalalamika (hasa wanawake) kwamba wameporwa waume na mabeki tatu, ama wamewafumania waume zao na mabeki tatu, ama wanaume wanalalamika kwamba wamenaswa na mapenzi ya mabeki tatu.

Sisi ni binadamu mkuu usisahau hilo kwahiyo ni muhimu sana kuwekeana mipaka ili kupunguza hizo risk badala ya kujiachia mwisho wa siku ni vilio katika ndoa za watu.

Mimi binafsi na mke wangu beki tatu hakanyagi chumbani kwetu kwa kipindi chote cha maisha yetu ya ndoa na hatutegemei kumruhusu aingie chumbani kwetu, eti atusaidie kufanya usafi? no bro., chumba chetu tunakifanyia usafi sisi wenyewe.

kama kuporana wataporana hata jikoni, ishu ni kwamba chumbani kwa baba/mama ni pa wahusika hao wawili tu, chochote cha humo ndani wafanye hao wawili tu, mie nimpe dada mataulo/shuka za room kwangu afue, adeki? hapana aisee, naona kama hazimstahili, ni wajibu wangu huo, kama siwezi kumpa hizo kazi na room kwangu hana umuhimu kwa kupajua/kuingia.
 
kama kuporana wataporana hata jikoni, ishu ni kwamba chumbani kwa baba/mama ni pa wahusika hao wawili tu, chochote cha humo ndani wafanye hao wawili tu, mie nimpe dada mataulo/shuka za room kwangu afue, adeki? hapana aisee, naona kama hazimstahili, ni wajibu wangu huo, kama siwezi kumpa hizo kazi na room kwangu hana umuhimu kwa kupajua/kuingia.

Siku zote mke ni mlinzi wa mume wake na mume ni mlinzi wa mke wake. Hapa simaanishi kwamba umlinde kwa maana ya kumfuatilia kila anachokifanya isipokuwa unatakiwa kutambua mazingira hatarishi kwa mkeo/mumeo na kujaribu kumuepusha nayo. Wapo wanaume wachache wanaotoka na mabeki tatu hata kama hawaingii vyumbani mwao lakini believe me wengi wao unakuta kuna mazoea yasiyo ya kawaida baina ya mume na beki tatu ambayo yamesababishwa na mwanamke kutafuta usawa kiasi kwamba kazi zote anamuachia beki tatu.

Kwa kawaida binadamu kadri unavyomtendea wema hata kama ni wajibu wako ndipo anapoanza kukuzingatia na baade kujenga matamanio. Wanaume wengi ni dhaifu kwa wanawake jamani hili kama hamtaki kulikubali siwalazimishi. Beki tatu anakula vizuri anavaa vizuri anajua kupiga vitopu na kubinua chuchu halafu mzee anarudi usiku anafunguliwa nabeki tatu anatengewa chakula na beki tatu, ananawishwa na beki tatu hata kitanda anatandikiwa na eki tatu? mtaishia kulia na kusaga meno sana.
 
Ninachoamini ni kwamba kila familia ina siri zake, na mimi nina siri zangu binafsi za familia yangu, sasa mzee mzima kama wewe hauna siri za familia yako nitashindwa kukuelewa na kukubalia.

La kuibiwa na beki tatu mkuu wala usinishangae mimi ni binadamu tu kama wengine, kwahiyo nina madhaifu yangu. Na ndio maana tumekubaliana na mama rhobi si kila kazi za ndani anafanya beki tatu, kuna kazi nyengine tunafanya sisi wenyewe.

Kinga ni bora kuliko tiba mkuu. Usisahau kwamba wanaume hodari huanguka kirahisi sana kwenye mikono ya wanawake!!

Ahsante sana kaka Mwita Maranya,

Naona Poti mjadala unaanza kunoga kwani hata wakongwe akina Nyamayao wako ndani ya nyumba..

Sababu zako mkee nazielewa... ila kuna nyingine bado zinanipa kigugumizi kidogo....

Una maana kwamba house girls ni hata kiasi hicho kwa ndoa??

Kwa upande wangu mie huwaona kama wanangu basi....

Na kwa vile wanangu wanaingia chumbani kwangu (kama mimi na bibi hatupo), basi hata wasaidizi hao wanaigia tu...

Ni hayo kaka,

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
tena sana, ulitembea kabla ya kutambaa, mie ni mmojawapo, dada hajui room kwangu kunafananaje, na sio kwamba nahofu atanikwapulia sijui nini na nini but huwa sipendi, kule ni pangu na mume wangu basi,mengine afanye but kama mama nimeamua kwamba hilo aliache kama lilivyo.

Kwa nini hupendi Nyamayao??

Poti wangu Mwita Maranya yeye kasema kuwa bed room kwake kuna siri zao (may be na ule uganga wa kule Poti umefichwa huko..lol:smiling::smiling::whistle🙂 na pia ni defence mechanism dhidi ya house girl asije kupindua gari....I hope I ma right kamanda???

Wewe kwani nini hutaki kusaidiwa na house girl??

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
kama kuporana wataporana hata jikoni, ishu ni kwamba chumbani kwa baba/mama ni pa wahusika hao wawili tu, chochote cha humo ndani wafanye hao wawili tu, mie nimpe dada mataulo/shuka za room kwangu afue, adeki? hapana aisee, naona kama hazimstahili, ni wajibu wangu huo, kama siwezi kumpa hizo kazi na room kwangu hana umuhimu kwa kupajua/kuingia.


Kwani mkiwa hotelini hizo taulo zenu huwa mnaziweka wapi??

Na huko hotelini huwa hampishi watu wakafanya usafi??

Naomba elimu yako Nyamayao..., hata ukitaka nilipe bill nitalipa!!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
kutandikiwa kitanda n matusi kwan inaonyesha wazazi wako hawajakufunda


Kwani ni mambo mangapi wazazi wametufunda ila tunayafanya knowingly or not??

What's so special na kutandika kitanda au kufanya usafi wa chumba??

Babu DC!!
 
Back
Top Bottom