Wazo la kuanzisha Ben Saanane Trust Fund (BSTF)

Wazo la kuanzisha Ben Saanane Trust Fund (BSTF)

Ndio walewaleeee!! WAPIGA DILI, duuuh Mara tuuuu! MNATISHA, SUBIRINI KIDOGO VYOMBO HUSIKA VINAFANYA KAZI, NI LAZIMA UKWELI UTAPATIKANA TU
maono yangu yananiambia,kuhusu sakata la kutoweka/kupotea/kupotezwa kwa ben saanane,sahau kupata msaada wa aina yoyote toka kwa hicho ulicho kiita "vyombo husika".

hayo ni maono yangu niliyo oteshwa ndotoni usiku wa kuamkia juzi.naomba niishe hapo.
 
Nauliza hivi, ile Alphonce Mawazo Trust Fund iliishiaga wapi?
 
-Tusubiri TCRA watoe Records za Simu zake aliyewasiliana naye mara ya mwisho na kujua simu ilizimwa eneo gani,naomba Chadema wafatilie kwa makini hizo records ndio zitatoa jibu,pili chukueni IMEI ya simu yake iangalieni inatumika au ilitumika kuwekwa namab gani.

-Chadema Makao Makuu,Makene,Mbowe au Mashindi watoe taarifa rasmi kuhusu kupotea kwa BEN.
 
Mchangamkie fursa ki halali. Si kila kitu dili.
Kama kuosha maiti kumegeuzwa dili itakuwa kuanzisha mfuko wa kuchangia hela za kumtafuta mtu ambaye bado haijathibitishwa kwamba amekufa?

Kuna watu wanaishi hapa mijini kwa kuuza sanda na siku ikitokea ajali na watu wengi wakafa wao husema leo biashara imechanganya. Hiyo tabia ya kujifanya watakatifu ndiyo inawafanya wahindi na waarabu wawe matajiri sisi tunaishia kuwa vibarua wao!!
 
UWIZI WA JUA KALI HUU
Umeibiwa nini? Haya ndiyo yale ya ile akaunti iliyofunguliwa Kagera. Hata hela haijaingia watu wakaanza kuweweseka kwamba hawa wataiba! Sasa wewe hapa umeibiwa nini?
 
Sifa moja ya wapiga dili, hawana aibu.

Mtu mzima kama Ben Saanane anapoteaje? amekuwa kalamu? Na kwanini mnahangaika sana wakati Boss wake anaendelea kujipiga selfie huko Ulaya?
Hili ni jambo zito na si la kutafutia sifa wala like unazopewa, utayaona tu muda si mrefu kwa maana hakuna ajuaye ya mbele
 
Umeibiwa nini? Haya ndiyo yale ya ile akaunti iliyofunguliwa Kagera. Hata hela haijaingia watu wakaanza kuweweseka kwamba hawa wataiba! Sasa wewe hapa umeibiwa nini?
Tumewashtukia mchana kweupe . ..achana nayo . .
 
Back
Top Bottom