TANZIA Waziri William Lukuvi (na Mbunge wa Isimani) afariki Dunia

TANZIA Waziri William Lukuvi (na Mbunge wa Isimani) afariki Dunia



Rais Samia, amesikitika kutangaza kifo cha William Vangimembe Lukuvi (Mb.), aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) pamoja na Mbunge wa Jimbo la Isimani.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi, Lukuvi amefariki dunia leo tarehe 25 Machi, 2026, majira ya saa moja asubuhi katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, alipokuwa akipatiwa matibabu kufuatia ugonjwa wa mshtuko wa moyo.

Rais Samia ametoa salamu za pole kwa Spika wa Bunge, familia ya marehemu, wananchi wa Jimbo la Isimani, ndugu, jamaa na marafiki, pamoja na Watanzania wote kwa ujumla kufuatia msiba huo.
View attachment 3562430


Historia ya William Lukuvi

William Vangimembe Lukuvi ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri wa Tanzania ambaye amekuwa na mchango mkubwa katika masuala ya ardhi, maendeleo ya makazi, na siasa za kitaifa. Akiwa Mbunge wa Jimbo la Ismani kwa zaidi ya miaka 30 tangu mwaka 1995 mpaka kufariki mwaka 2026, Lukuvi ameshikilia nyadhifa mbalimbali za uwaziri.

Maisha ya Awali na Elimu
William Lukuvi alizaliwa tarehe 15 Agosti 1955 katika kijiji cha Mapogoro, Wilaya ya Iringa Vijijini, Tanganyika. Alipata mafunzo yake ya awali katika Tabora Teachers College (TTC) na baadaye kuhitimu Shahada ya Uzamili katika Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Huria cha Tanzania.

Safari ya Kisiasa
Lukuvi alianza safari yake ya kisiasa kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Ismani mnamo mwaka 1995 kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo ameendelea kushikilia hadi amefariki Dunia March 25, 2026.

Aidha, amehudumu kama Waziri katika nyadhifa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Bunge.

Mnamo Juni 2023, Rais Samia Suluhu Hassan alimteua kuwa Mshauri wa Rais kuhusu Mahusiano ya Kisiasa na Kijamii na baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 Rais Samia alimteua William Lukuvi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) nafasi ambayo ameishikilia mpaka kufariki kwakwe.

Zaidi, Soma=> CV ya William Lukuvi
Huyu mzee amekula bata za nchi hii kwa muda mrefu sana. Mungu ailaze mahali pema peponi roho yake.
 
MMMMMMH HAYA MANABII UCHWARA MBONA YAANZA KUNITISHA, LILE NABII TAPELI JUZI HAPA LILISEMA MWAKA HUU WATADONDOKA VIONGOZI WA JUU SIIJUI WA NINI, NIMESAHAU, ANYWAY TUPENDANE NDUGU ZANGU DUNIA TUNAYO IPIGANIA KWA NGUVU SI KITU,WALE TUNAO ONA HAWASTAILI KUISHI NA SISI PIA TUSIJISAHAU, UKIPIGA MTU MNAKUWA WENGI ILA SIKI YAKO IKIFIKA UTAKUWA MWENYEWE KABULINI NDUGU ZANGU TUKUMBUKE HILO TUNAPO UMIZA WENZETU, KWETU KABULINI HUKO TUTAKAA SANA INSHAALLAH MWENYEZI MUNGU ATU SAMEHE MAKOSA YETU, AMIN🙏🙏🙏
 
Sikuwahi kuona thamani ya Lukuvi katika siasa na maendeleo ya Tanzania

Kwa uzoefu wake Bungeni na Serikalini amekufa akiwa CHAWA na siyo STATESMAN
 
Una akili sana wewe, umeconnect dots vizuri, nawaona wale wote waliokua na mawasiliano na HP wanapata kitu na box. Na huko HP alikofichwa anawataja wote. rip
Unajua ukijiuliza hata uadui wa Nchimbi na mazeri hupati sababu ila ukiconnect dots unagundua kuwa huenda Nchimbi wakati akiwa balozi automatically walikuwa na mawasaliano na mabolozi wenzake akiwemo HP sasa naamini kulikuwa na mambo mazito wanayapanga kwa pamoja so baada ya kukamatwa HP huenda Kuna mambo mengi sana yamegunduliwa na watakufa sana mbaya zaidi hawa watu ni kama hawana hata tahadhari maana vipigo kwa upande wao ni vingi mno.
Tutegemee time Magu au wenye angalau ka element kauzalendo watapukutishwa vibaya mpaka kufikia 2030. Km wana uwezo wanatakiwa wasichelewe sana kupoteza wakati waamue liwalo na liwe maana kama bado HP wanaye wataendelea kuyajua mengi mno.
 


Rais Samia, amesikitika kutangaza kifo cha William Vangimembe Lukuvi (Mb.), aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) pamoja na Mbunge wa Jimbo la Isimani.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi, Lukuvi amefariki dunia leo tarehe 25 Machi, 2026, majira ya saa moja asubuhi katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, alipokuwa akipatiwa matibabu kufuatia ugonjwa wa mshtuko wa moyo.

Rais Samia ametoa salamu za pole kwa Spika wa Bunge, familia ya marehemu, wananchi wa Jimbo la Isimani, ndugu, jamaa na marafiki, pamoja na Watanzania wote kwa ujumla kufuatia msiba huo.
View attachment 3562430


Historia ya William Lukuvi

William Vangimembe Lukuvi ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri wa Tanzania ambaye amekuwa na mchango mkubwa katika masuala ya ardhi, maendeleo ya makazi, na siasa za kitaifa. Akiwa Mbunge wa Jimbo la Ismani kwa zaidi ya miaka 30 tangu mwaka 1995 mpaka kufariki mwaka 2026, Lukuvi ameshikilia nyadhifa mbalimbali za uwaziri.

Maisha ya Awali na Elimu
William Lukuvi alizaliwa tarehe 15 Agosti 1955 katika kijiji cha Mapogoro, Wilaya ya Iringa Vijijini, Tanganyika. Alipata mafunzo yake ya awali katika Tabora Teachers College (TTC) na baadaye kuhitimu Shahada ya Uzamili katika Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Huria cha Tanzania.

Safari ya Kisiasa
Lukuvi alianza safari yake ya kisiasa kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Ismani mnamo mwaka 1995 kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo ameendelea kushikilia hadi amefariki Dunia March 25, 2026.

Aidha, amehudumu kama Waziri katika nyadhifa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Bunge.

Mnamo Juni 2023, Rais Samia Suluhu Hassan alimteua kuwa Mshauri wa Rais kuhusu Mahusiano ya Kisiasa na Kijamii na baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 Rais Samia alimteua William Lukuvi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) nafasi ambayo ameishikilia mpaka kufariki kwakwe.

Zaidi, Soma=> CV ya William Lukuvi
Hiki kifo kimenipa utata sana hasa niliposikia na ile hotuba waziri wa sanaa kuna maswali mengi ya kujiuliza

🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔
 
Hivi mke wake bado ana duka la furniture pale palm village mikocheni
Nakumbuka wakati harrier sahv mnaziita anaconda mama alivuta ile rangi nyeupe brand new,kipindi hicho bei aliyoivuta alinambia dah ilikuwa above 100m eti sahv kila mtu hko ana miliki
Kuhusu kva megawat kwani yule mzee alikuwa na mambo mengi mbona alikuwa mkimya mgwasu
Mkuu

Ova

Sijatimba kipindi kirefu sana Palm Village ,next month nina Appointment na Millard Ayo nitacheck kama bado lipo.

Noma sana Anaconda kwasasa zipo za kukinga yaani gari zikishaanza kushobokewa price inapungua ipo siku zitafika hadi 20m ni swala la muda tu ,si umeona Range Sports ilikuwa 200m ila sasa Lukosi anauza 30m.

Hawa viongozi kwa nje wanakuwa wakimya ila wana mambo mengi sana ya hovyo ,wewe si uliona Mkuu wa mkoa kanda ya ziwa alikuwa anamla NDOGO binti tu mdogo 18 -20 ,wengi wameungua.
 
Back
Top Bottom