Waziri wa Katiba na Sheria Mwigulu Nchemba awajibu TLS kuhusu Rais Samia Suluhu kuteua Baraza jipya la Mawaziri

Yaani wapinzani kulalamika ni jadi yao! Mnadhani kuna kupumua hapa? Magu spirit will prevail
Hili suala haliwahusu Wapinzani bali linahusu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na ndiyo maana Jiwe wakati wa uhai wake alijiimarisha pekee badala ya kuimarisha mifumo. Hii ni kutokana na kugundua kuwa waliomzunguka wengi wao wana mawazo finyu kama ulivyo wewe.
 
Kama ni ww unayeteua sawa!
Tatizo lenu nyie mataga ni kudhani kuamini kuwa kila anayepinga au kukosoa baadhi ya watendaji wa serikali ya ccm basi ni mpinzani na yupo nje ya system.

Mnafanya kosa kubwa sana
Kwa taarifa yenu humu wengine wapo jirani na meza ya wenye maamuzi ya nchi hii.
 
Mwigulu akija kupata madaraka makubwa, ataumiza na kuua watu mnoooo.

Narudia tena mnooooooooooooooooooo.

Weka madaraka makubwa mbali na Mwigulu. Siyo binadamu kabisa.

Na kibaya zaidi ni bingwa wa uchawa ili apewe vyeo. Kwa mfumo mbovu tulionao, no wonder huyu mtu akaja kuleta maafa tena makubwa mnoo.
Mungu atatutea!! Wako wapi akina farao??
 
Tatizo lenu nyie mataga ni kudhani kuamini kuwa kila anayepinga au kukosoa baadhi ya watendaji wa serikali ya ccm basi ni mpinzani na yupo nje ya system.

Mnafanya kosa kubwa sana
Kwa taarifa yenu humu wengine wapo jirani na meza ya wenye maamuzi ya nchi hii.
Ww ndio taga, aliyekuambia ss hatumo kwenye ' inner circle' ni nani? Ona sasa umesababisha nimejilipua mfyuuuuuu!
 
Ww ndio taga, aliyekuambia ss hatumo kwenye ' inner circle' ni nani? Ona sasa umesababisha nimejilipua mfyuuuuuu!
Ndiyo ujue kuwa haupo sehemu hiyo maana hata the principle Ethics za utumishi hujui
 
Mwigulu kama unajua tupo kwenye majonzi mazito, nguvu ya kuperuse mitandaoni kuitafuta ile doc ya TLS, kuisoma na kuijubunkwa hoja mufilisi umezitoa wapi?

Wewe pia upo unawaza mirathi badala ya mazishi na maslahi yako yapo at high stake kuliko hata hao TLS.
 
Bush lawyer ... nashauri Mwigulu aache kwanza wanaojua sheria walumbane mwisho tutapata muafaka. Halafu hii hulka ya kutaka KUWANYAMAZISHA watu utaiacha lini kaka Mwigulu???
 
Nimesoma andiko la TLS, kwa heshima zote kwa chombo chetu hiki kilichopewa mamlaka kisheria, Nimeshtuka sana, I wish to say,

Kwanza KATIBA HAIJAVUNJWA KWA MHE RAIS SAMIA SULUHU kuapa, na wala hakuna Mkanganyiko wowote wa Kikatiba, kwa yeye kutoteua PM na Baraza jipya. Mmekaa wote kweli mkaona hivyo.

Kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 42(5) kuna watu wa aina mbili wanaweza kuwa Rais. Moja, Rais Mteule ambaye anatokana na Ibara ya 42(1). Mbili, Mtu anayeshika kiti cha Rais ambaye anatokana na ibara ya 37(5) na 50(2)(d) ambaye ni Makamu wa Rais. Kwa Mazingira haya, Makamu wa Rais, baada ya kifo cha Rais, anakuwa Kaimu Rais baadae ndio ameapa na kuwa RAIS wa Nchi. Rais Mteule anapatikana kutokana na uchaguzi. Hivyo basi ibara ya 57(2)(f) ya Katiba haitumiki katika mazingira haya. Kwa mjibu wa Sheria, Mhe Rais alitakiwa kutoa taarifa hii kwenye Baraza la Mawaziri baada ya kuapa na alifanya hivyo, maana yake Baraza lipo.

Hata hivyo kwa tamaduni za Kiafrika, kitanzania na Misingi ya UTU, SIONI KAMA NI JAMBO JEMA SANA KUANZA KUJADILI MGAWANYO WA MADARAKA TUNGALI HATA HATUJAMZIKA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU. HUU SIO MSIBA MDOGO, JAMBO HILI ZITO LIKO MIKONONI MWA RAIS WETU MAMA SAMIA SULUHU, HALAFU SISI TUANZE KUMPATIA MAMBO YA MARA TEUA PM, MARA VUNJA BARAZA, KATIBA INAELEKEZA RAIS KUAPA NA NAMNA YA KUMPATA MAKAMU WA RAIS.

KWA MJIBU WA KATIBA RAIS ANARUHUSIWA KUVUNJA BARAZA MUDA WOWOTE NA KUPANGA ATAKAVYO HATA SIO KWA MAZINGIRA KUAPA KWAKE,

KWANINI HATUIONI HEKIMA YAKE YA KUSHUGHULIKIA MSIBA KUMSITIRI KWANZA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU? TUNAANZA NA MAZISHI AU MIRATHI? 😭😭😭😭

Pia soma > TLS: Kwa Mujibu wa Katiba, sasa Tanzania haina baraza la Mawaziri, Rais Samia atakiwa kuteua Waziri Mkuu ndani ya siku 14
Kwa hekima na busara kabisa Miwigulu Nchemba pamoja na kuwa wewe ni waziri wa sheria ulitakiwa ukae kimya tu katika hili kwasababu wewe una mgongano wa ki-maslahi katika bandiko la TLS.

Kwasababu Mh. Rais akiamua kulivunja Baraza la Mawaziri na wewe utakuwa muathirika No. 1. Kwahiyo tunakushauri Mwigulu Nchemba kaa kimya katika hili usitake kuwavuruga watu kwenye huu mjadala muhimu.
 
Huyu mama Samia asipoiga udikteta wa jiwe kwa hizi siku mbili tatu watampasua kichwa kwa maushari na makelele kitoka kila kona,hawa TLS walikuwaga wapi kipindi kile Jiwe linaikanyaga Katiba na kufanya neno lake kuwa sheria
Mama umeshaapa katiba yetu inakupa madaraka makubwa Sana!! Mtu asikupangie!! Fanya uonavyo vyema ili maadamu unacheza kwenye mamlaka Yako.
Inavyoelekea watu wanataka kukujaribu!! Mtangulizi wako aliwaambia wazi: "mimi sijaribiwi". Waonyeshe kwa vitendo wanaokujaribu kuwa haujaribiwi!! Mungu yuko pamoja nawe na watanzania walio wengi wako pamoja nawe!! Hawa wachache wanaopiga makelele wala usihangaike nao, wadharau tu! Watachoka na kuacha wenyewe!! Mfano mdogo tu, kwani TLS imeanza leo? mbona ilikuwa kimya mpaka tulishaisahau? Ni kwa sababu mbinu zao za kiharakati zilidharaulika!!
 
Back
Top Bottom