Mwigulu Nchemba-Out of touch. Anasema hakuna wizi serikalini, Rais ampa mfano wa mtandao wa wizi Mbeya

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,333
24,227
View attachment 2933564
IMG-20240313-WA0121.jpg
IMG-20240313-WA0122.jpg



#Habari: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi wateule kusimamia tatizo la wizi wa fedha unaofanywa na watumishi wa umma kwa kushirikiana na mitandao mingine nje ya serikali.

Rais Samia ameyasema hayo leo tarehe 13 Machi, 2024 wakati akiwaapisha viongozi wateule wakiwemo wakuu wa mikoa wapya na waliohamishwa vituo vya kazi na viongozi wengine katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam.

"Nataka mkasimamie pia mifumo ya ukusanyaji mapato, watu wanaiba fedha watu wote mko hapo, wakuu wa mikoa na wilaya mko hapo, kuna mitandao inachepusha fedha za halmashauri huko, kuna mtandao wa serikali na mtandao mwingine unaochepusha pesa, nashukuru Mbeya wamekuwa wa kwanza kutuambia tunafuatilia huo mtandao, na upo unaenda na wanaambizana wanachepusha pesa nyingi sana, lakini bado mnakaa huko sijui kitu gani kimeharibika mnahitaji pesa zinatoka wapi?"

Rais Samia


Dokta wa Uchumi kalewa kazi.
Amejitamba hadharahi kuwa sasa hakuna wizi wa fedha serikalini, na kwamba mama Samia kafanya makubwa kutokomeza kabisa wizi wa fedha za umma serikalini.

Mama kamgutua.
Ametoa mfano wa mtandao wa wizi wa fedha za serikali huko Mbeya.
Fedha zinaingia moja kwa moja mifukoni mwa watendaji wachache wajanja.

Dr Mwigulu Nchemba kalewa madaraka, uwaziri umemkolea hadi anasahau kazi.
Hili ni tatizo.

====
Oktoba 28, 2023 Dkt Mwigulu Nchemba alisema hakuna wizi wa fedha serikalini.
 
Kwahio kwenye hili Mama ni Safi kabisa Mwigulu ndio mbaya ? Huku ndio kulaumu mkono kwa kuiba badala ya mtu as a whole....

Lawama ziende kwa Serikali kwa Ujumla bila kusahau Kiongozi wao (Haya mambo ya kupeana lawama kwa Mafungu ni kutoana Mbuzi wa Kafara)
 
View attachment 2933564View attachment 2933565View attachment 2933566


#Habari: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi wateule kusimamia tatizo la wizi wa fedha unaofanywa na watumishi wa umma kwa kushirikiana na mitandao mingine nje ya serikali.

Rais Samia ameyasema hayo leo tarehe 13 Machi, 2024 wakati akiwaapisha viongozi wateule wakiwemo wakuu wa mikoa wapya na waliohamishwa vituo vya kazi na viongozi wengine katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam.

"Nataka mkasimamie pia mifumo ya ukusanyaji mapato, watu wanaiba fedha watu wote mko hapo, wakuu wa mikoa na wilaya mko hapo, kuna mitandao inachepusha fedha za halmashauri huko, kuna mtandao wa serikali na mtandao mwingine unaochepusha pesa, nashukuru Mbeya wamekuwa wa kwanza kutuambia tunafuatilia huo mtandao, na upo unaenda na wanaambizana wanachepusha pesa nyingi sana, lakini bado mnakaa huko sijui kitu gani kimeharibika mnahitaji pesa zinatoka wapi?"

Rais Samia



Dokta wa Uchumi kalewa kazi.
Amejitamba hadharahi kuwa sasa hakuna wizi wa fedha serikalini, na kwamba mama Samia kafanya makubwa kutokomeza kabisa wizi wa fedha za umma serikalini.

Mama kamgutua.
Ametoa mfano wa mtandao wa wizi wa fedha za serikali huko Mbeya.
Fedha zinaingia moja kwa moja mifukoni mwa watendaji wachache wajanja.

Dr Mwigulu Nchemba kalewa madaraka, uwaziri umemkolea hadi anasahau kazi.
Hili ni tatizo.

====
Oktiba 28, 2023 Dkt Mwigulu Nchemba alisema hakuna wizi wa fedha serikalini.
Shida anaongea sana badala ya kupita na vichwa yeye anaongea au wezi kuwahamishia kwingine.
 
Katika mawaziri wachache wanaojitqmbua. Bashe akiwa mmoja wapo ana behave kama waziri muda wote akitoa maelezo ana figure, data from credible government sources na justification.

Bashe pia anapokwaruzana na watu huko serikalini ana maelezo ya sababu za kisera kwanini anawavaa. Also it must be said mipango yake uwa ni ovyo kutokana na limitations zake to how things work. Matokeo yake mwisho wa siku anaishiaga kubomoa zaidi kuliko kujenga. But still he comes across as ministerial figure to how he represent himself.

Huyo Mwigulu hana tofauti na Steve Nyerere anaetuambia SGR ipo majaribioni muda si mrefu tutaenda mwanza kwa siku moja. Haya ndio aina ya mambo Mwigulu anayoongelea mara nyingi ropo ropo kama chawa wa mtaani na sio mtu mwenye mamlaka makubwa serikalini.
 
Back
Top Bottom