Opportunity Cost
JF-Expert Member
- Dec 10, 2020
- 9,035
- 6,907
Unaota wewe,soma hiyo 👇.4.5T zinamwagwa mtaani kuchochea uchumiMwigulu Nchemba anakuharibia maana hakuna sehemu amewahi kuwepo na kufanya jambo la maana zaidi ya kujenga chuki na mwisho wa siku lawama zinaenda kwa aliyemteua.
Mwigulu anayafanya haya akifikiri anakufurahisha lakini sidhani kama anakufurahisha bali anakupa mtihani katika Serikali yako.
Kama Serikali imeweza kuwasamehe wahujumu uchumi mabilioni ya fedha waliyoiibia Serikali inakuwaje Serikali hiyohiyo inakwapua kile kidogo cha mwananchi wa kawaida tena kimabavu kabisa.
Mh Rais SSH huyu waziri Mwigulu Lameck Nchemba hapaswi kuwepo katika ofisi yoyote ya Umma.