Waziri Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amewaahidi wafanyabiashara wa soko la Mchele la Magugu mkoani Manyara kufanyia kazi kero ya utozaji wa ushuru

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944

WAZIRI ASHATU KIJAJI AAHIDI KUTATUA KERO YA UTOZAJI USHURU KWA WAFANYABIASHARA WADOGO MKOA WA MANYARA

Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amewaahidi wafanyabiashara wa soko la Mchele la Magugu mkoani Manyara kufanyia kazi kero ya utozaji wa ushuru wa Shilingi 1500 kwa mfuko wa ujazo wa kilo 50 na kwa kushirikiana na Waziri wa Kilimo pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi.

Waziri Kijaji ametoa ahadi hiyo Mei 12, 2023 alipotembelea soko la Mchele la Magugu mkoani Manyara na kukutana na Wafanyabiashara kwa lengo la kujionea hali ya biashara katika soko hilo wakati wa mwanzo wa msimu wa mavuno ya Mpunga kwa mwaka 2023.

Wakiongea na Waziri Kijaji, Wafanyabiashara wa Magugu wameipongeza Serikali kwa kusaidia kuboresha mazingira ya Wafabyabiashara wadogo na wameiomba Serikali iwapunguzie tozo ya ushuru wa Shilingi 1500 kwa mfuko wa ujazo wa kilo 50 kwa kuwa inaongeza gharama katika biashara.

Aidha, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ameshiriki Mkutano wa 15 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika tarehe 12/5/2023 jijini Arusha. Mkutano huo pamoja na mambo mengine umejadili masuala ya kibajeti ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.28(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.28(1).jpeg
    54.2 KB · Views: 8
  • WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.28.jpeg
    WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.28.jpeg
    41.5 KB · Views: 6
  • WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.27(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.27(2).jpeg
    40.2 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.26(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.26(2).jpeg
    52.1 KB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.27.jpeg
    WhatsApp Image 2023-05-14 at 11.37.27.jpeg
    39 KB · Views: 5

WAZIRI ASHATU KIJAJI AAHIDI KUTATUA KERO YA UTOZAJI USHURU KWA WAFANYABIASHARA WADOGO MKOA WA MANYARA

Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amewaahidi wafanyabiashara wa soko la Mchele la Magugu mkoani Manyara kufanyia kazi kero ya utozaji wa ushuru wa Shilingi 1500 kwa mfuko wa ujazo wa kilo 50 na kwa kushirikiana na Waziri wa Kilimo pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi.

Waziri Kijaji ametoa ahadi hiyo Mei 12, 2023 alipotembelea soko la Mchele la Magugu mkoani Manyara na kukutana na Wafanyabiashara kwa lengo la kujionea hali ya biashara katika soko hilo wakati wa mwanzo wa msimu wa mavuno ya Mpunga kwa mwaka 2023.

Wakiongea na Waziri Kijaji, Wafanyabiashara wa Magugu wameipongeza Serikali kwa kusaidia kuboresha mazingira ya Wafabyabiashara wadogo na wameiomba Serikali iwapunguzie tozo ya ushuru wa Shilingi 1500 kwa mfuko wa ujazo wa kilo 50 kwa kuwa inaongeza gharama katika biashara.

Aidha, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ameshiriki Mkutano wa 15 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika tarehe 12/5/2023 jijini Arusha. Mkutano huo pamoja na mambo mengine umejadili masuala ya kibajeti ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Shida ya kula ugoro.....mchele kahama ushuru ni 700 kwa mfuko
 
Back
Top Bottom