Waziri Kangi Lugola ameipindua Bendera ya Taifa

Waziri Kangi Lugola ameipindua Bendera ya Taifa

Baada ya kuteuliwa kuwa waziri wa mambo ya ndani Mh Kangi Lugola amebuni vazi lake jipya ambalo amebandika Bendera ya Taifa kifuani upande wa kushoto, kulia na pia kwenye mikono na kama hiyo haitoshi anatembea na ilani ya CCM ambapo amenukuliwa akisema akifa azikwe na ilani ya chama hicho ya wakati huo kwakuwa kwake hakuna Ilani kama ya CCM na anapenda kutembea nayo katika utelelezaji wa shughuli za Kiserikali.

Lakini ukiangalia vizuri hilo vazi lake ni kuwa utagundua amegeuza mkao wa Bendera ya Taifa aliyoibandika upande wa kulia wa vazi lake ameipindua badala ya mistari ya njano na nyeusi kuelekea juu ikitokea kona ya chini upande wa kushoto kuelekea kona ya juu kulia yeye kaiweka ikitokea kona ya juu kushoto kuelekea kona ya chini kulia. Ile iliyopo upande wa kushoto ndio imekaa kwa usahihi hivyo hata hiyo ya kulia inapaswa aiweke kama hiyo ya kushoto.

Haitakiwi kuigeuza hiyo bendera kwa namna yoyote ile. Amwambie fundi wake airekebishe vinginevyo anazidi kujiabisha.

36836040_1940956792634972_6709772448692174848_n.jpg
Mhhhhm Sasa mkuu hiyo suruali ina kuhusu nini mbona imempendeza tu? Ila ahsante kwa kutuonyesha
 
Mhhhhm Sasa mkuu hiyo suruali ina kuhusu nini mbona imempendeza tu? Ila ahsante kwa kutuonyesha
Mie nimezungumzia hiyo bendera alivyoiweka visivyo. Hiyo suruali ndio kama ulivyoiona imemtoa fresh pamoja na raba zake ila ilani angemwachia polepole yeye adili na katiba na sheria za nchi. Ila kwa jinsi alivyoanza ameshachemsha. Yeye anamtimuaje mtendaji wake mkuu hadharani? Huko ni kudhalilishana kusikokuwa na sababu unless awe hajui matumizi ya ofisi. Hii yote ni kutokana na kufanya kazi kwa media kutafuta umarufu.
 
Kumbuka yeye ni Waziri wa mambo ya ndani usalama wa raia waliokusanyika kuipokea ndege unamuhusu na hata usalama wa Rais pia unamuhusu bado pia yeye km waziri wa Mambo ya ndani akitoka hapo anaelekea kazini kuendelea na majukumu mengine
Waziri na raba ofisini? Unajua vazi la ofisini kweli? Huyu anatakiwa azuiwe getini asiingie kabisa ofisini na kiatu hicho, mkuu kuna vazi la ofisini na la kijiwe cha kahawa sio kila vazi linavaliwa popote
 
Wallah hapa nilipo machozi yanatoka kwa kucheka yaani kila comment inaishinda nyingine
Hapo ilikuwa ni wakati wa wimbo wa taifa. Waliokosea kusimama inavyotakiwa hapo ni Mengi, Mrema, mchungaji na mama kushoto kwa mchungaji anayeangalia chini. Wakati wa wimbo wa taifa kwa Tanzania mikono inakuwa usawa wa miguu kama alivyosimama Mwakyembe, Sheikh, Ninja mwenyewe na wengineo. Jinsi alivyosimama Mengi ni kama anaimba wimbo wa Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote(patriotic song)
 
suluali yake sasa utazani ile mifuko ya kwenye mashine za kusagia....waziri hajua ata kuvaaa....sijui kaokotwa wapi huyu
 
Yaani upuuzi mtupu. Tunajadili bendera umegeuzwa kweli?
 
Baada ya kuteuliwa kuwa waziri wa mambo ya ndani Mh Kangi Lugola amebuni vazi lake jipya ambalo amebandika Bendera ya Taifa kifuani upande wa kushoto, kulia na pia kwenye mikono na kama hiyo haitoshi anatembea na ilani ya CCM ambapo amenukuliwa akisema akifa azikwe na ilani ya chama hicho ya wakati huo kwakuwa kwake hakuna Ilani kama ya CCM na anapenda kutembea nayo katika utelelezaji wa shughuli za Kiserikali.

Lakini ukiangalia vizuri hilo vazi lake ni kuwa utagundua amegeuza mkao wa Bendera ya Taifa aliyoibandika upande wa kulia wa vazi lake ameipindua badala ya mistari ya njano na nyeusi kuelekea juu ikitokea kona ya chini upande wa kushoto kuelekea kona ya juu kulia yeye kaiweka ikitokea kona ya juu kushoto kuelekea kona ya chini kulia. Ile iliyopo upande wa kushoto ndio imekaa kwa usahihi hivyo hata hiyo ya kulia inapaswa aiweke kama hiyo ya kushoto.

Haitakiwi kuigeuza hiyo bendera kwa namna yoyote ile. Amwambie fundi wake airekebishe vinginevyo anazidi kujiabisha.

36836040_1940956792634972_6709772448692174848_n.jpg


People are not after one's appearance, they need deliverables and solutions to their problems
 
Jamaa kavaa kishamba sana kama kawaida ya watu wa kanda ya ziwa hiyo suti na raba kama mbingu na ardhi

don't generalise watu wa kanda ya ziwa,kuwa specific na mkoa anapotokea mlemgwa wa mada hii.au unawaogopa?
 
Na shehe naye kavaa Sandro's mbona hamumzemi
Mkuu,ukimuona mtu kavaa Kanzu au Joho na buti au raba ujue huyu mshamba,hizo nguo zinakwenda na sandales,mitarawanda au unaweza kuvaa hata kanda mbili, lakini huwezi kuvaa raba au buti kama umevaa hizi nguo,Sheikh hajakosea,amevaa inavyotakiwa

Mkuu,na wewe wa kanda ya ziwa nini😀
 
Hivyo nani kawaambia wavae bendera ya taifa siku hizi? Aliyepigania uhuru hakuivaa vipi hawa?
Wanaona wao ndio wazalendo halisi kumzidi hata Nyerere. Pia wao wanajifanya kukipenda chama na kukijua zaidi kuliko Nyerere ndio maana wanasema wanataka wazikwe na ilani ya chama
36975845_504761559942917_5612737466562772992_n.jpg
36959190_504761663276240_502062671672115200_n.jpg
 
Back
Top Bottom