Baada ya kuteuliwa kuwa waziri wa mambo ya ndani Mh Kangi Lugola amebuni vazi lake jipya ambalo amebandika bendera ya taifa kifuani upande wa kushoto, kulia na pia kwenye mikono na kama hiyo haitoshi anatembea na ilani ya CCM ambapo amenukuliwa akisema akifa azikwe na ilani ya chama hicho ya wakati huo kwakuwa kwake hakuna Ilani kama ya CCM na anapenda kutembea nayo katika utelelezaji wa shughuli za Kiserikali.
Lakini ukiangalia vizuri hilo vazi lake ni kuwa utagundua amegeuza mkao wa bendera ya taifa aliyoibandika upande wa kulia wa vazi lake ameipindua badala ya mistari ya njano na nyeusi kuelekea juu ikitokea kona ya chini upande wa kushoto kuelekea kona ya juu kulia yeye kaiweka ikitokea kona ya juu kushoto kuelekea kona ya chini kulia. Ile iliyopo upande wa kushoto ndio imekaa kwa usahihi hivyo hata hiyo ya kulia inapaswa aiweke kama hiyo ya kushoto. Haitakiwi kuigeuza hiyo bendera kwa namna yoyote ile. Amwambie fundi wake airekebishe vinginevyo anazidi kujiabisha