Mkuu naomba unisaidie majibu ya maswali haya kwa niaba ya January
1. Ni Lini January Makamba alijua uhusiano wa dada yake na Muitaliano?
2. Je January anaweza kueleza uhusiano wa muitaliano na dada yake ulikuwa ni uhusiano wa namna gani? Na ulianza lini?
3. Je January mwenyewe ameshawahi kuonana na Muitaliano?
4. Je January amewahi kuongea kwenye simu na huyo Muitaliano?
5. Muitaliano kwenye clip anasema kuwa kila alipoomba kuonana na January, Mh. January alimtumia Mzungu fun Meseji, sasa Je January katika kumbukumbu zake anakumbuka kuwahi kumtumia meseji zozote mzungu?
6. Kama jibu ndio alimtumia meseji mzungu wa kiitaliano alikuwa anamtumia meseji za kusema nini?
7. Ni lini January alijua kuwa huyu Muitaliano si mtu safi, Ni tapeli, hana wasifu wa kuwa karibu na waziri?
8. Je ni kweli kwamba January alipokea pesa kutoka kwa Muitaliano kwa ajili ya Bumbuli Development Corporation (BDC)
9. Kama ni kweli Muitaliano alichangia Mfuko wa Bumbuli Je, Huyu bwana alichangia hali January akijua kuwa huyu Muitaliano si safi na akapokea hizo pesa??
10. Je January anadhani ni sahihi kwa waziri kuwa na mahusiano ya karibu, au kufahamiana, au kufanya biashara, au kupokea mchango, au zawadi au kuwasiliano na mtu ambaye ni Tapeli na anayetumia madawa ya kulevya na anadaiwa madeni lukuki mpaka ameshindwa kutoka nchini?
Ingekuwa awamu iliyopita ningekuwa na mashaka kuw amambo yafuatayo yatafanyika.
a. TCRA wataamlishwa kufuta data zote za mawasiliano ya simu ya January na Huyo muitaliano kama yalikuwepo
b. Polisi wataamuliwa kwenda kumkamata muitaliano na kumuweka ndani kasha kumfungulia charge za makosa ya kuishi nchini kinyume cha sheria, makosa ya mitandao, madeni na hata matumizi ya madawa ya kulevya
Sijui Serikali ya Awamu ya 5 Serikali ya Magu itabehave vipi kwenye hili.