Wazazi kuna hizi shule za English Medium ni majina tu ila ni takataka. Lakini bado zipo!

Basi hilo nakusamehe....

Haya wewe teacher wa English... Nipe forms za Verb 'be' ..

Wapumbavu nyinyi mnakula hela zetu kichwani weupe.. failures..
Punguza makasiriko, kunywa maji, Tafuta hela
 
Embu fikiria mtoto wako wa std six hajui Mkoa gani huanza kabla ya kufika Dar...!?? Geography.

Au hajui Verb forms za Verb 'be'.. English.

Wazee..! Kuna ujinga na tunapigwa. Nilitaka wasafirisha wanangu waende holidays ila nimekuta weupe. Naingia nao Class. I'm a teacher...

Walimu Wao ntakutana nao January.
Mkoa unaoanza kwenye nini, ukubwa, umaarufu, wingi wa viwanda au kwenye alphabeti.
 
Tatizo ni wanao na wewe mwenyewe...
Sasa hilo swali lako hata mimi sijui..
Mkoa kabla ya Dar..
Kutokea wap?
Kwa kutumia usafiri gani?
Dar inapakana na Mkoa mmoja tu wa Pwani, uwe umetokea Kaskazini, Kusini au Magharibi. Mashariki tu ndio inapakana na Nchi ya Zanzibar.
 
Mkuu
Kuna kipindi EATV kinaitwa skonga
Kuna segment ya kuuliza maswali
Ukisikiliza majibu ya watoto wale kama wewe ni mwalimu unaweza chapa shule nzima watoto ni weupee
Yaani hamna kitu

Achana na hao nenda chuo kikuu ndio utachoka

Kuna wanafunzi wa UDSM wanaosoma maswala ya siasa
Waliulizwa swali hili

"Barabara ya mwenge kwenda ubungo inaitwa Sam Nujoma Road, je huyu Sam Nujoma ni nani?

Hakuna mwanafunzi alipata hili swali
Nilisikitika sana, kuona mwanafunzi wa UDSM anasoma Mambo ya siasa afu hajui swali dogo kama hilo
Duu! Hii kiboko. Mwanafunzi wa Chuo Kikuu anasomea Siasa hamjui Sam Nujoma. Elimu yetu iko taabani. Kumbe ndio maana wakija huku makazini wengi wao uwezo wao ni mdogo sana. Unabaki unajiuliza ina maana hizi Shahada zao wanapewa tu?
 
Badilisha namna ya kupima uwezo wa watoto wako...
Hii likizo wafundishe stadi tofauti za maisha...acha kuwachosha
Jinsi ya kutengeneza funza kwa kutumia kinyesi cha ng'ombe
Jinsi ya kupanda mbogamboga kwenye magunia
Jinsi ya kutengeneza kiti cha mbao
N.k n.k..
Oya mzazi nifundishe kutengeneza wadudu kwa mbolea basi maana sielewi ila natamani .

Note :Usidhani mimi kilaza kama watoto wa mshikaji wangu blogger nipo njema kwenye mambo mengine ya dunia hasa Afya na starehe .

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Kuna wanafunzi wa UDSM wanaosoma maswala ya siasa
Waliulizwa swali hili
"Barabara ya mwenge kwenda ubungo inaitwa Sam Nujoma Road, je huyu Sam Nujoma ni nani?
Inaelekea tatizo ni kubwa kwa wazazi, na si walimu wala watoto. Sasa kumjua Sam Nujoma ni suala la siasa?
 
Duu! Hii kiboko. Mwanafunzi wa Chuo Kikuu anasomea Siasa hamjui Sam Nujoma. Elimu yetu iko taabani. Kumbe ndio maana wakija huku makazini wengi wao uwezo wao ni mdogo sana. Unabaki unajiuliza ina maana hizi Shahada zao wanapewa tu?
kuna yale mashindano ya AIRTEL vyuo vikuu africa,ilikutana tanzania,kenya,nigeria na south africa
wajinga wa kwanza tulikua sisi kila tukielekezewa mpaka kengere inalia jibu halijapatikana.

Sent from my Redmi Note 8 using JamiiForums mobile app
 
kuna yale mashindano ya AIRTEL vyuo vikuu africa,ilikutana tanzania,kenya,nigeria na south africa
wajinga wa kwanza tulikua sisi kila tukielekezewa mpaka kengere inalia jibu halijapatikana.

Sent from my Redmi Note 8 using JamiiForums mobile app
Hivi yale mashindano bado yapo..?

Kama yapo yanaonyweshwa kwenye decoder gani, lini, ....?

Pale kama ubongo wako umejaza mashairi ya kina mboso lazima uzalilike peupee 😂😂
 
Back
Top Bottom