Shule za English Medium ni kiwanda cha kuongeza Depression kwa wazazi na watoto. Serikali iboreshe shule za umma

FRESHMAN

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
8,822
33,527
Wazazi wengi wana msongo wa mawazo kutokana na stress za kutafuta ada za shule za kina junior wao wanaosoma english medium eg. Atlas, Tusiime, etc. Muda wa kulipa ada ukifika mzazi anakuwa na hasira hasira tu sababu ya msongo wa mawazo

1700041651299.jpeg
Watoto na wao wana msongo wa mawazo kutokana na ratiba ya shule zao hizo za kisasa english medium. School bus inakuja saa 11 alfajiri na kumrudisha saa 12 jioni. Hapo mtoto kabebeshwa bonge la begi mgongoni lenye vitabu ma madaftari ya masomo yote.

Hapo hapo hapati muda wa kupumzika wala kucheza ku enjoy utoto wake, maana kila siku ana home work, na likizo hakuna kufunga shule kisingizio ni kujiandaa na mitihani. Hapo Mtoto anapata depression toka utotoni maskini.

Pili hizi shule zina fake lifestyle, zinamfundisha mtoto softlife ambayo mtaani hakuna hiyo soft life. Vitu kama kufanyiwa usafi, kufatwa na school bus, mtoto huyu huyu akija kukutana na maisha halisia ya kugombea mwendokasi ama daladala anaona anaonewa.

Hapo tena mtoto anakuwa na depression akikosa hiyo soft life after school. Tukumbuke schooling is a lifestyle not a place. Mtu aliyezoea soft lifestyle lazima apate depression akikutana na real life.

Pia hii tabia ya wazazi ku buy education at high price kunawafanya wazazi washindwe kuwekeza kwenye assets zingine ili watoto wao wapate hata pa kuanzia mbeleni.

Mzazi anaishi nyumba ya kupanga ila anatumia milioni 10 kila mwaka kulipia watoto wake ada Atlas ama Tusiime. Mzazi huyu anashindwa kujenga nyumba ya familia yake ama kuanzisha miradi. Siku huyu mzazi akiumwa ama kufukuzwa kazi anakunywa sumu.

Ushauri kwa wazazi ambao bado hatujawekeza vya kutosha tuwe makini na hizi shule za english medium za kisasa.

Serikali pia ibadilike. Demand ya hizi shule ni kubwa sana, waongeze shule za umma, english medium ziwe nyingi. Sio Olimpio na Bunge tu.

Pia Jeshi la kujenga taifa ( JKT) pia.. lisiishie kuwekeza kwenye kujenga kumbi za harusi, kujenga fremu, bar na mambo ya catering tu JKT lingewekeza kwenye low cost english medium primary schools kwenye miji mikubwa. Bei za ada zao ziwe kama olimpio na bunge.
 
Hakuna asiesota kwenye depression ya mtaa kwa sababu wasomi karibu wote, wanachokitarajia sio wanachokipata,

Kwa hiyo ni kheri kumfundisha mtoto elimu sahihi ya fedha toka nyumbani ili asije shindwa hata kulipa dada wa kazi wa kumpa hiyo soft life maana in reality, hakuna asiyeipenda

Kingine kwa dunia ya sasa, depression kwa mzazi haepukiki na kheri shule kama kuna extra activities, mzazi anakuwa na uhakika wa usalama wa mtoto pahali alipo kuliko huku kitaa ambapo hujui, yupo na nani na anafanywa nini au umuache nyumbani kumbe kuna mdogo wako ambaye balehe inachemka.. Niishie hapa
 
Utawakiwa vibaya mno, watakuambia tafuta hela, wana majibu mabaya, ukweli ndiyo ulivyo kwa shule hizo za fasheni. Utakuta mwingine ni hohehahe eti naye atajikakamua apeleke mtoto wake huko ili aonekane anazo kutaka sifa za kijinga huku akiumia.

Kwanza hiyo elimu inayotolewa huko ni ya kawaida tu kama ya umma na haina maajabu ya kumfanya mtoto awe fiti kimasomo. Labda ataambulia kiiengereza cha kubabaisha
 
Wazazi wengi wanaowapeleka watoto kwenye hizo shule wanajiweza.
Nyumbani kuna gari au safari ni kwa uber, bolt, taxi nk.

Nenda siku za kufunga au kufungua shule uone hadhi za wazazi na ndinga zinazoshusha wanafunzi hapo Tusiime.

Na pia mzazi una uhuru wa kuchagua ni wapi umpeleke mwanao, yaani serikali iumize kichwa kwa uchaguzi wako mbovu. Shule za bei rahisi zipo huko private hujashikiwa bastola mkuu.
 
Kuna ukweli hapo kwenye watoto kuwa 'soft'

Mimi nimesoma hizo shule kwanzia primary mpaka sekondari, kiufupi kuna mtazamo flani tunakua nao, unakua hujazoea shida, unakua mlalamikaji sana, unaona maisha ni marahisi.....

Ni tatizo kwa kweli mimi mwenyewe najaribu kujibadilisha baada ya kufika chuo na kuanza kuona uhalisia wa maisha....

vitu vidogo vidogo kama kupika, kubudget hela vinatushinda kwa kweli.....

Ni vyema mtoto apitie ugumu kidogo ila awe 'flexible' kwenye maisha, kudekezwa raha ila unachelewa kukua....

Haya ni maoni yangu tu....
 
Kuna ukweli hapo kwenye watoto kuwa 'soft'

Mimi nimesoma hizo shule kwanzia primary mpaka sekondari, kiufupi kuna mtazamo flani tunakua nao, unakua hujazoea shida, unakua mlalamikaji sana, unaona maisha ni marahisi.....

Ni tatizo kwa kweli mimi mwenyewe najaribu kujibadilisha baada ya kufika chuo na kuanza kuona uhalisia wa maisha....

vitu vidogo vidogo kama kupika, kubudget hela vinatushinda kwa kweli.....

Ni vyema mtoto apitie ugumu kidogo ila awe 'flexible' kwenye maisha, kudekezwa raha ila unachelewa kukua....

Haya ni maoni yangu tu....
Wewe hukufundishwa vizuri nyumbani sio shuleni,
Hakuna shule Tz hii inafundisha kupika, sijui kubudget pesa zako (unless usomee mapishi au uhasibu)
Wew tu home walikudekeza na walikupa pesa nyingi mno bila bajet hahah,

Sorry mkuu ila ndio ukweli
 
Kuna ukweli hapo kwenye watoto kuwa 'soft'

Mimi nimesoma hizo shule kwanzia primary mpaka sekondari, kiufupi kuna mtazamo flani tunakua nao, unakua hujazoea shida, unakua mlalamikaji sana, unaona maisha ni marahisi.....

Ni tatizo kwa kweli mimi mwenyewe najaribu kujibadilisha baada ya kufika chuo na kuanza kuona uhalisia wa maisha....

vitu vidogo vidogo kama kupika, kubudget hela vinatushinda kwa kweli.....

Ni vyema mtoto apitie ugumu kidogo ila awe 'flexible' kwenye maisha, kudekezwa raha ila unachelewa kukua....

Haya ni maoni yangu tu....
Toto soft hili...mara nyingi mashoga wanatokeaga medium schools
 
Wew hukufundishwa vizuri nyumbani sio shuleni,
Hakuna shule Tz hii inafundisha kupika, sijui kubudget pesa zako (unless usomee mapishi au uhasibu)
Wew tu home walikudekeza na walikupa pesa nyingi mno bila bajet hahah,

Sorry mkuu ila ndio ukweli
wengi tupo hivyo si nipo nao mimi nawaona😅

ila umeongea ukweli
 
Wazazi wengi wanaowapeleka watoto kwenye hizo shule wanajiweza.
Nyumbani kuna gari au safari ni kwa uber, bolt, taxi nk.

Nenda siku za kufunga au kufungua shule uone hadhi za wazazi na ndinga zinazoshusha wanafunzi hapo Tusiime.

Na pia mzazi una uhuru wa kuchagua ni wapi umpeleke mwanao, yaani serikali iumize kichwa kwa uchaguzi wako mbovu. Shule za bei rahisi zipo huko private hujashikiwa bastola mkuu.
Una majibu mabovu kiasi one would stop and wonder if it’s a human speaking or a toilet overflowing with .

Na hata hiyo Tusiime huijui na huna uelewa wa unachokisema.
 
Kuna ukweli hapo kwenye watoto kuwa 'soft'

Mimi nimesoma hizo shule kwanzia primary mpaka sekondari, kiufupi kuna mtazamo flani tunakua nao, unakua hujazoea shida, unakua mlalamikaji sana, unaona maisha ni marahisi.....

Ni tatizo kwa kweli mimi mwenyewe najaribu kujibadilisha baada ya kufika chuo na kuanza kuona uhalisia wa maisha....

vitu vidogo vidogo kama kupika, kubudget hela vinatushinda kwa kweli.....

Ni vyema mtoto apitie ugumu kidogo ila awe 'flexible' kwenye maisha, kudekezwa raha ila unachelewa kukua....

Haya ni maoni yangu tu....
Asipitie magumu, bali ayaishi maisha halisi na siyo ya kwenye Tv.

Siku hizi hadi majina ya watoto tunatoa kwenye Tv eti Frozen, sijui Snowwhite!

A very plastic generation!
 
Wew hukufundishwa vizuri nyumbani sio shuleni,
Hakuna shule Tz hii inafundisha kupika, sijui kubudget pesa zako (unless usomee mapishi au uhasibu)
Wew tu home walikudekeza na walikupa pesa nyingi mno bila bajet hahah,

Sorry mkuu ila ndio ukweli
Shule niliyosoma Mimi primary na secondary mpaka high school, tulikua na Cookery Classes, Sewing classes, Farming & Gardening projects, home keeping na family nurturing.

Hazikua ‘english mediums’ na hizo shule zipo mpaka leo na bado hayo masomo yapo mpaka leo.
 
FRESHMAN naomba uzungumzie huu uwekezaji uliofanywa na ajira zinazotolewa kwenye hizo 'english medium schools/private secondaryschools' na ukiweza tuambie wazazi wote wakipeleka watoto wao kwenye shule za umma, hizi shule zifungwe?
 
Shule niliyosoma Mimi primary na secondary mpaka high school, tulikua na Cookery Classes, Sewing classes, Farming & Gardening projects, home keeping na family nurturing.



Hazikua ‘english mediums’ na hizo shule zipo mpaka leo na bado hayo masomo yapo mpaka leo.
Upo sahihi, ila shule zinazofundisha hayo kwa sasa si ajabu kwa mkoa ikawa moja au isiwepo kabisa,

Huyo jamaa hapo wazazi wake tu hawakumpa malezi ya kupika na kubajet,
Huyo hata angeenda kayumba bado asingejua kubajeti au kupika, in short alidekezwa, na hilo sio kosa la shule, ni kosa la home kwao
 
wengi tupo hivyo si nipo nao mimi nawaona😅

ila umeongea ukweli
Ila mkuu, hata muwe 1000 wenye hio shida ila mm naona wakupewa lawama ni home, hamkupewa nafasi ya kupika au kupewa pesa kwa bajeti, mliachiwa pesa kama zote na mkapikiwa na house girls, kitu ambacho hata mngeenda Kayumba msingejifunza kabisa, kwa hio usilaumu shule, anza kujifunza kupika YouTube+ kubajet pesa pia hujachelewa,

Jifunze sasa
 
Kifupi shuleni kwa sasa watoto wanaenda tu kukua kwasababu elimu yetu inafundisha kuajiriwa wakati wakati sio uhalisia.

Kwahiyo tuchague sehemu salama ya watoto wetu kwenda kukua.
Lkn nikipongeze mtoa maada umetoa tafakuli nzuri
 
Back
Top Bottom