Wazazi hawataki nioe Mchaga

Wazazi hawataki nioe Mchaga

Status
Not open for further replies.
Habari,

Nina mchumba wangu ambaye nimepanga kwenda kujitambulisha kwao mwezi huu August lakini kwa sasa niko kwenye hali ngumu kwa kuwa wazee wangu wa huku Meru hawataki nioe Mchaga na wanasema ni bora ningeoa Mmeru kuliko Uchagani wakitoa sababu tofauti tofauti.

Mchumba wangu huyu ni mchanganyiko wa Mkibosho(mama) na Mmachame(baba) ingawa nilishakuwa na uhusiano na binti wa Kimeru na ndio wamekazia hapo?

Nifanyeje? Hivi ingawa ni tabia ya mtu binafsi lakini nani zaidi kati ya Mmeru na Mchaga?

Ee Bana Me Baba kaniambia nisioe Mchaga Toka nimemaliza form six 2008, Hata Juzi alipofika mama yangu mzazi kaja na ujumbe uleule Baba yako kasema usioe mchaga.
Basi tena. Wazazi wana maono
 
Kama wazazi wanakupangia wazalishe wote alafu ukiona kesi waoe wote ila dem wa kichaga kwa karne hii ni (lulu) +dili yaani hakunaga dem mchaga ----
 
Kama wazazi wanakupangia wazalishe wote alafu ukiona kesi waoe wote ila dem wa kichaga kwa karne hii ni (lulu) +dili yaani hakunaga dem mchaga ----

Mh!!! Umezicheki post zao humu? Nina maana hakunaga!!
 
Kama wewe ni mvivu,hauna haraka ya maisha,kichwani hako poa na unaishi bila mipango,kweli usioe mchaga
 
Wachaga si wabaya hivyo ila wako serious na maisha unakuta kuliko hata hao waume zao,ni watafutaji mno, ila tatizo linakuja kwa wazamiaji kwenye familia za watu wanotaka kuzeekea kwa watu, kupewa mitaji kwa watu, kushindia kwa watu,kupikiwa kwa watu eti ni mashemeji mara mawifi mlikuwa wapi saa watu wanatafuta kwa bidii mnakuja kuelemea familia ndio hao wanojifanya kusema ohh sikuhizi hatuendi kwa kaka kisa kaoa mchanga kalisheni masaburu majumbani kwenu
 
Waheshimu baba yako na mama yako ili upate miaka mingi ya kuishi....Katika Mithali zake mfalme Suleimani kuna shm anasema mwanangu sikiliza wosia wangu....achana na hao wachaga na pia jaribu sana kusikiliza wosia wa wazazi wako, mara nyingi wazazi uwa hawakosei. Mi nilikatazwa kuoa mchaga nikajifanya kichwa ngumu, huo u-boy friend na U-girl friend tu ulitaka kunitoa roho....sa izi nimetulia na mke wangu toka kanda ya ziwa...yaani nusu mtu, nusu malaika...asante Mungu kwa kunipa mwanamke huyu.
 
Mbona sisi wachaga wazazi wetu hawatushauri kabila la kuoa? Mi nna kaka yangu anaoa mluguru na wazee wanampa support, mimi pia ntaoa muhuya na wazee wamesema Sawa... Nyinyi makabila mengine kuoa lazima mchahuliwe kabila. Duuuh kwa akili hizo ni dhahir CCM itaendelea kubaki madarakani maana watu wengi bado ni primitives.

We speak and want democracy but in reality our lives doesn't exercise democracy. Sasa hata kuoa tu bado kuna udictetor hivi tupo tayar kwa mabadiliko?
 
Habari,

Nina mchumba wangu ambaye nimepanga kwenda kujitambulisha kwao mwezi huu August lakini kwa sasa niko kwenye hali ngumu kwa kuwa wazee wangu wa huku Meru hawataki nioe Mchaga na wanasema ni bora ningeoa Mmeru kuliko Uchagani wakitoa sababu tofauti tofauti.

Mchumba wangu huyu ni mchanganyiko wa Mkibosho(mama) na Mmachame(baba) ingawa nilishakuwa na uhusiano na binti wa Kimeru na ndio wamekazia hapo?

Nifanyeje? Hivi ingawa ni tabia ya mtu binafsi lakini nani zaidi kati ya Mmeru na Mchaga?

Ushauri wa wazazi usiupuuzie, usikilize, ila mwisho wa siku kumbuka mke ni wako, so maamuzi ufanye mwenyewe. Ili chochote kitakachotekea mbeleni, iwe huzuni au furaha, iwe ni juu yako. Inaumiza saana ilitokea shida afu uanze kujilaumu kwa nini uliwasikiliza wazazi, kumbuka wao teyari wana maisha yao, haya ni yako. Na pia inaweza kukusumbua usipowasikiliza wazazi afu kikatokea kitu kibaya.

So, ushauri wangu, as a man sikiliza ushauri, ila mwish wa siku inakubidi uweke msimamo wako, na uusimamie huo huo no matter what happens.
 
mimi nakushauri umuoe huyo manka...huyo ni mtaji wa mawazo anayekutaka urudi om na hela
 
Zifuatazo ni baadhi ya vigezo vya kuoa mchaga..#1 .Uwe na kazi/biashara ya uhakika.#2 .Uwe na malengo kimaisha ambayo yanatekelezeka
#3 .Uwe na upendo wa kweli.
#4 .Uwe tayari kwenda Moshi kila mwisho wa mwaka.
#5 .Uwe na wivu wa maendeleo
#6 .Uwe msikivu kwa mkeo anapokushauri ni lazima ukubaliane nae kwa zaidi ya 80%..n.k
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom