Binafsi niliwafahamu watanzania katika umri mdogo sana,o' level kulikua na tatizo la upungufu wa chakula(halafu ni private) lakini kwenye kuwasilisha malalamiko wengi walikua ni waoga,baada ya kusota sana kamgomo baridi kalinyoosha mambo haraka sana.
A' level tena kiumeni tulikokotwa sana kama watoto wadogo hadi kwenye mambo yaliyodhahiri, wakati wa mitihani ya pre national lilitoka katazo la kutokutoka chumba cha mtihani kabla ya msimamizi.
Hili katazo lilikiukwa na baadhi yetu hivyo waalimu wakajipanga kutupiga bakora ,sitasahau vijana waligombania kuchapwa wawahi pepa 😀(ilikuja kutokea comeback moja vijana wakaleta noma na ombi lao ni kuzungumza na mkuu ,inshort yule mzee ni msabato safi sana ila ilibidi aivunje siku hiyo)
NB:nimejifunza watanzania ni wabinafsi mno imagine hata waliokosa miili ya ndugu zao wameshindwa hata kuhoji wenye mamlaka kwa njia rafiki, hivyo kila mmoja ashinde mechi zake hakuna kujitoa kwa ajili ya wengine.