Watumishi 3 wasimamishwa kazi kwa kusababisha Kifo cha Mjamzito kisa hajatoa Tsh. 150,000

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
1699950330121.png
Nimepokea kwa masikitiko makubwa habari za kifo cha mjamzito na kichanga chake, kilichotokea Wilaya ya Handeni Tanga tarehe 11/11/2023 katika kituo cha Afya Kabuku kwa kinachoelezwa kuwa ni uzembe wa watumishi wa kituo hicho.

Pia soma > Tanga: Mjamzito afariki kwa kukosa Tsh. 150,000

Tayari Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe Waziri Kindamba ametuma Timu kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa inayojumuisha Madaktari bingwa wawili - Daktari Bingwa wa Wanawake na Uzazi na Daktari Bingwa wa Huduma za Usingizi - ili kufanya uchunguzi wa tukio hili.

Pili, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni tayari amewasimamisha kazi watumishi watatu (3) walioshiriki kumpatia huduma mama huyo tangu alipopokelewa kituoni hadi umauti ulipomkuta ili kupisha uchunguzi wa tukio hili baya na lisilopaswa kuvumiliwa!

Tatu, Tuhuma hizi pia tayari zimeshapokelewa na Mabaraza ya kitaaluma (Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT) na Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania (TNMC)) na vyombo vingine vya dola kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Hivyo, ninaelekeza Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT) na Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania (TNMC) ndani ya Siku 7 kuanzia leo kuniletea Taarifa ya Uchunguzi wa tukio hili na mapendekezo ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa.

Nne, nataka niwahakikishie umma wa watanzania kuwa baada ya kupokea taarifa ya Uchunguzi, kila mtumishi aliyehusika atachukuliwa hatua kali za kitaaluma, kiutumishi na kijinai ikiwemo kufikishwa Mahakamani kujibu tuhuma za kijinai pale itakapothibitika hivyo.

Nichukue fursa hii kuwakumbusha watumishi wa Afya kote nchini wafanye kazi kwa kuzingatia maadili ya taaluma zao na sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Nawapa pole familia iliyoguswa na msiba huu na niahidi kuwa serikali itaendelea kusimamia ubora wa huduma za afya ili kufikia matarajio ya wananchi.
 
Je, familia ya marehemu wanaweza kufungua docket ya kumshitaki waziri wa Afya kwa tukio hili ambalo serikali imeshakiri kuwa kulikua na uzembe?,yaani nikiifikiria nchi yangu hii na watanzania hawa,nakata tamaa kabisa, royal families hawapati haya kwa sababu wao ni india, UK, Canada au Netcare Millpark,ndiko wanakotibiwa
 
Nimepokea kwa masikitiko makubwa habari za kifo cha mjamzito na kichanga chake, kilichotokea Wilaya ya Handeni Tanga tarehe 11/11/2023 katika kituo cha Afya Kabuku kwa kinachoelezwa kuwa ni uzembe wa watumishi wa kituo hicho.
Stop that nonsense, huduma siyo bure, hawa siyo wapuuzi kumtoza 150,000. Kuweni wakweli
 
Huko na huko wanakomaa kununua magari ya milioni 450 kwa wanaowaita viongozi, yaani nchi ngumu sana hii, sasa kama hapo kabuku peupe kabisa hapo tena barabarani mtu anakufa kwa kukosa huduma tena ya laki na nusu, je huko pembezoni kabisa inakuaje? nasisitiza nchi ngumu sana hii, ngumu mnoooo, ila mlichagua wenyewe pambaneni.
 
Katika kichwa cha habari sh 150,000 zilikuwa zinadaiwa; Lakini kwenye maelezo yanayofuata inadaiwa huduma ni bure - labda huko mbele tutajua ukweli ni nini.

Vyovote iwavyo - mfumo wa bima za afya kwa wote ni muhimu mno - kwa vile kiuhalisia ni wengi tu wasiotangazwa wanaathitika kwa kushindwa kumudu gharama za matibabu.

Marehemu wapumnzike kwa Amani.
 
Stop that nonsense, huduma siyo bure, hawa siyo wapuuzi kumtoza 150,000. Kuweni wakweli
Sio Bure but alitakiwa apatiwe Huduma then aandikiwe deni siku ya kutoka atoe ndo atolewe. Kuna jirani yangu mmoja mkewe kajifungua mpaka sasa kazuiliwa hosp kisa hela Hana. Mmewe ni jobless ni kibaka. Hata vifaa vya kujifungulia majirani ndo wameungaunga. Kazuiliwa but kikubwa keshajifungua
 
Et kibaka we jamaa umejuaje?
Anadaiwa shingap?
Sio Bure but alitakiwa apatiwe Huduma then aandikiwe deni siku ya kutoka atoe ndo atolewe. Kuna jirani yangu mmoja mkewe kajifungua mpaka sasa kazuiliwa hosp kisa hela Hana. Mmewe ni jobless ni kibaka. Hata vifaa vya kujifungulia majirani ndo wameungaunga. Kazuiliwa but kikubwa keshajifungua
 
Hii nchi bhana!! Kila sehemu ni siasa tu. Wanasema wajawazito, watoto wachanga na wazee wanatibiwa bure! Na wakati ukienda kwenye hizo hospitali zao, mambo ni tofauti kabisa.

Kwa mfano hao mama wajawazito, kula kitu cha kujifungulia wanajigharamia wenyewe! Sasa hizo huduma bure wanazohubiri ni zipi!!!
 
Sio Bure but alitakiwa apatiwe Huduma then aandikiwe deni siku ya kutoka atoe ndo atolewe. Kuna jirani yangu mmoja mkewe kajifungua mpaka sasa kazuiliwa hosp kisa hela Hana. Mmewe ni jobless ni kibaka. Hata vifaa vya kujifungulia majirani ndo wameungaunga. Kazuiliwa but kikubwa keshajifungua
Kibaka muda wa kupiga pumbu anaupata wapi??na hivi Hospital wakikushikilia huwezi kutoroka??naomba siku waje wamshikilie mgonjwa wangu au mimi mwenyewe nitakachowanya hawataamini!!!kwa mfano kwa hiyo isu ningekuwa mimi ndio Mume wa huyo Mama kichanga ningewaita hao Manesi waliomshikilia Mke wangu na ningewaambia mimi Pesa ya kuwapa sina,mimi na Mke wangu tunaondoka tunawachia mtoto mumlee wenyewe,simple tu
 
Tuwe wakweli, huduma siyo bure kwa hao wamama. Utaambiwa vifaa vya operation vimeisha,mnapaswa mkanunue. Huko dukani mtalipia mawe?
 
Back
Top Bottom