Adrian Stepp
JF-Expert Member
- Jul 1, 2011
- 2,764
- 2,581
Katika kesi hii inasemekana kulikuwa na kihoja cha aina yake; Inabidi mfumo wetu wa sheria uangalie upya suala zima la kuwatumia wazee wa baraza kama hawa, ambao hali zao tu zinaonyesha wako katika mazingira rahisi mno ya kuhongwa na kupindisha ukweli.
Na ikiwa hakimu mwishowe hazingatii ushauri wao, kuna haja gani ya kuwa na wazee wa baraza?

Jana katika mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam wazee wa baraza katika kesi ya Swetu Fundikira waliushangaza umma uliohudhuria kesi hiyo (nafikiri hata na ndugu wa washtakiwa hawakutegemea kile walichosikia) baada ya wote watatu kudai kuwa washtakiwa waachiwe huru kwa kuwa hakuna ushahidi kuwa wao walimuua Swetu Fundikira. Aliyetoa kali kabisa ni Mzee Raha Saidi aliyedai polisi wamewabambikia kesi washtakiwa ki ujanja ujanja. Mzee mwingine Ali Kampea alidai kifo cha marehemu ni ajali tu kwani alianguka ndipo akaumia kichwani na kupeleka kifo chake. Bibi Johari yeye alidai kuwa yeye haoni kama washtakiwa walikuwa na nia mbaya na hatimaye kumuua Swetu Fundikira bali washtakiwa ni watu wazuri na nia yao ilikuwa ni kumpeleka polisi tu na si vinginevyo hivyo yeye anaona hawana hatia.
Hawa lazima wawe kafu tu!