Msamaha wa raisi hawezi kutoa msamaha kwa makosa ya mauaji ,ujambazi wa kutumia silaha na kesi za uhujumu uchumi!sheria za nchi zinakataza!
katika kesi hii inasemekana kulikuwa na kihoja cha aina yake; inabidi mfumo wetu wa sheria uangalie upya suala zima la kuwatumia wazee wa baraza kama hawa, ambao hali zao tu zinaonyesha wako katika mazingira rahisi mno ya kuhongwa na kupindisha ukweli.
Na ikiwa hakimu mwishowe hazingatii ushauri wao, kuna haja gani ya kuwa na wazee wa baraza?

jana katika mahakama kuu kanda ya dar es salaam wazee wa baraza katika kesi ya swetu fundikira waliushangaza umma uliohudhuria kesi hiyo (nafikiri hata na ndugu wa washtakiwa hawakutegemea kile walichosikia) baada ya wote watatu kudai kuwa washtakiwa waachiwe huru kwa kuwa hakuna ushahidi kuwa wao walimuua swetu fundikira. Aliyetoa kali kabisa ni mzee raha saidi aliyedai polisi wamewabambikia kesi washtakiwa ki ujanja ujanja. Mzee mwingine ali kampea alidai kifo cha marehemu ni ajali tu kwani alianguka ndipo akaumia kichwani na kupeleka kifo chake. bibi johari yeye alidai kuwa yeye haoni kama washtakiwa walikuwa na nia mbaya na hatimaye kumuua swetu fundikira bali washtakiwa ni watu wazuri na nia yao ilikuwa ni kumpeleka polisi tu na si vinginevyo hivyo yeye anaona hawana hatia.
WATUHUMIWA katika mauaji ya Swetu Fundikira, MTM 1900 Sajenti Roda Robert (42) wa kikosi cha JKT - Mbweni na MT 75854 Koplo Ally Ngumbe (37) wa JWTZ-Kunduchi leo wamehukumiwa kifo baada ya kupatikana na hatia na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam. HABARI NA PICHA ZAIDI KUWAJIA HIVI PUNDE!
loooh imani yangu ni kwamba mahakama imetenda haki..
Uliwahi kujinasibu hapa kwamba umewahi kupewa makuzi ya kiislam kupitia madras! lakini kwa kushabikia upuuzi huu ninawasiwasi sana kama kweli malezi hayo yalikuwa na manufaa yoyote kwako zaidi ya kukufanya mtumwa wa ujinga na fitina/uzandiki!
mkuu maneno yako ya busara sana!
Uliwahi kujinasibu hapa kwamba umewahi kupewa makuzi ya kiislam kupitia madras! lakini kwa kushabikia upuuzi huu ninawasiwasi sana kama kweli malezi hayo yalikuwa na manufaa yoyote kwako zaidi ya kukufanya mtumwa wa ujinga na fitina/uzandiki!
Hivi vikongwe vinatakiwa mahakama ya kadhi sio hapaKatika kesi hii inasemekana kulikuwa na kihoja cha aina yake; Inabidi mfumo wetu wa sheria uangalie upya suala zima la kuwatumia wazee wa baraza kama hawa, ambao hali zao tu zinaonyesha wako katika mazingira rahisi mno ya kuhongwa na kupindisha ukweli.
Na ikiwa hakimu mwishowe hazingatii ushauri wao, kuna haja gani ya kuwa na wazee wa baraza?

Jana katika mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam wazee wa baraza katika kesi ya Swetu Fundikira waliushangaza umma uliohudhuria kesi hiyo (nafikiri hata na ndugu wa washtakiwa hawakutegemea kile walichosikia) baada ya wote watatu kudai kuwa washtakiwa waachiwe huru kwa kuwa hakuna ushahidi kuwa wao walimuua Swetu Fundikira. Aliyetoa kali kabisa ni Mzee Raha Saidi aliyedai polisi wamewabambikia kesi washtakiwa ki ujanja ujanja. Mzee mwingine Ali Kampea alidai kifo cha marehemu ni ajali tu kwani alianguka ndipo akaumia kichwani na kupeleka kifo chake. Bibi Johari yeye alidai kuwa yeye haoni kama washtakiwa walikuwa na nia mbaya na hatimaye kumuua Swetu Fundikira bali washtakiwa ni watu wazuri na nia yao ilikuwa ni kumpeleka polisi tu na si vinginevyo hivyo yeye anaona hawana hatia.
| ||
|