Kikwajuni One
JF-Expert Member
- Mar 18, 2013
- 13,142
- 6,947
Zina ni tendo la ndoa, wanaloanza kufanya watu wawili kwa siri,kabla kutambulika na mamlaka husika za kifamilia na kutolea baraka.Lakini ikiwa tendo,linafanyika baaada ya mamlaka husika za kifamilia kukutana na kukubaliana,hiyo haiitwi zinaa,na ndio ukaona katika dini zote duniani,ikiwemo uislamu,waliokwisha kuwa mume na mke,baada ya mamlaka za kifamilia,kukubaliana kama wahusika ni wanando,wanahesabika ni wanandoa.Ndio maana dini zote, kokote ulimwenguni wanandoa,wanaohama kutoka dini moja kuingia dini nyingine,wanahesabika ni wanandoa sio wazinifu.Nina uhakika hujawahi kusikia leo kanisani kuna ndoa ya waislamu,au wamasai au wazungu au...waliongia ukristo wanaozeshwa upya.Na kwenye uislamu ni hivyo,hujawahi kusikia wanandoa wakristo au...wanaozeshwa upya.Mkuu hebu ifike mahali nyeusi iitwe nyeusi na nyeupe vivyo hivyo! Lakini nilitahadharisha kabla jamani; tukianza kufukua makaburi ya "manabii na mitume" humu tusije onana wabaya au kwamba tunatusi dini za watu; maana kuna "mabomu" mengine ya mitume yakiwekwa hapa "mbingu na ardhi zitatikisika"; tahadhari hiyo.
Ok, labda mimi sijui maana ya neno zinaa! Kwa tafsiri rahisi, nijuavyo mimi, uzinifu au zinaa ni kwa alieoa/olewa kutembea nje ya ndoa. Naomba tukubaliane hapa kwanza au kama tafsiri yangu sio sahihi nifahamishe tafadhali.
Kwa hiyo uelewe ndoa,ni makubaliano ya jamii husika,wenye mamlaka na jamii,kujiwekea utaratibu ndoa ifungwe vipi.
Hapo kwa Nabii Ibrahimu,ingekuwa ni uzinifu,mke wake,asingejuwa kama mumewe,aenda fanya tendo la ndoa,lakini yeye mwenyewe mke ndio amemtaka mumewe,afanye hivyo,ni kwamba tayari mamlaka husika ya kijamii,imeshatoa idhini ya Ibrahimu kumuoa mjakazi wake,na kila,akiwemo mkewe wa kwanza,walifahamu kama Ibrahim,anamuoa mwanamke fulani.
Kwa hiyo ukisema kama uzazi wa Ibrahimu kupitia mwanamke huyu, ni wa zinaa,basi hapata bakia mtu yoyoye duniani hata mmoja,akiwemo wewe mwenyewe, kuwa ni uzao wa zinaa,kwasababu babu zako,walioana kabla ya kuingia ukristo, je waliona kivipi,na ikiwa walikuwa hawana dini.