Tetesi: Watu wanaodhaniwa Askari wa Polisi na Maafisa Msitu wawapiga Wananchi, kuchoma moto makazi na mazao Wilaya ya Chemba na Ikungi

Midimay

JF-Expert Member
Apr 12, 2015
2,908
4,771
Habari za mchana wana JF.

Hali ya sintofahamu imeendelea kwa siku mbili sasa katika kijiji cha Handa kilichopo katika Wilaya ya Chemba mkoa wa Dodoma karibu na mpaka na Wilaya ya Ikungi ambayo ipo katika Mkoa wa Singida. Ni karibu pia na Mpaka na Wilaya ya Hanang katika mkoa wa Manyara.

Hali hiyo imesababishwa na watu wanaojitambulisha kama Askari wa Jeshi la Polisi na wengine wakijitambulisha kama Askari wa Misitu. Watu hao wamefika katika kijiji hicho siku ya tarehe 6/11/2023 na kuanza kuchoma moto makazi ya wananchi wanaoishi na kufanya shughuli zao za kilimo na ufugaji katika kijiji hicho.

Madai yao ni kwamba eti eneo walililopo halipo katika Wilaya ya Chemba bali lipo katika Wilaya ya Ikungi. Wananchi hao walipata ardhi hiyo baada ya kugawiwa na halmashauri ya kijiji.

Huu ni uonevu wa hali ya juu kwa wananchi ambao ni raia wa Tanzania wanaojishughulisha kiuchumi. Eneo kutokuwa katika Wilaya ya Chemba inawaohusu nini wananchi? Au Mkoa wa Singida ni Jamhuri inayojitegemea? Huo mkoa na Wilaya ina uraia wake tofauti na huu wa Tanzania? Na kama kuna mgogoro kati ya vijiji, kwanini usitatuliwe kwa misingi na sheria?

Kwanini wananchi wachomewe mali zao zikiwepo mazao yaliyohifadhiwa, makazi yao ya kujihifadhi, mavazi na malazi?

RPC mkoa wa Singida, OCD Ikungi, RPC Dodoma, OCD Chemba, RC Mkoa wa Singinda, RC Mkoa wa Dodoma, DC Wilaya ya Ikungi, DC Wilaya ya Chemba wanahitajika kwenda kuwaokoa hao wananchi kwa misingi ya sheria na kuwawajibisha wote waliojichukulia sheria mkononi kwa kuwachukulia hatua kali.

Wananchi wapewe fidia ya upotevu wa mali zao na kutibiwa kwa waliomizwa kwa vipigo kwa watenda jinai hao. Kama kuna mgogoro wa mipaka ya wilaya au vijiji utatuliwe haraka kwa misngi ya sheria.

DSC_0045.JPG


Mtanzania ana haki ya kwenda popote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupata hifadhi, kufanya kazi ya kujipatia kipato bila kuvunja sheria.

Uchunguzi pia ufanyike ili kujua kama kuna anayelitumia jeshi la polisi wilaya ya Ikungi kwa manufaa yake binafsi.

Haki itendeke kwa walioumizwa. Hadi leo watu hao wanaendelea kuteketeza makazi, malazi, mavazi, chakula na mifugo kwa moto kwa madai kwamba wamelivamia eneo hilo.

Kwanini wanajichukulia sheria mkononi? kwanini wananchi wanyonge, wakulima wadogo na wafugaji wanyanyaswe na watu wanaojiita jeshi la polisi?
Usalama wa Raia uko wapi kama watu walioaminiwa ndio wanaovunja sheria?

Naomba pia wabunge Mohammed Mmuni wa Chemba, Ramadhani Ighondu wa Singida Kaskazini, Miraji Mtaturu wa Ikungi Mashariki na Mbunge wa Hanang' Mhandisi Samwel Hhayuma wawasaidie wananchi hao wanyonge ili waweze kutendewa haki.

Majibu ya Serikali, soma hapa - Mamlaka ya Misitu (TFS) yatoa ufafanuzi kuhusu zoezi la kuwahamisha Waliovamia Msitu wa Mgori
 
Kataarifa kameletwa kidizaini kama wale wenzetu wakiwaga saluni. Kwa kweli sikatai wananchi kuonewa lakini sababu iliyoletwa na presenter huyu sio ya kuaminika
 
KIZIMKAZI sio MTU makini wanachezea tu Tanganyika yetu kisa YY atarudi znz
 
Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Kanda ya Kati, Mathew Kiondo anafafanua: "Kinachofanyika ni maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan kuondoa wavamizi waliopo katika Msitu wa Mgori.

“Rais alipokuwa akiwasili Singida katika ziara akasema wakati akiwa anawasili aliona msitu mzuri lakini unaharibiwa, kwa tamko hilo maana yake ni maelekezo ya Mkoa na Wilaya.
Hapa nipo 100% na mamlaka.
Hatuwezi kuwa nchi ya kufanya mambo shaghalabaghala tu.
Mtanzania ana haki ya kwenda popote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupata hifadhi, kufanya kazi ya kujipatia kipato bila kuvunja sheria.
Hapo kazia sana kwenye maneno "...BILA KUVUNJA SHERIA."

Makosa yanaanzia kwa viongozi huko chini kutokuwa makini wanapoona jambo linalofanyika halistahili kufanyika, na wao kukaa kimya juu yake.
Hawa ndio wanao stahili kuchukuliwa hatua.
 
Habari za mchana wana JF.

Hali ya sintofahamu imeendelea kwa siku mbili sasa katika kijiji cha Handa kilichopo katika Wilaya ya Chemba mkoa wa Dodoma karibu na mpaka na Wilaya ya Ikungi ambayo ipo katika Mkoa wa Singida. Ni karibu pia na Mpaka na Wilaya ya Hanang katika mkoa wa Manyara.

Hali hiyo imesababishwa na watu wanaojitambulisha kama Askari wa Jeshi la Polisi na wengine wakijitambulisha kama Askari wa Misitu. Watu hao wamefika katika kijiji hicho siku ya tarehe 6/11/2023 na kuanza kuchoma moto makazi ya wananchi wanaoishi na kufanya shughuli zao za kilimo na ufugaji katika kijiji hicho.

Madai yao ni kwamba eti eneo walililopo halipo katika Wilaya ya Chemba bali lipo katika Wilaya ya Ikungi. Wananchi hao walipata ardhi hiyo baada ya kugawiwa na halmashauri ya kijiji.

Huu ni uonevu wa hali ya juu kwa wananchi ambao ni raia wa Tanzania wanaojishughulisha kiuchumi. Eneo kutokuwa katika Wilaya ya Chemba inawaohusu nini wananchi? Au Mkoa wa Singida ni Jamhuri inayojitegemea? Huo mkoa na Wilaya ina uraia wake tofauti na huu wa Tanzania? Na kama kuna mgogoro kati ya vijiji, kwanini usitatuliwe kwa misingi na sheria?

Kwanini wananchi wachomewe mali zao zikiwepo mazao yaliyohifadhiwa, makazi yao ya kujihifadhi, mavazi na malazi?

RPC mkoa wa Singida, OCD Ikungi, RPC Dodoma, OCD Chemba, RC Mkoa wa Singinda, RC Mkoa wa Dodoma, DC Wilaya ya Ikungi, DC Wilaya ya Chemba wanahitajika kwenda kuwaokoa hao wananchi kwa misingi ya sheria na kuwawajibisha wote waliojichukulia sheria mkononi kwa kuwachukulia hatua kali.

Wananchi wapewe fidia ya upotevu wa mali zao na kutibiwa kwa waliomizwa kwa vipigo kwa watenda jinai hao. Kama kuna mgogoro wa mipaka ya wilaya au vijiji utatuliwe haraka kwa misngi ya sheria.

Mtanzania ana haki ya kwenda popote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupata hifadhi, kufanya kazi ya kujipatia kipato bila kuvunja sheria.

Uchunguzi pia ufanyike ili kujua kama kuna anayelitumia jeshi la polisi wilaya ya Ikungi kwa manufaa yake binafsi.

Haki itendeke kwa walioumizwa. Hadi leo watu hao wanaendelea kuteketeza makazi, malazi, mavazi, chakula na mifugo kwa moto kwa madai kwamba wamelivamia eneo hilo.

Kwanini wanajichukulia sheria mkononi? kwanini wananchi wanyonge, wakulima wadogo na wafugaji wanyanyaswe na watu wanaojiita jeshi la polisi?
Usalama wa Raia uko wapi kama watu walioaminiwa ndio wanaovunja sheria?

Naomba pia wabunge Mohammed Mmuni wa Chemba, Ramadhani Ighondu wa Singida Kaskazini, Miraji Mtaturu wa Ikungi Mashariki na Mbunge wa Hanang' Mhandisi Samwel Hhayuma wawasaidie wananchi hao wanyonge ili waweze kutendewa haki.

============


UFAFANUZI WA MAMLAKA YA MISITU

Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Kanda ya Kati, Mathew Kiondo anafafanua: "Kinachofanyika ni maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan kuondoa wavamizi waliopo katika Msitu wa Mgori.

“Rais alipokuwa akiwasili Singida katika ziara akasema wakati akiwa anawasili aliona msitu mzuri lakini unaharibiwa, kwa tamko hilo maana yake ni maelekezo ya Mkoa na Wilaya.

"Kamati ya Ulinzi na Usalama ikatoa tangazo watu wahame katika Hifadhi ya Msitu wa Mgori, siku ya kwenda kupeleka tangazo hilo Wananchi waliovamia msitu huo wakawashambulia watu wa usalama akiwemo Mkuu wa Wilaya kwa kutumia mishale, mawe, rungu na nyinginezo.

"Baada ya kujipanga tukarejea na kwenda kufanya zoezi la kuwaondoa wavamizi hao, hatukutumia nguvu, kwa kuwa wao waliona tumeongozana na Watu wa Usalama, Askari wa FFU, Mgambo hawakufanya fujo, zoezi ni endelevu na litafanyika kwa siku 14.

“Tulichofanya tuliharibu makazi yao ya muda ambayo yapo ndani ya Msitu, wanafanya hivyo kujenga makazi ya muda kwa kuwa wanajua sio sehemu sahihi kwao.

“Kilichoharibiwa ni makazi yao lakini mazao, chakula na mifugo vyote havijachukuliwa wamekabidhiwa na kutakiwa kurejea kwenye vijiji ambavyo vipo kando ya Misitu.

"Lazima tuwe na ubinaadamu, kisheria ilitakiwa hata mifugo yote tuitafishe lakini tuliwaachia waondoke nayo.

“Pamoja na hivyo zipo taarifa zisizo rasmi kuwa baadhi ya mifugo ambayo inaingizwa ndani ya Hifadhi ni ya watu wenye nafasi katika siasa, hivyo hawa Wananchi wanatumika tu.”
Wananchi wamepigwa, wameumizwa, mazao yamechomwa moto.
 
Kataarifa kameletwa kidizaini kama wale wenzetu wakiwaga saluni. Kwa kweli sikatai wananchi kuonewa lakini sababu iliyoletwa na presenter huyu sio ya kuaminika
Hujaona hata TFS kanda ya Kati wamekubali kutenda jinai hiyo?
 
Back
Top Bottom