Watoto wa vigogo na ajira BoT

Kwa hiyo ulitaka nani aajiliwe? Kama vipi soma kozi zinazohusiana na mambo ya BOT ili ukaombe ajira huko kama unaona wivu kwa kuajiriwakwa watoto wa vigogo huko.
Sioni wivu wala sina haja ya kuajiriwa huko. Nimeshangazwa na mawazo yako uliyotoa eti ''hata kama tungekuwa sisi tungefanya hivyo hivyo''. Mawazo yako yanapotosha na ni ya enzi za mawe. Huwezi kuhalalisha ''uki-gogonization'' eti kwa vile hata sisi tungefanya hivyo. Mazee nakuapia hata mwenyekiti wa kijiji chetu ambae hajasoma hawezi kutoa mawazo kama hayo. Yaani tuache wakuu wa idara za serikali wafanya wanavyotaka kwa kuwa eti hata kama tungekuwa sisi tungefanya hivyo?? La haula .... nimelewa bila kunywa kilevi. Na mtu mwenye mawazo kama haya unaweza kuta amemaliza chuo kikukuu!!!!!
 
Mkumbuke prof. Sarungi aliacha udakitari akawa mwanasiasa

This is Pumba of the Day

Siasa si mtu yeyote anaweza enda haitaji Professionalism. Yeyote sasa masuala ya finance na medical yanaingiliana??
Kweli??
Oh God ....
 
hivi ukiwa mtoto wa kigogo ndiyo huna haki ya kuajiriwa BKT??? Tufanye utafiti kwanza...tujue taasisi inawaajiriwa wangapi??? kati yao watoto wa "vigogo" ni wangapi??.....walipata ajira kihalali??na tujue pia "kigogo" ni nani?? sio tuna kuja na mada za kulalamika tu....tukiwatunalalamika tu mwishowe tutazoea kulalamika...
Hakuna mtu aliyesema ukiwa mtoto wa kigogo huna haki ya kuajiriwa BOT. Hiyo ni conclusion yako uliyofikia na inaonekana huelewi watu wanahoji nini). Sisi tunashangazwa na ''coincedence'' ya watoto 14 wote wa vigogo kuajiriwa sehemu moja (nyeti na yenye malipo nzuri). Mbona hatuioni ''coincidence'' hii ikitokea sehemu nyingine...!!!!!!!
 

Umeguswa nini Mkuu? Anyway ishu ni hapo kwenye red! Hao vijana wa wakubwa ukifuatilia hata academic records history wengi ni vilaza maana tumesoma nao na wengine tunawajua vichwani ni 'empty heard'. Mtu anapata Division IV Form six lakini kwa vile Baba yake anapesa anamrusha nje kusoma digrii. Within five years laiter unashangaa yumo ndani ya 'Twin Towers'.

Mfano?
 
Ona nchi yetu ilivyo
FILBART SUMAYE, PAMELA LOWASA, ZARIA KAWAWA,HERIETH LUMBANGA, SALAMA MWINYI,RECHAL MUGANDA, SALMA MAHITA,JUSTINA MUNGAI, KENETH NCHIMBI, BLASIA W. MKAPA, VAOLETH LUHANJO, LIKU KATE KAMBA, THOMAS MONGELA NA JABIRI KIGODA.
HIYO NI TIMU YA WATOTO WA VIGOGO WALIOAJIRIWA BOT BADO KATIKA BALOZI ZETU NJE YA NCHI.NCHI YETU INAFISADIWA NANI WA KUTUOKOA WENGI WAO WAMEGHUSHI ELIMU ZAO
HII MESEJI IMEZAGAA MITAANI KWA SANA SASA SIJUI KWAMBA NI KUJIVUNIA VIONGOZI WETU KUTUONYESHA KUWA ELIMU NI MSINGI WA MAISHA KWA KUWAPA WATOTO WAO ELIMU BORA AU
NI WANANCHI KUONA HUKO NI KUPENDELEANA KATIKA AJIRA ZENYE MASLAHI MAZURI AU
NI WIVU WA WATANZANIA TU?
jmsekwa.jpg


Jackob P. Msekwa

Minister Counsellor
Tanzania Embassy in Nordic and Baltic Countries



Ms. Lily Munanka - Minister Plenipotentiary/Head Of Chancery. - DC

Ms. Mindi Kasiga Minister Counselor-Information, Education Communication & Tourism - DC


Samuel Shelukindo - Tanzania Embassy BUJUMBURA, BURUNDI



 
Lingekuwa ni jambo la busara endapo ungeletwa uchambuzi wa sifa zao hawa wenzetu kiasi cha kuweza kuajiriwa hapo BOT na sio vijana wengine wenye sifa pengine kama za kwao ambao hawakuweza kuajiriwa mahala hapo.

Kwa mfano Filbert Sumaye ionyeshwe kabla ya kwenda UK kusomea Degree yake ya computer science alisoma wapi kabla ya hapo hadi kuwa na sifa za kwenda UK university na kulipa maelfu ya paundi za uingereza, ana baada ya hapo awe na uhakika kwamba akirudi Tanzania anaingia BOT moja kwa moja bila kuchakarika kidogo.

Kwahio anaefahamu au mwenye details za uhakika huu ndio wakati wa kusema.

Pia BOT walitumia utaratibu gani wa kufanya usaili kiasi kwamba watoto 14 wa viongozi mbalimbali wa serikali ya CCM wamepata nafasi za kazi katika idara hiyo nyeti, huku vijana wengine wakitupwa nje.
 
Ninacho jiuliza na sipati majibu mpaka sasa ni hiki, kama imetokea coincidence BOT ikaajiri watoto 14 wa vigogo je, coincidence hiyohiyo inaweza kutokea kwenye wizara ya elimu watoto wenye majina kama hayohayo wakapangwa kwenda kufundisha shule za kata vijijini ambako hakuna maji wala umeme na wakaendelea kuifanya kazi hiyo kwa moyo wa kizalendo bila kujalisha kuwa mishahara imechelewa na hawaja pandishwa vyeo na wakati huohuo wakiidai serikali sikivu malikimbizo?!

Hivi kweli binadamu wote ni sawa kwa maana ya fursa za ajira bila kuangaliana usoni?! Hasa BOT?
 
Kama Waliqualify sawa ...kama walingia Kwa Memo ...that's Problem

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Hawa ni watoto wao. Na hawala wao wapo na ndugu na wajomba. Hoja ya kusoma nini haijitoshelezi wakuu. Kwani hizi kozi kam B.Com na zingine wamesoma watoto wa vigogo tu. Me nilikimbilia sayansi siku moja mtaniona ni Director Recovery BOTmaana baba amepata nec-taifa. Mnakazi watz............
 
ukweli hata iweje wewe umesoma shule za walimu 2 kingereza cha kubahatisha, leo hii ukafanye competition na watoto hawa watakushinda maana wao hawajasoma shule hizi za walimu njaa na wachache wenye uhaba wa vyoo, vitabu, hata nyumba za kuishi. mwalimu akiamka anawaza familia yake watakula nini lakini hawa wezetu wamesoma shule nzuri pengine nje ya nchi kwa system zote za shule

shida ndo inaanzia hapa,
kwa kweli watoto wa vigogo wanapatiwa elim bora, hata tunapoenda kwenye ushindan kwenye intavyu, sie tunatumia kiingereza cha shule za kata, wao wanatumia cha inglish midia, na kwa haraka haraka wanaonekana wanajua kujenga hoja, kiasi kwamba hata wale panelisti wanawehuka na kuona wanafaa.

wamesoma kwenye vyuo vizuri na vyenye sifa kimataifa, koz wazazi (vigogo) wanajiweza kumudu gharama.
 
Huko ni BOT, hebu wenye taarifa za NEC CCM, nimesikia imekuwa Baba Mama na watoto.
 
Ona nchi yetu ilivyo
FILBART SUMAYE, PAMELA LOWASA, ZARIA KAWAWA,HERIETH LUMBANGA, SALAMA MWINYI,RECHAL MUGANDA, SALMA MAHITA,JUSTINA MUNGAI, KENETH NCHIMBI, BLASIA W. MKAPA, VAOLETH LUHANJO, LIKU KATE KAMBA, THOMAS MONGELA NA JABIRI KIGODA.
HIYO NI TIMU YA WATOTO WA VIGOGO WALIOAJIRIWA BOT BADO KATIKA BALOZI ZETU NJE YA NCHI.NCHI YETU INAFISADIWA NANI WA KUTUOKOA WENGI WAO WAMEGHUSHI ELIMU ZAO
HII MESEJI IMEZAGAA MITAANI KWA SANA SASA SIJUI KWAMBA NI KUJIVUNIA VIONGOZI WETU KUTUONYESHA KUWA ELIMU NI MSINGI WA MAISHA KWA KUWAPA WATOTO WAO ELIMU BORA AU
NI WANANCHI KUONA HUKO NI KUPENDELEANA KATIKA AJIRA ZENYE MASLAHI MAZURI AU
NI WIVU WA WATANZANIA TU?

System inatengenezwa kuanzia mbali sana, hao watoto wanapewa scholarship au kusomeshwa in some of the best schools in the world. They use the opportunity and once hiring starts wanakuwa na upper age compared to the rest of us. Try to look deeper, very few wanhold degree za hapa kwetu!!
 
Mkuu, inawezekana na wala hakuna muujiza. Usikate tamaa. BoT na TRA ni moja ya Taasisi zinazosemekana kuwanyima fursa watanzania wa kawaida na kuajiri watoto wa vigogo. Hili si kweli, na kama wapo ni asilimia chache tu. Lakini pia tusisahau hata watoto wa vigogo wamesoma, na kama wana sifa zinazotakiwa kwanini wasiajiriwe? Mbona mimi ni mtoto wa mlalahoi asiyejulikana lakini nimebahatika kufanya kazi kwenye Taasisi zote hizi? Haya ni majungu tu. Kwani hao aliowataja ni asilimia ngapi ya wafanyakazi wote wa BoT?

Tuambie mkuu mara ya mwisho kabisa kufanya kazi kwenye taasisi hizo ilikuwa ni lini?
 
Tangu nikiwa mdogo nimekuwa na ndoto kuja kuwa mfanyakazi wa BOT sikati tamaa! Najua iko siku milango ya watoto wa wakesha hoi itakuwa wazi japo hata kwa kumuokotea gavana kalamu zikidondoka!inshaallah

mkuu maneno mazito sana haya.inauma lakini.
 
Tuambie mkuu mara ya mwisho kabisa kufanya kazi kwenye taasisi hizo ilikuwa ni lini?

TRA nilitoka 2010 nikajiunga na BoT. Unadhani ni long sana kamaunavyotaka kuaminisha watu hapa? Sema tu watu wakiitwa kwenye interviewswakapiga zile Aptitude Tests na kuchemsha wanaanza mbwembwe, mara "ooh, paleBoT/TRA huwezi kupata kama wewe siyo mtotowa kigogo au labda una ki-memo kutoka kwa kigogo". Aaaah wapi?! Mi sikuwa naki-memo na wala simjui mtu yeyote. Mi ni mtoto wa mkulima wa kawaida kabisa.Ndio maana nikamuuliza mleta uzi, hao anaowasema ni asilimia ngapi ya wafanyakaziwote wa Benki Kuu? Au mnadhani hao mliowataja ndio watoto pekee wa vigogo wotemnaowajua nchi hii? Porojo zingine zinafaa kupelekwa kwenye vijiwe vya kahawana wala siyo hapa kwa Great Thinkers!
 
Lingekuwa ni jambo la busara endapo ungeletwa uchambuzi wa sifa zao hawa wenzetu kiasi cha kuweza kuajiriwa hapo BOT na sio vijana wengine wenye sifa pengine kama za kwao ambao hawakuweza kuajiriwa mahala hapo.

Kwa mfano Filbert Sumaye ionyeshwe kabla ya kwenda UK kusomea Degree yake ya computer science alisoma wapi kabla ya hapo hadi kuwa na sifa za kwenda UK university na kulipa maelfu ya paundi za uingereza, ana baada ya hapo awe na uhakika kwamba akirudi Tanzania anaingia BOT moja kwa moja bila kuchakarika kidogo.

Kwahio anaefahamu au mwenye details za uhakika huu ndio wakati wa kusema.

Pia BOT walitumia utaratibu gani wa kufanya usaili kiasi kwamba watoto 14 wa viongozi mbalimbali wa serikali ya CCM wamepata nafasi za kazi katika idara hiyo nyeti, huku vijana wengine wakitupwa nje.

Wewe unafanya kazi wapi ?
Toa detail zako za elimu uoneshe umefikaje hapo ulipo?
Sio kuomba details za watu tu watanzania bwana
 
Back
Top Bottom