Watoto wa vigogo na ajira BoT

Watoto wa vigogo na ajira BoT

Kumbe mpaka usome Ulaya au America ndo upate ajira kwenye EPA?

sio lazima ila watu wengi wanaotoka vyuo vya nje kama ulaya na america upstairs wanakuwa wana vitu kuliko sie tunaodesa ifm , na ud
naongelea kwa experience nimeshakutana na wafanyakazi kibao ambao wametoka nje (vyuo vya maana) ni tofauti na wafanyakazi waliosoma hizi shule zetu hasa wale wa degree za pichu

mfano mzurri chukua mtu aliyesoma mtu aliyesoma Harvard business school na mtu aliyesoma Cbe au Ifm au mtu aliyesoma MIT ( massachusetts institute of technology ) na watu waliosoma learn IT angalia tofauti zao kama hujakutana nao tafuta mie nimeshakutana nao naongea kitu ninachikijua

tusiongelee kiushabiki kisa umekosa kazi Bot ila ongea kwa facts mkuu na huo ndio u GT
 
Haha Pole sana usilolijua ni usiku wa Giza.

Wengi wameingia hapo na Elimu ya Form 4, Na wakiwa hapo wakapata course za nje na kuungaunga kusoma nje ndio maana leo ukiwakagua unaweza kukuta wengine wana zile Degree na Masterz za kina nchimbi(Feki).

Refer viky kamata alisoma Masterz 2008 akiwa BOT ambapo aliajiriwa akiwa na Certificate na sasa ana masterz na aijulikani alisoma DegrEe wapi.
www.jamiiforums.com/jukwaa-la-elimu-education-forum/290803-mh-vicky-kamata-cv-[-mungu-tuokoe].html


mkuu mbona umetoa mfano wa vicky kamata toa mfano wa watoto wa vigogo wenye strong financial background ya family vicky kamata yule mtoto wa mkulima na kwa yeye sipingi lolote kwakwe
mie nawatetea watotowa wakubwa watoto wa vigogo hapa
 
Nae mtoto wa Mkuu wa Fedha ametoka juzi juzi huko UK,baada ya baba kupew madarakasasa yuko Benki hapa Bongo,rafiki yangu anafanye nae kazi,sikilizia kidogo tu atapewa cheo cha ajabu
 
Aisee mmenikatisha tamaa sana, ngoja ni some ka electrical engineering nikavute nyaya kwenye magorofa au nikaanzishe kakampuni kangu ya kuweka wayaring kwenye resident.
 
Mimi mpaka leo najiuliza Mbowe aliwezaje kupata kazi BOT pamoja na kuwa hajasoma. Je na yeye alichomekwa huko na Mtei?
 
Umbea mbaya sana hasa ukiwa unafanywa na wanaume!
 
Sio BOT tu,hata taasisi kama balozi Ulaya
1.Angalia Offisi yetu UN huko State kuna majina common
a.Rose Mkapa -Admin Attache
b.Tully Malecela Mwaipopo-Secondary Secretary

2.Sweden
a.Jacob Msekwa-Minister Councellor

Ndio maana wanatumia resources zao nyingi ku make sure wanabaki madarakani ili wajukuu zao pia washike hatamu
 
Benk hii imekuwa sio ya watoto wa wakulima.Lazima huwa mtoto wa kigogo.

Iweje watoto wa:

3 former Prime Ministers-Kawawa,Lowassa na Sumaye wawe pale?
2 former Presidents -Mkapa ,Mwinyi?

Buku7 watasema eti walisoma shule nzuri???Oxford,Havard?
 
Benk hii imekuwa sio ya watoto wa wakulima.Lazima huwa mtoto wa kigogo.

Iweje watoto wa:

3 former Prime Ministers-Kawawa,Lowassa na Sumaye wawe pale?
2 former Presidents -Mkapa ,Mwinyi?

Buku7 watasema eti walisoma shule nzuri???Oxford,Havard?
Ndugu yangu siku zote anayefanyia kazi hotelini analia hotelini. wewe angalia utakataje huo mduala wa umasikini na sio kuangalia watoto wa mawaziri wanafanyaje. ushawahi kuona tangazo la ajira BOT??
 
Mimi siyo miongoni mwa buku 7 ila ninauliza hao watoto wana kosa gani kuwa hapo kama wanakidhi viwango? Hapo tutakuwa tunawaonea hao watoto.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Ratio ya hao watoto wa vigogo na maskini ni kiasi gani BOT??.Ndugu yangu uchwara, BOT ya sasa si kama ya zamani, siku hizi pale ni sehemu ya kawaida tu, hakuna maisha kama ya zamani, kwa hiyo usihofu sana.
 
Back
Top Bottom