Watanzania Wengi ni Wavivu – Kauli ya Mtume Boniphace Mwamposa na Rais Mstaafu Mkapa Zinagusa Ukweli Mchungu?

Watanzania Wengi ni Wavivu – Kauli ya Mtume Boniphace Mwamposa na Rais Mstaafu Mkapa Zinagusa Ukweli Mchungu?

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,990
Reaction score
12,019
  • Mtume Boniphace Mwamposa ametamka: “Watanzania wengi ni wavivu ” Watu wakakasirika, wengine wakabaki kimya. Lakini hii si mara ya kwanza kauli hii kusemwa na mtu maarufu kama Mtume Mwamposa.

  • Mwaka 2011, Rais mstaafu Benjamin Mkapa aliwahi kusema waziwazi kuwa “Watanzania tumejaa visingizio, tunapenda kuwalaumu wengine na hatutaki kufanya kazi kwa bidii.” Alisema haya kwa uchungu, akisisitiza kwamba uvivu ni kikwazo kikuu kwa maendeleo yetu Watanzania wengi wavivu wa kufikiri-Mkapa

  • Hii ina maana moja tu: kwa zaidi ya muongo mmoja sasa, viongozi wetu wamekuwa wakituamsha kutoka usingizi wa uvivu – lakini bado tunasuasua. Tumezoea starehe kuliko jasho, lawama kuliko suluhisho.
  • Hapa majuzi kila mtu anamlaumu Mchina kwamba kajaa Kariakoo amekuja hadi mikoani. Mchina huyohuyo amejaa kila eneo na anafanya "retail" business. Nani alaumiwe? Mchina, mzawa mvivu, au serikali?>

  • Tuna ndoto za maisha bora, lakini hatuko tayari kulala saa 5 na kuamka saa 11 kufanya kazi. Tunataka magari na majumba, lakini hatuwezi kusimamia muda wetu wala kujifunza kwa bidii (matokeo yake hadithi zetu nyingi ni kuwahusu wenye mali nyingi na wenye magari ya kifahari-hao nao tunawaita wana utajiri wa manyoka - hatuamini katika bidii na maarifa kama chanzo cha ukwasi-TUNA SHIDA KUBWA).

  • Uvivu wetu uko kila mahali: kwenye vijiwe, ofisini, mashambani, na hata kwenye ndoto zetu. Tunatamani tusifanye chochote lakini tupate kila kitu. Hii ni ndoto isiyo na mwisho (Nililima kwenye moja ya vijiji vya Tukuyu wenyeji wanataka ujira mkubwa walipwe kwa pay-day na kazi wanafanya kisoda - ikabidi niwe naenda Ileje kuwaleta Wandali wafanye kazi hapo shambani au niende Ntokela kuleta Wasafwa waje kufanya kazi hapo shamba - Tuna shida KUBWA).

  • Kila siku tunakutana na vijana wenye nguvu, elimu na muda — lakini wanaishia mitaani wakisubiri miujiza. Hawajafungua biashara, hawajajitolea, hawajifunzi ujuzi wowote. Wanangoja “koneckshen” ni watu wa kulaumu na matusi, hawana nidhamu yao binafsi wala ya kazi, hawaajiriki-ukiwaajiri lazima wakuibie sana.

  • Si vijana tu – hata taasisi zetu baadhi zimelemaa. Uamuzi mdogo unachukua miezi. Miradi mikubwa inacheleweshwa kwa sababu ya uvivu wa kiutendaji na kukosa uwajibikaji.

  • Tumejifunza kuishi kwa “polepole,” tukikumbatia uzembe kama sehemu ya utamaduni. Lakini dunia haikusubiri – mataifa mengine yanapiga hatua kwa bidii na nidhamu.

  • Kauli ya Mwamposa na ile ya Rais Mkapa zinafanana kwa ujumbe mmoja: Uvivu ni adui wa maendeleo. Na Watanzania wengi, tusipobadilika, tutajikuta tukibaki nyuma zaidi.

  • Kwa hiyo leo, si lawama bali ni wito: Amka. Jitume. Tenda. Tuanze na sisi binafsi. Tufanye kazi kwa bidii, tuthubutu, tuache kusingizia serikali kila siku. Mabadiliko hayawezi kuja kama hatutayachochea wenyewe.
  • Tunazo rasilimali nyingi sana zinazoweza kutukomboa. TUAMKE; TUBADILIKE.

NB: Soma kimyakimya, toa comment, matusi kwenye huu uzi pendwa hayaruhusiwi. Nyadikwa huwa ha tolerate ujinga.

Wahega
 
Unakuta mazee na mavijana yanacheza bao na pool mchana unajiuliza hawa wanafanya kazi wakati gani? Badala ya mtu kuwepo kwenye shughuli zake wakati wa kazi yeye yupo vijiweni anacheza bao, drafti, pool na upuuzi mwingine kama wa vijiwe vya kahawa wakati wa kazi. Kwa hali hii umasikini utatoka kweli? Wazee wa mashambani wanapaswa kushindia mashambani mwao na wengine hivyo hivyo wawepo kwenye shughuli zao. Pumzika inapobidi lakini usikimbie kazi
 
Unakuta mazee na mavijana yanacheza bao na pool mchana unajiuliza hawa wanafanya kazi wakati gani? Badala ya mtu kuwepo kwenye shughuli zake wakati wa kazi yeye yupo vijiweni anacheza bao, drafti, pool na upuuzi mwingine kama wa vijiwe vya kahawa wakati wa kazi. Kwa hali hii umasikini utatoka kweli? Wazee wa mashambani wanapaswa kushindia mashambani mwao na wengine hivyo hivyo wawepo kwenye shughuli zao. Pumzika inapobidi lakini usikimbie kazi
Kuna wakati huwa nawaza sijui zitungwe sheria za kufanya kazi kwa lazima. Ukikutwa haupo kazini na ni mzima upelekwe ukalime mashamba makubwa sana jela
 
MWAMPOSA ANACHOKITAFUTA ATAKIPATA, WABONGO HAWACHELEWESHI, MASTER J ALIWASHA MOTO TUKAAMBIWA ANALIWA TIGO
 
MWAMPOSA ANACHOKITAFUTA ATAKIPATA, WABONGO HAWACHELEWESHI, MASTER J ALIWASHA MOTO TUKAAMBIWA ANALIWA TIGO
Ndiyo mambo wabongo wanaweza. Kumkaanga mtu anaewaambia ukweli.

Kupinga ukweli huu ni sawa na kupiga kwenzi ncha ya kisu.

Wabongo wengi hasa kizazi hiki cha GenZ ni wavivu sana. Hawataki kazi wanapenda dezo wanataka kulelewa, walalamishi, ukiwapa kazi hata iwe nzuri vipi lazima wakutie loss mwajiri, rejea vijana wa bodaboda, bolt na bajaj majority wasivyo waaminifu kwa maboss zao. Shuhuda zimo humu jf.
 
Ndiyo mambo wabongo wanaweza. Kupinga ukweli huu ni sawa na kupiga kwenzi ncha ya kisu. Wabongoland hasa vijana wengi ni wavivu sana na visingizio tele
Hap wavivu na akili ndogo ndio mtaji wake huyo mwamposa
 
MWAMPOSA ANACHOKITAFUTA ATAKIPATA, WABONGO HAWACHELEWESHI, MASTER J ALIWASHA MOTO TUKAAMBIWA ANALIWA TIGO
Kwanza ye mwenyewe ndo chanzo cha hao wavivu wengi... Ukitaka muombea mtu ili apate hela , gari nyumba au kazi maana ake unamjenga mtu uvivu aamini upumbavu hayo atayapata kwa kwenda kuombewa balada ya kazi.

Ukiacha hilo ni kweli Watanzania tuwavivu aisee

Uvivu wa watanzania ni mkubwa mnoo.. Yaan hata ukiwa unatembea kwa miguu utagundua hilo yaan watu wanatembea kama makondoo ukiwa na haraka utakasirika njia nzima mtu anatembea kama kavunjwa miguu.. Yaani kuanzia uvivu wa mwili hadi akili.

Na uvivu wetu mkubwa ndo chanzo wengi tapeliwa wanataka shortcuts .
 
Kwanza ye mwenyewe ndo chanzo cha hao wavivu wengi... Ukitaka muombea mtu ili apate hela , gari nyumba au kazi maana ake unamjenga mtu uvivu aamini upumbavu hayo atayapata kwa kwenda kuombewa balada ya kazi.

Ukiacha hilo ni kweli Watanzania tuwavivu aisee

Uvivu wa watanzania ni mkubwa mnoo.. Yaan hata ukiwa unatembea kwa miguu utagundua hilo yaan watu wanatembea kama makondoo ukiwa na haraka utakasirika njia nzima mtu anatembea kama kavunjwa miguu.. Yaani kuanzia uvivu wa mwili hadi akili.

Na uvivu wetu mkubwa ndo chanzo wengi tapeliwa wanataka shortcuts .
Hizi Aya zako za mwisho zimegongelea msumari. Hata uendeshaji magari unagundua tu "hawa watu kwao kutunza muda si lolote si chochote" uvivu kiwango cha juu sana. Mtu hata umlipe pesa bado pesa sio motisha kwake bado atakuwa goigoi kazini na vizingizio tele!
 
  • Mtume Boniphace Mwamposa ametamka: “Watanzania wengi ni wavivu ” Watu wakakasirika, wengine wakabaki kimya. Lakini hii si mara ya kwanza kauli hii kusemwa na mtu maarufu kama Mtume Mwamposa.

  • Mwaka 2011, Rais mstaafu Benjamin Mkapa aliwahi kusema waziwazi kuwa “Watanzania tumejaa visingizio, tunapenda kuwalaumu wengine na hatutaki kufanya kazi kwa bidii.” Alisema haya kwa uchungu, akisisitiza kwamba uvivu ni kikwazo kikuu kwa maendeleo yetu Watanzania wengi wavivu wa kufikiri-Mkapa

  • Hii ina maana moja tu: kwa zaidi ya muongo mmoja sasa, viongozi wetu wamekuwa wakituamsha kutoka usingizi wa uvivu – lakini bado tunasuasua. Tumezoea starehe kuliko jasho, lawama kuliko suluhisho.
  • Hapa majuzi kila mtu anamlaumu Mchina kwamba kajaa Kariakoo amekuja hadi mikoani. Mchina huyohuyo amejaa kila eneo na anafanya "retail" business. Nani alaumiwe? Mchina, mzawa mvivu, au serikali?>

  • Tuna ndoto za maisha bora, lakini hatuko tayari kulala saa 5 na kuamka saa 11 kufanya kazi. Tunataka magari na majumba, lakini hatuwezi kusimamia muda wetu wala kujifunza kwa bidii (matokeo yake hadithi zetu nyingi ni kuwahusu wenye mali nyingi na wenye magari ya kifahari-hao nao tunawaita wana utajiri wa manyoka - hatuamini katika bidii na maarifa kama chanzo cha ukwasi-TUNA SHIDA KUBWA).

  • Uvivu wetu uko kila mahali: kwenye vijiwe, ofisini, mashambani, na hata kwenye ndoto zetu. Tunatamani tusifanye chochote lakini tupate kila kitu. Hii ni ndoto isiyo na mwisho (Nililima kwenye moja ya vijiji vya Tukuyu wenyeji wanataka ujira mkubwa walipwe kwa pay-day na kazi wanafanya kisoda - ikabidi niwe naenda Ileje kuwaleta Wandali wafanye kazi hapo shambani au niende Ntokela kuleta Wasafwa waje kufanya kazi hapo shamba - Tuna shida KUBWA).

  • Kila siku tunakutana na vijana wenye nguvu, elimu na muda — lakini wanaishia mitaani wakisubiri miujiza. Hawajafungua biashara, hawajajitolea, hawajifunzi ujuzi wowote. Wanangoja “koneckshen” ni watu wa kulaumu na matusi, hawana nidhamu yao binafsi wala ya kazi, hawaajiriki-ukiwaajiri lazima wakuibie sana.

  • Si vijana tu – hata taasisi zetu baadhi zimelemaa. Uamuzi mdogo unachukua miezi. Miradi mikubwa inacheleweshwa kwa sababu ya uvivu wa kiutendaji na kukosa uwajibikaji.

  • Tumejifunza kuishi kwa “polepole,” tukikumbatia uzembe kama sehemu ya utamaduni. Lakini dunia haikusubiri – mataifa mengine yanapiga hatua kwa bidii na nidhamu.

  • Kauli ya Mwamposa na ile ya Rais Mkapa zinafanana kwa ujumbe mmoja: Uvivu ni adui wa maendeleo. Na Watanzania wengi, tusipobadilika, tutajikuta tukibaki nyuma zaidi.

  • Kwa hiyo leo, si lawama bali ni wito: Amka. Jitume. Tenda. Tuanze na sisi binafsi. Tufanye kazi kwa bidii, tuthubutu, tuache kusingizia serikali kila siku. Mabadiliko hayawezi kuja kama hatutayachochea wenyewe.
  • Tunazo rasilimali nyingi sana zinazoweza kutukomboa. TUAMKE; TUBADILIKE.

NB: Soma kimyakimya, toa comment, matusi kwenye huu uzi pendwa hayaruhusiwi. Nyadikwa huwa ha tolerate ujinga.

Wahega
Moja ya kazi ya kiongozi ni kujua weakness na strength ya unaowaongoza. Kulalamika bila kuchukuwa hatua ni upumbavu wa hali ya juu. Kuna njia moja kuu ambayo kiongozi anaweza kuichukuwa ili kuondoa hili tatizo nayo ni kuhakikisha kila raia wa nchi anavuna kile anachopanda. Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa uvivu wa watanzania ni wa kutengenezwa kutokana na aina ya uongozi tulio nao. Na zaidi, hata huyo Mwamposya ni mmoja ya watu wanaofanya watanzania wawe wavivu kwa kuwalisha fix zake za mafanikio kwa njia ya mafuta.
 
Moja ya kazi ya kiongozi ni kujua weakness na strength ya unaowaongoza. Kulalamika bila kuchukuwa hatua ni upumbavu wa hali ya juu. Kuna njia moja kuu ambayo kiongozi anaweza kuichukuwa ili kuondoa hili tatizo nayo ni kuhakikisha kila raia wa nchi anavuna kile anachopanda. Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa uvivu wa watanzania ni wa kutengenezwa kutokana na aina ya uongozi tulio nao. Na zaidi, hata huyo Mwamposya ni mmoja ya watu wanaofanya watanzania wawe wavivu kwa kuwalisha fix zake za mafanikio kwa njia ya mafuta.
Nadhani wajibu wake kama kiongozi wa dini ni kutoa mafundisho, kitu ambacho naona kafanya.

Amebainisha gap lililopo.

Ametoa maonyo kama religious leader
 
Nadhani wajibu wake kama kiongozi wa dini ni kutoa mafundisho, kitu ambacho naona kafanya.

Amebainisha gap lililopo.

Ametoa maonyo kama religious leader
Mwamposya huwa anatoa mafundisho au ni chawa wa Samia na pia ni tapeli anayekusanya sadaka za watanzania wavivu? (huu nao ni mjadala) BTW mimi nimesema tatizo ni la uongozi hivyo angeelekeza nguvu zake kwenye huu uongozi anaousifia usiku na mchana! Vijana wamekatishwa tamaa na maelfu ya wapigaji wanaoiba fedha za serikali kwa sababu ya uongozi dhaifu, wanaona kumbe unaweza kuishi bila kufanya kazi. Nakuhakikishia kosa ni lauongozi kwa sababu nchi kama Afrika Kusini ilijengwa kwa asilimia kubwa na wazawa huku wakisimamiwa na wazungu wenye uongozi bora.
 
Mwamposya huwa anatoa mafundisho au ni chawa wa Samia na pia ni tapeli anayekusanya sadaka za watanzania wavivu? (huu nao ni mjadala) BTW mimi nimesema tatizo ni la uongozi hivyo angeelekeza nguvu zake kwenye huu uongozi anaousifia usiku na mchana! Vijana wamekatishwa tamaa na maelfu ya wapigaji wanaoiba fedha za serikali kwa sababu ya uongozi dhaifu, wanaona kumbe unaweza kuishi bila kufanya kazi. Nakuhakikishia kosa ni lauongozi kwa sababu nchi kama Afrika Kusini ilijengwa kwa asilimia kubwa na wazawa huku wakisimamiwa na wazungu wenye uongozi bora.
Focus mkuu. Ukiingiza politics na feelings utashindwa kujenga hoja. Alichosema Mwamposa kina logic hakina!?
 
Yeye mwenyewe ni mvivu ndio maana ameamua kufanya biashara ya kutapeli watu.
 
Focus mkuu. Ukiingiza politics na feelings utashindwa kujenga hoja. Alichosema Mwamposa kina logic hakina!?
Mbona wabongo mnadhani politics ni kitu ambacho hakipaswi kujadiliwa kwenye maisha? CCM imewaharibu kweli kweli. Politics is your life mazee. Hata ukienda kanisani ni politics. Politics siyo ushabiki wa vyama bali ni mambo muhimu kuhusu nchi inavyoongozwa na utendani wa wananchi wote, including viongozi wa dini. Mwamposya ameshindwa kujua chanzo cha tatizo, huwezi kutibu tatizo bila kujua chanzo chake. Upo?
 
Back
Top Bottom