Watangazaji wanaokubalika katika Idhaa za Kiswahili

Hivi qualifications zao ni tofauti na hawa watangazaji wengine wa redio za bongo?mana ni kama wanaongea kwa ufasaha zaidi

Mkuu hawa wanaqualificatio za kiraia yaani kawaida sema nijinsi tu anajibidisha katika vyombo vya habari vya ndani lakin ctaki comparison na watangazi wa redio mawingu cjui wakina mchomvu,dj fet,mbwiga hapana hawa ni wakwe2 na 2nawapenda sana,na elimu kidogo inapewa kipaumbele na maadili ya utangazaji yaani humu jamvini watu wamekula chumvi huenda lakin mwambie umeanza kumsikia othuman miraji lini katika idhaa ya kiswahili,utapewa jibu huta amin.
 
nahisi wabongo tatizo ni lugha ya pili . wakenya wazuri kiingereza na watu kama wanyarwanda wazuri kifaransa
Mkamiti kibayasi-VOA
 
Namkubali sana ibunga muyaombe,vicent makori(miwani) na kuna bibi flan sauti yake inkwaluza balaaa(wa DW)
 
Habari zenu wakuu, Nashukuru kwa fursa hii huenda kukawa kuna makosa katika uandishi wa majina ya hawa ndugu zangu ambao nawakubali huenda kwa uwezo wao binafsi katika nyanja ya utangazaji na uwakilishi katika baadhi ya idhaa za kiswahili,nashukuru kwa kupewa nafasi, 1. Oumylakher Amidou-DW 2. Vicent Mokori-VOA 3. Othuman Miraji-DW 4. Lubunga Biyaombe-BBC 5. Othuman Dodo Abdallah-RFI 6. Kazungu Rose-BBC 7. Dina Shahari-BBC 8. 9. niambie na wengine ambao huenda unawakubali lakina hakikisha wawe ni wale wa idhaa tu ,haya tuendeleze mtiririko huu

huyu wa DW, Humrykher ni mwanamke au manaume?
 
Oumilkheir Hamidou, Mohamed Abdulrahmani, Sekione Kitojo, Kazungu Lozi hawa ni DW. Bashkedash Yushkodai, Lubunga Bya'ombe, Patrice Chiterra BBC Wengine ni Francis Chandiona, Petty Kaunda, Kaleja Kaunda na Willium Njolanje kutoka RSA na mwisho kwenye list yangu ni Taderera na Bernard Otieno kutoka Channel France Internationale (eng). Dah! Zamani kweli!
 
Mkishamaliza wote, mwisho wa siku Charles Hillary ni mwisho wa maarifa

Apepe anko Julius Nyaisangah
 
ndio,mkuu nimemsikiliza majuzi huyo anaitwa abdul shakur abood...kwel anatangaza kiswahili hasa,kama marehemu john ngahyoma naye kwel nilipenda staili yake ya utangazaji.
Shakur Aboud anatangaza vizuri hadi raha aisee!!
 
nahisi wabongo tatizo ni lugha ya pili . wakenya wazuri kiingereza na watu kama wanyarwanda wazuri kifaransa
Mkamiti kibayasi-VOA
Kumbe wengi ni Wakenya enh? Sikuwahi kujiuliza wanatoka wapi! Na kama ni Wakenya basi wengi wao watakuwa kutoka Mombasa manake Wakenya wa Bara, mnh...wanakibamiza sana kiswahili ukutani.
 
ndio,mkuu nimemsikiliza majuzi huyo anaitwa abdul shakur abood...kwel anatangaza kiswahili hasa,kama marehemu john ngahyoma naye kwel nilipenda staili yake ya utangazaji.
huyo abdul shakur ana undugu wowote na hayati 2pac shakur?
 
Back
Top Bottom