Idhaa za Kiswahili hazina wasikilizaji wengi kama tunavyodhani

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Hii ni mada nimetaka kuileta kwa muda mrefu sana ila naona kama ni muda muafaka kufanya hivyo. Kwa muda mrefu kumekuwa na dhana kuwa mtu ukihojiwa na BBC au DW Idhaa za Kiswahili basi dunia nzima imekusikia. Naomba leo nitoe mwanga kidogo kuhusu suala hili.

Kuna vituo mbalimbali vya kimataifa ambavyo vimeanzisha idhaa za Kiswahili, mfano kituo cha Ujerumani cha DW, cha Uingereza cha BBC na cha Marekani cha Voice of America (VOA). Vituo hivi vimetoa ajira kwa Watanzania na vimekuwa nafasi nzuri ya Watanzania kadhaa kuongeza ujuzi na maarifa katika nyanja ya Uandishi wa Habari.

Mada yangu imejikita katika idadi na aina ya wasikilizaji wa Idhaa hizi na impact yake katika majadiliano mbalimbali ya kisiasa, kijamii au kiuchumi. Tofauti na wengi wanavyodhani, vituo hivyo kutokana na lugha wanazotumia katika idhaa hizo, hawana idadi ya maana ya wasikilizaji au watazamaji kwa raia wa nchi hizo husika. Kwa hiyo mahojiano, habari au taarifa zozote nzuri au mbaya zinazoihusu Tanzania zinazotangazwa na vituo hivyo tuziweke katika mizania hiyo itatusaidia sana.

Nikitoa mfano wa Voice of America. Kituo hicho kilianzishwa mahususi kwa ajili ya kupromote image ya Marekani kimataifa. Na kama nakumbuka vizuri, sheria iliyotumika kuanzishwa kwake inasema wazi kuwa kituo hicho hakitafanya matangazo yake ndani ya Marekani (nadhani kuepuka wanasiasa wa Marekani kukitumia kushambuliana wenyewe kwa wenyewe). Kwa maana hiyo basi, Mtanzania anapoenda kufanya mahojiano Voice of America idhaa ya Kiswahili au hata ya Kiingereza, kumbuka wasikilizaji na watazamaji wake wengi wao SIYO Wamarekani.
 
That's Obvious wasikilizaji wake wengi ni huku huku Afrika Mashariki tunakozungumza hizi lugha, wasikilizaji ni wengi ila sio wa nchi za huko. Hata target audience sio wao ni sisi

Kwa minajili hio wasikilizaji ni wengi ukilinganisha na other local TVs/ Radios.
 
Nadhani hizi vyombo zina vituo vya redio Inazoongea lugha mahalia. Kwa Tz wana wafuasi wengi
 
Kama ni msikilizaji wa Radio Free Africa au Radio Tumaini automatically wewe utasikiliza Dw au BBC
 
MC44 Kipangaspecial Farolito Mgeni wa Jiji Daudi Mchambuzi KeyserSoze

Baadhi mliojibu nadhani hamjaelewa msingi wa hoja yangu. Sisemi kuwa huu ufahamu ni mpya kwa wengi.

Ninachosema baadhi ya hoja zinazopelekwa na kutangazwa zinakosa mrejesho wenye nguvu kutoka jumuiya za kimataifa kwa sababu wasikilizaji wake ndiyo sisi wenyewe tu waswahili na siyo raia wa nchi husika.

Nimeshaona mara kadhaa waswahili wenzangu kudhani kuwa mada fulani inaweza kuleta reaction kubwa kutoka jumuiya ya kimataifa kwa sababu tu wameona BBC Swahili, VOA au DW wameiongelea.

Niwaulize hata nyie mliojibu, wangapi wameshafanya utafiti kujua utendaji wa kazi na coverage ya VOA, hata ile ya Kiingereza ikoje?
 
MC44 Kipangaspecial Farolito Mgeni wa Jiji Daudi Mchambuzi KeyserSoze

Baadhi mliojibu nadhani hamjaelewa msingi wa hoja yangu. Sisemi kuwa huu ufahamu ni mpya kwa wengi.

Ninachosema baadhi ya hoja zinazopelekwa na kutangazwa zinakosa mrejesho wenye nguvu kutoka jumuiya za kimataifa kwa sababu wasikilizaji wake ndiyo sisi wenyewe tu waswahili na siyo raia wa nchi husika.

Nimeshaona mara kadhaa waswahili wenzangu kudhani kuwa mada fulani inaweza kuleta reaction kubwa kutoka jumuiya ya kimataifa kwa sababu tu wameona BBC Swahili, VOA au DW wameiongelea.

Niwaulize hata nyie mliojibu, wangapi wameshafanya utafiti kujua utendaji wa kazi na coverage ya VOA, hata ile ya Kiingereza ikoje?
Serikali za mabeberu zina njia nyingi za kupata taharifa hazitegemei hivyo viredio
 
Back
Top Bottom