Watanganyika watakiwa kuondoka Zanzibar!

Yale yale ya South Africa.
Tumewaweka Mazimbu, morogoro hadi wakapata uhuru.
Tumekwenda kufanya kazi kwao, matokeo yake ni kuuawa kinyama.
Ndio litakalofuata huko Zanzibar.
The way the cookie crumbles in Zanznibar.

Wapemba nao wafunge maduka yao Dar es salaam?
Pazuri sana hapo!

Wana bahati haitotokea kwakuwa waTanganyika sio wapuuzi kihivyo japo kila uvumilivu una mwisho!

Bora hao viongozi wa SUK watoe tamko na kuanza kulifanyia kazi tatizo hili! Hakuna anaye sema lolote; sio Shein wala Maalim! Au ndio wanchezeana offside trick (kama jina la kundi ya mduara ya Zenji)?
 
bwana ee, waondoe tu huu muungano wao, huu muungano ni mradi mwingine, watu wanasuluhisha kero za muungano miaka nenda rudi !!
 
chuki za wazenji ni za kidini na si vinginevyo.kwanini bar na makanisa ndo vimekuwa vikichomwa moto? wakati kina shehe Basaleh wakimwaga sumu dhidi ya ukristo hadharani serikali iliwaacha waendelee na matokeo yake ndo haya.

Yeah, Lakini Unasikia wanataka kuwa Wakimbizi Uingereza... Sasa hapo ni Double Standard au ni fitina tu?

Wamejazana London, na wengi wao Wapo kwa sababu ya 1995; Sasa wanafanya uchokozi huo ili tu waondoke Z'Bar?
 
Ccm imewabeba sana hawa pimbi. Nakumbuka miaka ya nyuma sisi tulikuwa tunatakiwa lazima twende zanzibar na passport lakini wao ruksa kuja tanganyika bila hata kitambulisho. Kodi hawakusanyi. Kodi zetu watanganyika ndio zinalipia mishahara ya wafanyakazi wao. Umeme wametumiaa weeeee na deni wamekataa kulipa na serikali ya ccm imewasamehe. Hivi kweli huu ni muungano au utumwa? Watanganyika ustaarabu utatuponza. Hawa jamaa walipofika na wanapotaka kutupeleka siko. Ni wakati muafaka wa kuwaeleza wapemba na waunguja wote walioko tanganyika tukianzia na wale wanaonunua mpunga kyela, wanaofanya kazi katika kiwanda cha sukari kagera, wenye maduka msasani, namanga, tandika, kariakoo na sehemu zingine zote za nchi yetu waanze kuuza mali zao zote kwani sisi tunawapa muda wa kufanya hivyo kwa hiari yao kabla hatujaamua kujichukulia madaraka mikononi mwetu. Tuachieni nchi yetu yenye uhuru wa kuabudu mrudi kijijini kwenu.
 
punguza jazba mkuu two wrongs dont make it right. haya mambo yanayoendelea zanzibar yamenisikitisha sana especially suala la kuchomwa makanisa nashindwa kuelewa and somebody can help on that kuvunjika kwa muungano na makanisa kuna uhusiano gani? inauma sana
 
Maneno yako ni makali sana Comrade ni Kweli Umeonesha hasia zako za ndani kabisa,tulicheka na nyani lakini sasa tunavuna mabua,
Kikubwa ni kupambana na hako kakikundi kadogo ka uamsho ili kasije kugeuka Boko Haramu tukazivuna damu za ndugu zetu hapo baadae
 
Yanayo tokea huko Zanzibar ni hatari kwa mustakabali wa amani kwa taifa hili,hali kama hii ikiachiwa ikachukuwa nafasi hatari yake hakuna ataye weza kuikabili bali machafuko na vita vya wenyewe kwa wenyewe vita shika kasi.Gharama ya kuilinda amani ni kubwa sana.Gharama yenyewe ni uvumilivu na subira miongoni mwetu.

Serikali isipokuwa makini Watanganyika nao uvumilivu utawaishia na majibu yake itakuwa ni pigo kubwa kwa amani ya nchi yetu.Mwalimu aliliona hili mapema ndiyo maana alilikemea kwa nguvu zote bila kuuma uma maneno.Huku kuoneana haya ndiyo matokeo yake yanayojiri leo huko Zanzibar.

Kigezo cha kutaka kuujadili muungano isiwe kigezo cha kuwamaliza ndugu zetu toka bara kwa kuwachomea makazi yao na nyumba zao za ibada.Watanzania hatukulelewa kwa misingi ya kibaguzi ndo maana leo hii wapemba wengi wanafanya biashara zao huku bara bila kubuguziwa.

Dhambi hii ikiachiwa itatumaliza wote na kutia dosari ndani ya taifa letu lililojivunia kuwa kisiwa cha amani.Ombwe hili la uongozi sasa limekwenda mbali ikiwa ni pamoja na kushindwa kufanya majukumu yake ya kuhakikisha amani yetu inalindwa kwa nguvu zote.Dalili zilijionyesha mapema wakati maeneo ya biashara za watanzania toka bara kuchomwa moto lakini hatukusikia hatua yeyote kuchukuliwa leo tena yamejirudia.

Kama staili ya muungano ndiyo inakithirisha kubaguana kuna haja gani ya kuwa na Muungano.Ipo wapi ile interejensia ya jeshi la Polisi kushindwa kuzuia machafuko haya ilihali ikifanikiwa kuitumia kudhibiti maandamano ya wananchi na vyama vya siasa yaliyo halali kikatiba.Kwa hili lililojitokeza huko visiwani kamwe hatutalivumilia kama serikali haitatoa maelezo ya kutosha.Hatuwezi kuvumilia ndugu zetu wakidhulumiwa haki yao ya kuishi kama Watanzania ili mradi hawavunji sheria ilihali wenzetu wanaotoka huko visiwani wanaishi hapa bara kwa amani bila buguza yeyote. Tanzania yetu itajengwa tu na wale wenye moyo safi.
 
Wengi tunajiuliza "kama hawataki muungano" then suala la udini (kuchoma makanisa limetoka wapi?) It's very bad!
 
Tuwaogope kama ukoma waumini wote wa ubaguzi,tuwakemee na tuwape onyo.Kwani wao wana nini wameweza hata sisi tushindwe tuna nini!
 
''panapofuka moshi zima moto chini''
serikari chukueni hatua sitahiki kabula watu hawajaanza kuchomoa majambia yao na kuchinjana kama kuku.
 
Ccm imewabeba sana hawa pimbi. Nakumbuka miaka ya nyuma sisi tulikuwa tunatakiwa lazima twende zanzibar na passport lakini wao ruksa kuja tanganyika bila hata kitambulisho. Kodi hawakusanyi. Kodi zetu watanganyika ndio zinalipia mishahara ya wafanyakazi wao. Umeme wametumiaa weeeee na deni wamekataa kulipa na serikali ya ccm imewasamehe. Hivi kweli huu ni muungano au utumwa? Watanganyika ustaarabu utatuponza. Hawa jamaa walipofika na wanapotaka kutupeleka siko. Ni wakati muafaka wa kuwaeleza wapemba na waunguja wote walioko tanganyika tukianzia na wale wanaonunua mpunga kyela, wanaofanya kazi katika kiwanda cha sukari kagera, wenye maduka msasani, namanga, tandika, kariakoo na sehemu zingine zote za nchi yetu waanze kuuza mali zao zote kwani sisi tunawapa muda wa kufanya hivyo kwa hiari yao kabla hatujaamua kujichukulia madaraka mikononi mwetu. Tuachieni nchi yetu yenye uhuru wa kuabudu mrudi kijijini kwenu.

Naungana na wewe jamaa, .....hivi ugomvi kuhusu muungano una uhusiano gani na makanisa? Tanzania kama jamhuri ya muungano ina uhuru wa kuabudu lakini wazanzibari hawataki huo uhuru kwao uislamu ndiyo dini ya nchi yao.......hakuna sababu ya kuendelea na muungano na watu wenye mawazo mfu kama hao... the ealier the better waondoke warudi kwao unguja na pemba watuachie Tanganyika yetu.....hatuihitaji zanzibar ili tuishi..... we can still do well in there abscence.......tumechoka na ushenzi unaofanywa na watu wanaojiita waislamu wenye msimamo mkali......VUNJA MUUNGANO NA WAHUNI!!!!!!
 
Nachelea kuzungumza kwa hasira, hata hivyo wapo watu wanaofikiri kwa wao kuwapiga wengine, huenda wanaopigwa hawawezi kupiga. Hakuna binadamu mwenye mwili wa chuma, hakuna binadamu awezaye jiona mwamba kwa mtu aliye mstaarabu. Ninafikiri ni vyema waonao kuwa wanaweza fanya jeuri wakajua hata wanaofanyiwa jeuri kama sio hekima na busara na kuthamini utu wanaweza fanya tena kwa nguvu na jeuri mbaya zaidi. Ni wakati wa watu kuona mambo katika uhalisia. Muungano na kuchoma makanisa ni vitu tofauti, na hii inajionesha kuwa kuna watu bado hawajui maana ya uislamu---SLM ndio msingi wake nalo ni amani. Anayeshauri wabara waondoke ikiwa usalama wao wanaona hauwezi kulindwa ni wazo la kutaka kuwapa kichwa, wao wakiondoka basi na hawa wafadhili wao wanaoouza iliki soko la kariakoo na viguo tandika nao wajipange waondoke, wala sio wataondoka. Ninasikitika huku tunakopelekwa na wahafidhina wajifichao katika misingi ya dini.
 
"we either stay together as wise people or die together as fools". Hakuna atakae baki, wakianzisha hiyo itakuwa ni laana itakayowatafuna wote. Hekima inahitajika na serikali ikiwa iko hai ichukue nafasi la sivyo watu watajilinda na hapo ni mwanzo wa mwisho.
 
Wazanzibari wamenishangaza sana wanapotaka wa-Tanganyika waondoke Zanzibar bila ya kuwaita Wazanzibari walioko Tanganyika warudi Zanzibar! Pia wanashangaza pale wanapowaacha wananchi wa nchi nyinginezo waishi kwa raha mustarehe na kuwakazania tu Watanganyika watoke Zanzibar! Mimi nawashauri kama kweli hawautaki Muungano warudi kwao Zanzibar bila ya kuambiwa warudi na waachie post zote za Muungano na zisizo za Muungano, wasihudhurie Bunge la Muungano! Hapo kweli tutaona kuwa hawautaki Muungano, otherwise ni unafiki wa hali ya juu na kuna ajenda iliyofichika!
 
Naungana na wewe jamaa, .....hivi ugomvi kuhusu muungano una uhusiano gani na makanisa? Tanzania kama jamhuri ya muungano ina uhuru wa kuabudu lakini wazanzibari hawataki huo uhuru kwao uislamu ndiyo dini ya nchi yao.......hakuna sababu ya kuendelea na muungano na watu wenye mawazo mfu kama hao... the ealier the better waondoke warudi kwao unguja na pemba watuachie Tanganyika yetu.....hatuihitaji zanzibar ili tuishi..... we can still do well in there abscence.......tumechoka na ushenzi unaofanywa na watu wanaojiita waislamu wenye msimamo mkali......VUNJA MUUNGANO NA WAHUNI!!!!!!

Watu wenye akili zetu tunajua tatizo sio muungano tatizo ni udini. Kibaya zaidi hata hao viongozi wakubwa wa CCM na CUF zanzibar wanacheka na kufurahia hivyo vitendo vya kinyama walivyo wafanyia wakristo na WATANGANYIKA au machogo Kama vile wanavyotuita. Nimewahi kushuhudia mbunge toka Zanzibar akiapa kutompatia mbunge ambaye siyo muislam kura katika uchaguzi wa wabunge wa Africa mashariki mbele yangu na akijua fika kwamba mimi si muislam. Zaidi ya hii nilishaelezwa na the so called friends MIAKA Kama mitano iliyopita kwamba hawataki kanisa lijengwe mtaani kwao na nikamuuliza sasa watoto wangu wakija kutembea Zanzibar watasali wapi? Hakuwa na jibu zaidi ya kujikanyaga tu baada ya kushtuka kwamba amechemka! Mimi nimekuwa karibuni sana na WAZANZIBARI wa rika zote matajiri kwa maskini, wanasiasa wadogo kwa wakubwa na nilichojifunza kwao wote Ni chuki kubwa walionayo dhidi ya WATANGANYIKA. Enough is enough, sasa ni zamu yetu kulianzisha ili wajue kwamba WATANGANYIKA hatuupendi huu muungano kuliko wao. It is time for the referendum! How do we force for referendum to take place? Maoni tafadhali
 
Comrade na genge la watu wachache tu kwa maslahi yao si umeona waliofunguliwa mashtaka 90% ni under 17,genge hili lisiachwe liendelee nashangaa watawala na wanaharakati wako kimya tu siwaoni wale waliombeza Tindu lisu baada hotuba yake pale mjengoni,hata wanyama mwituni watautaka muungano
 
Back
Top Bottom