Watanganyika watakiwa kuondoka Zanzibar!

Mkuu unaandika uwongo uwongo mimi niko zanzibar hilo uloandika lako mwenyewe hakuna kitu hicho zanzibar. Unachochea chuki tu huna lolote mzushi mkubwa .kama ni vile usemavyo wewe nambie mbara gani kapigwa na wanatembea bila kuulizwa chochote WAZANZIBAR WANATAKA dola ya zanzibar bila muungano huu hawana shida na watanganyika,wakenya,wataliana au waarabu watu wanataka nchi yao 2 basi
.Kama suala ni kutaka nchi yenu je njia sahihi ni kuanza kuchoma Makanisa na kutishia waumini wa Makanisa hayo?.Mimi naamini Wazanzibari ni jamii ya watu waotambua ustaarabu wa Dunia ya leo na kama suala ni kudai nchi yenu kujitoa kwenye Muungano ziko njia nyingi tu.Kwa hili sasa mmetufanya sisi wengine ambao huwa hatujibu hoja zenu zisizo na tija tuanze kuingilia kati na kama Wazanzibari hamtambui Wabara wengi katika maisha yao ya kila siku hawana chochote cha kupoteza kama Muungano utavunjika.
 
je inatosha wazazabar kuwaona watanganyika ni adui yao kama wana uthubutu waowangewashughulikia vingozi wao nahilo baraza la uwilishi ili wajitoe kwenye muungano kwakuwa hata watanganyika hawautaki huu muungano hapa ulipofikia ili viongazi wetu ndio wanaungangani hukmsikia jakaya alisema tukizungumzia katiba swala la muungano lisizugumzwe hivyo basi wanzazibar kama mwataka zanzibar yanu badala ya kuua watanganyika na kuchoma mali zao nawashauri mchome nyumba za baraza la wawakilishi na viongozi wenu
 
Tatizo kubwa la wazanzibari ni Ubaguzi kwa misingi ya dini. Naamini wanachoma makanisa kwasababu wanaamini wakristo wengi wanatoka bara. Hivyo kulingana na mtazamo wao, wanapofanya hivyo wanawaadhibu wabara. Utakapovunjika huu muungano wategemee kifuatacho ambacho ni kubaguana wao kwa wao. Unguja itakuwa nchi na pemba itakuwa nchi. Baada ya kuvunjika muungano ni lazima hawa jamaa watatumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe, na kwasababu hiyo basi, ile Dubai wanayoitarajia kuiona itageuka na kuwa Somalia.
 
Me natamani kusikia muungano umevunjika ili tuuze mifugo na mazao yet kwa fedha za kigeni. Jamani ni soko la bidhaa zetu
 
Jamani si tuandae kongamano kubwa dar la kulaani kinachoendelea Zanzibar?
 
Mbna south sudan walipokua wanadai nchi yao hawakuchoma misikiti au kuua raia wa kaskazini? Wao walihangaika na serikali mpk kikaeleweka. Hawa ndugu zetu ni wabaguzi wa imani coz hata sisi tunasoma na m1 alitishia kufukuza wasichana fulani kwenye group disc au yeye ahame kisa tu hawafuniki vichwa japo siyo waislamu, na mpaka leo inawabidi wale wawe wanakuja na mtandio kwa kumwogopa bwana yule yaani yupo too agresive.
 
Mkuu majid. unaweza kua sawa upande fulani na kukosea upandemwengine, mimi nawafaham sana wazenji, machafuko ya kisiasa yaliodumu kwa miaka pamoja na mihadhara na yanayotokea sasa chanzo kikuu ni muungano, mkuu tusijaribu kuuficha ukweli tukatafuta sababu zisizo za ukweli zanzibar hawakuridhika na hawaridhiki na aina ya muungano uliopo ila wanaenda kwa sababu ya nguvu ya viongozi wenye madaraka tu, na nadhani kama katiba yao inavosema juu ya madaraka ya wananchi hawa wana haki tena ya msingi kabisa katika kuujadili muungano,

Lakini si ni hawahawa wabunge wa CCM na CUF kutoka ZNZ walipitisha sheria ya mabadiliko ya katiba kwa mbwembwe nyingi tena kwa kuwabeza wabunge wa CDM?!

Sheria yenyewe ya mabadiliko ya katiba mwanzoni ilikuwa imepiga MARUFUKU kuongelea MUUNGANO na MDARAKA YA rais. Baada ya juhudi za CDM kwenda kumuona Rais ndipo masharti yakalegezwa na kuruhusu kujadili MUUNGANO lakini kwa Lengo la kuuboresha. At least CDM wamefanya MUUNGANO uongeleka.

Kama hawa UAMUSHO hawautaki MUUNGANO mbona hatukuwasikia wakilaani wawakilishi wao wala kuandamana? Ninashawishika kuamini UAMUSHO wana agenda yao SIRI na siyo MUUNGANO. Wanatumia dini because RELIGION IS A MENTAL DISEASE. Na kwa style hiyo wamefanikiwa because most of people will join a band wagon without questioning.
 
Watanganyika bana!!! Nguvu mdomo tu, fanyeni kwa vitendo acheni blah blah. Angalieni Wazenji, action, action, action. Kama kweli mnayaweza na nyinyi yaanzisheni. Sio blah blah blah blah blah blah blah blah blah blah blah blah. Chakubanga.
 
Historia ya Zanzibar inatokea mbali, 1964 waliuwawa watu wengi sana. Sasa sioni kama kuna sababu ya kuendelea kutonesha makovu. Mimi bado nina hoji busara za Polisi kwenye kuanzisha vurugu hizi. Hakukuwa na sababu ya kuvamia watu ambao wameisha wachochea maamuma wao siku zote hizi na kuwakamata. Busara zaidi ilitakiwa, maana ya Zanzibar nani aliye yajua?. Wato bado wana mioyo ya visasi na wanatafuta nafasi tu.

 
Last edited by a moderator:
Wamesahau kwamba wapemba kibao wana majumba na maduka huko Dar!

Mjomba, hata wapemba wakaondoka wote dar na wakaachi hayo maduka na nyumba bado tu kama hatupendani na ukabila wetu tutabaki maskini tu
 
Warudi tu Tanganyika maana inakoelekea sasa itakuwa ni kuviziwa mtu unapotezewa uhai.

kama watanganyika wanafukuzwa zenji basi na sisi wa bara tuanze kupita kariakoo na sehemu zingine tuzoe wapemba wote na wazenji wengine warudi kwao zanzibar....
 
.Kama suala ni kutaka nchi yenu je njia sahihi ni kuanza kuchoma Makanisa na kutishia waumini wa Makanisa hayo?.Mimi naamini Wazanzibari ni jamii ya watu waotambua ustaarabu wa Dunia ya leo na kama suala ni kudai nchi yenu kujitoa kwenye Muungano ziko njia nyingi tu.Kwa hili sasa mmetufanya sisi wengine ambao huwa hatujibu hoja zenu zisizo na tija tuanze kuingilia kati na kama Wazanzibari hamtambui Wabara wengi katika maisha yao ya kila siku hawana chochote cha kupoteza kama Muungano utavunjika.

una ushahidi gani kuthibitisha kuwa waliochoma makanisa ni wazanzibari?? au hao waislamu??

Jee ikiwa hao wanaomiliki makanisa waliyachoma wenyewe??? kwani hawana walinzi wao??? hapa kuna kila aina ya mbinu za propaganda
 
kama watanganyika wanafukuzwa zenji basi na sisi wa bara tuanze kupita kariakoo na sehemu zingine tuzoe wapemba wote na wazenji wengine warudi kwao zanzibar....

hizi ni mbinu wanazotaka kanisa kuzitumia yaani kuzusha haya majambo ili wapate sababu lakini naona ita back-fire sana tu

fikiri zaidi sina haja ya kuandika zaidi
 
Mkuu unaandika uwongo uwongo mimi niko zanzibar hilo uloandika lako mwenyewe hakuna kitu hicho zanzibar. Unachochea chuki tu huna lolote mzushi mkubwa .kama ni vile usemavyo wewe nambie mbara gani kapigwa na wanatembea bila kuulizwa chochote WAZANZIBAR WANATAKA dola ya zanzibar bila muungano huu hawana shida na watanganyika,wakenya,wataliana au waarabu watu wanataka nchi yao 2 basi

Unasema hakuna kitu gani Zanzibar?? Yaani kanisa halijachomwa na gali kuunguzwa au sijakuelewa vizuri vinginevyo naona umekamwatwa pazuri sana na si bure utakuwa umeshiriki kwenye hivyo vitendo wewe!
 
Back
Top Bottom