Watambue madalali wa shetani

Watambue madalali wa shetani

Laaaa hii huwa ni kali, tena hao wachungaji feki wameligawa kanisa kwa grade ya utoaji wa sadaka kuna waumini wa kuanza kutoa sh elf 5 labda mpk laki,wengine kuanzia laki mpk 1 mil,kuna wa kuanzia hiyo 1 mil kuendelea hapa ndipo utajua usemi wa Mungu kule ktk Hosea 4:4. WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA. S kwamba wataangamia suku zijazo bali wanaangamia wakt huohuo ww unapochukua hela yako na kuisend ktk namba za hao wachungaji wa viwango vya sadaka kisha unaenda kulala njaa na watoto hauon kuwa unaangamia kwa mda huohuo?

Una kila aina ya mahitaji ya lazima km nguo za watoto mahitaji ya kila uchao lakin we ni kukimbiza hela kwa huyo mchungaji anakutapeli lakin kakufumba macho kuwa ukitoa nyingi utapata nyingi we unadhani nikutoa pesa upate pesa? Kacheze biko utapata pesa hayo ma-laki unayotoa kwa mwaka ungekuwa unaxcheza BIKO ungeshapata pesa yako taam.

Kutoa kuko hivi km kweli unaaja ya kumtolea Mungu sadaka nenda kwa wahitaji masikin,wagonnjwa,wasiojiweza na jamii yenye uhitaji wako wengi sana,na pale unapojitolea kwa ajili yao unajiwekea HAZINA MBINGUNI si hizi hazina ya kubahatisha kwa hawa wachungaji feki.

Ili somo la zaka na zadaka hawa wachungaji feki wanawaangamiza nao sn waumini wao kwa faida zao binafsi

Njia ya kuwatambua ni so simple. 1. Wanafundisha na kuhimiza watu wawe matajiri hapa duniani tu kwa mafanikio ya muda tu.wanaacha kuwahimiza watu kuutafuta uzima wa milele ulio katika Kristo Yesu. 2. Hawamhubiri Yesu kama ni njia ya wokovu na uponyaji, badala yake wanajiinua wenyewe wakiichukua nafasi ya Bw .Yesu. 3. Mungu wanayemuinua, ni Mungu wao na sio MUNGU Baba wa Bw.Yesu Kristo.. Kwa mfano ,:- mungu wa machomanne, mungu wa kanisa Machomanne NK, NK. 4.Angalia matunda yao sio matendo yao-- Wazinzi, Wanazaa nje ya ndoa zao, Wafiraji, Wabakaji, Watu wenyewe visasi.. 5. Wananena kwa Lugha zisizofahamika wakiunga na kiswahili kama za watoto wanaojifunza kuongea (baba, mama, Dada, kaka, tata, Toto, dodo, moto,raba, sata,maka, NK,NK.), ukiwabana wanakwambia wanaongea lugha ya kimalaika.. 6.Zingatia haya:--- a.Lugha ya malaika hata ibilisi anafahamu kwa vile naye ni malaika. b. Watu wanapaswa kufundishwa kuhusu safari ya kwenda mbingini aliko Yesu, na sio Ulaya wala America. c. Utajiri wa duniani sio kipaumbele cha mkristo bali ni Ufalme wa Mbinguni. Utajiri ni kitu cha nyongeza..
 
Sawa kwa kutoa unapokea, sipeleki kanisani au msikitini, nawapa mwenyewe watu wanaonizunguka kwani ninawafahamu. Nimekosea?
Kusaidia maskini ni kazi takatifu, kutoa Zaka na Sadaka ni kazi njema pia, hapa jambo linalo zumgumziwa ni kwamba Viongozi wa dini wanazitumiaje nafasi zao hizo ?
Ivi utapenda sadaka yako itumike kununulia pombe au kuhonga wanawake za watu au waumini ?
Sadaka inabidi ifanya kazi njema ya kueneza Injili na kusaidia maskini.
Sadaka au zaka inapaswa impe mahitaji muhimu (kama kula na malazi) kiongozi wa Dini na inayobaki ajenge Kanisa Bora, na inayobaki aitumie kupanua kazi ya Uinjilishaji, na inayobaki awekeze katika huduma za kusaidia jamii kama Hospitali Shule nk.
Zaka na Sadaka zifanye kazi iliyokusudiwa na siyo nje ya hapo.
Ndiyo Lengo La Mada hii.
 
Waumini wengi wanapenda miujiza kuliko kumpenda Mungu na hapo ndipo wanapoibiwa wengi, mtu yuko tayari atende dhambi na machukizo ya kila aina hataki kuskia habari za Mungu ila akisikia kuna mtumishi flani anatenda miujiza na yeye huyo anajumuika
Halafu muujiza wenyewe Eti wa kupata gari la kutembelea, sasa sijui hiye service ya hilo gari nayo ifanyike kwa miujiza pia labda.
Hawajui kulihudumia gari linalo tembea ni ghalama zaidi ya kulinunua, kama huwezi kununua gari hata kulitunza hautaweza kabisa.
Hakuna muujiza mkubwa kama,
Jinsi ulivyoumbwa na kuwekwa duniani bila hiyari yako.
Jinsi ulivyo na afya njema na unaishi salama.
Jinsi unavyopata mahitaji muhimu kama chakula, hewa, maji, malazi na mavazi,
Jinsi ulivyopata bahati ya kulisikia Neno la Mungu aliyekuumba.
Jinsi Mungu alivyokuahidi kuwa hata ukifa atakufufua tena na utaishi maisha bora zaidi ya haya.
Jinsi unavyoshirikia kwa upendo na ndugu na jamaa zako.
Jinsi unavyojiweza hata kumudu kufanya kazi za kukupa ridhiki ya kila siku na kuhudumia familia yako.
Jinsi unavyo ishi kwa uhuru na amani.
Jinsi unavyopata nguvu ya kumwabudu Mungu aliyekuumba
Nakadhalika nakadhalika nakadhalika.
Hii ndiyo miujiza mikubwa zaidi uliyotendewa bila ghalama yoyote.
Utajiri wa mali sio muujiza ndiyo maana Yesu Kristo mtenda miujiza hakutaka kuwa tajiri, wala hakuwapa maskini utajiri.
Bali aliwapa afya njema kwa kuwaponya magonjwa yao, na pia aliwapa Uzima kwa kuwafufua wafu.
Kuna watu wakipata mali ndio wanaharibikiwa kabisa, na kuzama moja kwa moja kwa Shetani.
Tafuteni Kwanza Ufalme wa Mbingu hayo Mengine ni ya Ziada tu.
 
Tutawatambuaje hali ya kuwa wanatenda miujiza ya kuponya na kufufua kama manabii walio tangulia?

Kuhusu utajiri wao ni neema zitokanazo na kulishwa shambani mwa Bwana.
Waumini tumeaswa kwenye maandiko matakatifu tuwalishe watumishi wa Mungu.

Hata wateule wa zamani kina Daudi na Suleimani walikuwa matajiri wakubwa kupitia ukulima, ufugaji na uhunzi wa zana mbalimbali.

Mkuu mshana jr unataka kutuaminisha ya kwamba dhana ya uwepo wa dini ni utapeli uliotukuka?
Je, hujawahi kushuhudia matendo makuu ya Mungu ktk kuishi kwako hapa Duniani?

Tusiwahukumu kwa matendo yao na umiriki wao wa mapambo ya Dunia, vyote tutaviacha hapahapa.

Kwa Mungu kila goti litapigwa.
Kila mmoja apambane kuurithi ufalme wa Mbinguni.
Hakuna Nabii , wanaponya wapi kiini macho na mipete yao ya Nigeria
 
Hawa si wengine bali ni mitume na manabii wa uongo (sio wote, namaanisha mitume na manabii wa uongo)
Utawambuaje?
Hawatoi bali wanapokea
Hawafuati bali wanafuatwa
Hawachangi bali wanachangiwa
Hawalishi bali wanalishwa
Hawahudumii bali wanahufumiwa
Kwao kila kitu ni fedha
Mahubiri yao ni utajiri na kutenda miujiza... Wanashindana kwa vitu vya kidunia.. Utajiri, vyombo vya usafiri, (magari boat, meli ndege nk) mavazi ya bei ghali, majumba ya gharama kubwa nknk... Ni watu wasiopitwa na fasheni yoyote
Ni wachoyo na ni wa binafsi wamepiliza! Pesa zao zinazotokana na kuwakamua waumini maskini na wenye uhitaji hawazitumii kwa manufaa ya jamii bali wao wenyewe na watu wao wa karibu
Pamoja na mabilioni wanayomiliki daima utawakuta mitandaoni wakishindana kupost vitu wanavyomiliki vya bei ghali...
Wakiamua kuwekeza pesa zao hizo ni kwenye biashara na kamwe sio kwenye huduma za kijamii kwa wasiojiweza kama lishe elimu afya na vituo vya misaada kwa walemavu yatima na yeyote mwenye uhitaji wowote .. Haya sio yao haya hayawahusu. ..
Watu wa kaliba hii wanaojipenda kujikweza na kupenda kutukuzwa, wapenda Mali na ibada za karamu zilizojaa ukakasi mwingi ni makuwadi wa kuzimu na madalali wa shetani

NB: Niombe radhi kwa wale watakwaza na hii mada


Kwa hiyo ndugu yangu mshana jr baadhi ya hawa ndugu zetu tunaowachangia michango ya harusi na wao hawatoi chochote kumbe nao ni mashetani na wanafunga ndoa na mashetani wenzao?
 
Hakika dini ya Haki mbele ya Allah au Mwenyezi Mungu muumba was mbingu na Ardhi na vilivyomo ndani yake ni UISLAM.
 
Tutawatambuaje hali ya kuwa wanatenda miujiza ya kuponya na kufufua kama manabii walio tangulia?

Kuhusu utajiri wao ni neema zitokanazo na kulishwa shambani mwa Bwana.
Waumini tumeaswa kwenye maandiko matakatifu tuwalishe watumishi wa Mungu.

Hata wateule wa zamani kina Daudi na Suleimani walikuwa matajiri wakubwa kupitia ukulima, ufugaji na uhunzi wa zana mbalimbali.

Mkuu mshana jr unataka kutuaminisha ya kwamba dhana ya uwepo wa dini ni utapeli uliotukuka?
Je, hujawahi kushuhudia matendo makuu ya Mungu ktk kuishi kwako hapa Duniani?

Tusiwahukumu kwa matendo yao na umiriki wao wa mapambo ya Dunia, vyote tutaviacha hapahapa.

Kwa Mungu kila goti litapigwa.
Kila mmoja apambane kuurithi ufalme wa Mbinguni.
Umeongea point mkuu
 
Mshana jr leo umekuja kivingine
Niongezee tu moja pia hupenda kuita kufuatwa badala ya kufuata
Huku wakiamini Mungu wa kweli hupatikana walipo tu
 
Tutawatambuaje hali ya kuwa wanatenda miujiza ya kuponya na kufufua kama manabii walio tangulia?

Kuhusu utajiri wao ni neema zitokanazo na kulishwa shambani mwa Bwana.
Waumini tumeaswa kwenye maandiko matakatifu tuwalishe watumishi wa Mungu.

Hata wateule wa zamani kina Daudi na Suleimani walikuwa matajiri wakubwa kupitia ukulima, ufugaji na uhunzi wa zana mbalimbali.

Mkuu mshana jr unataka kutuaminisha ya kwamba dhana ya uwepo wa dini ni utapeli uliotukuka?
Je, hujawahi kushuhudia matendo makuu ya Mungu ktk kuishi kwako hapa Duniani?

Tusiwahukumu kwa matendo yao na umiriki wao wa mapambo ya Dunia, vyote tutaviacha hapahapa.

Kwa Mungu kila goti litapigwa.
Kila mmoja apambane kuurithi ufalme wa Mbinguni.
Soma Biblia yako muujiza ni kwa watu wasioamini
Je sisi ni kipi tusichokiamini au hatujaambiwa
Na wao wanatumia nafasi vizuri
 
Sasa mshana ndiyo nini hivyo wakati nilikuwa nishapanga kuanzisha huduma ya kuponya na kanisa langu liwe kubwa la kifahari sasa ushanikatisha tamaa naona uvivu kuanza huyu mungu wa baphomet anasaidia baadhi ya watu.....
baphomet goddess wa ashki..beelzebub...memphis.horus wanawasaidia watu kupata wateja kanisani inexchange of their souls
 
Hakika dini ya Haki mbele ya Allah au Mwenyezi Mungu muumba was mbingu na Ardhi na vilivyomo ndani yake ni UISLAM.
Uislam sio DINI ni mfumo wa maisha unaowapasa watu kuishi kama alivyoishi Mudy.

Unajua maana ya Dini?

Unaweza kuthibitisha kuwa uislam ni dini?
 
Tutawatambuaje hali ya kuwa wanatenda miujiza ya kuponya na kufufua kama manabii walio tangulia?

Kuhusu utajiri wao ni neema zitokanazo na kulishwa shambani mwa Bwana.
Waumini tumeaswa kwenye maandiko matakatifu tuwalishe watumishi wa Mungu.

Hata wateule wa zamani kina Daudi na Suleimani walikuwa matajiri wakubwa kupitia ukulima, ufugaji na uhunzi wa zana mbalimbali.

Mkuu mshana jr unataka kutuaminisha ya kwamba dhana ya uwepo wa dini ni utapeli uliotukuka?
Je, hujawahi kushuhudia matendo makuu ya Mungu ktk kuishi kwako hapa Duniani?

Tusiwahukumu kwa matendo yao na umiriki wao wa mapambo ya Dunia, vyote tutaviacha hapahapa.

Kwa Mungu kila goti litapigwa.
Kila mmoja apambane kuurithi ufalme wa Mbinguni.
Endelea kuwaamini
Mkuu kama hujamwelewa mshana hutokuja mwelewa yeyote pole yako evidence + reality hujamwelewa....
Endelea kutoa sadaka ukijua ni sadaka inaenda kunakopaswa..
 
Mi nafikiri tunashindwa kutofautisha mambo hapa.Wale watu si kwamba wao wanakuponya au wanatatua shida zako,bali imani yako.Wanachokifanya kikubwa ni kukuongoza tu ili imani yako itokee kwenye maandiko matakatifu.Ndio maana mzazi wako alipoongozwa na huyu mchungaji na yeye akaweka imani basi akaanza kuona mabadaliko.Kwa mjadala huu tutaaminishwa kuwa watumishi wote ni manabii wa uongo.Ni seme tu kwamba hawa jamaa wamejikita kutafasiri neno la mungu physically yaani katika mambo ambayo ni matamanio ya mwili na si spiritually.Kutafasiri neno la Mungu kiroho unahitaji roho mtakatifu,hapo dipo nguvu za kumbadilisha muumini zinakuwa za kudumu.Kimsingi hawa manabii wengi wao wamekosa nguvu za roho mtakatifu ndio maana wamebaki kutumia nguvu zao wenyewe kuwaaminisha watu kwa kuonyesha utajiri.Na kwa sababu imani yako ndio inakuponya basi wanajithidi wavute imani za watu ili waonekane wana Mungu.Changamoto ni kwamba wale wanaotengeneza imani zao kwa kuangalia uwezo wa nje wa hao jamaa wanakuwa katika matatizo yasio isha kila siku unakuta wanatoka kwa huyu wanaenda kwa huyu matatizo yao yanapoa kwa muda tu.Utawatambua kwa kauri zao,wanavyowasifia hao manabii kwa majina bila kutambua jina la kristu.
Hawa manabii ni mara chache sana kuubiri injiri ya kutoa kwa masikini,kwa wajane,kwa wakimbizi,kwa wagonjwa,na kwa yatima au kwa kifupi injiri ya Upendo kwa wengine.Kwa sababu injiri hiyo ndipo kristu alipo na wao hawapo kwa ajili ya kristu hapo ndipo nakubaliana na mleta mada.
Tambua ndugu kuwa mtu yeyote anaweza akauubiri injiri,lakini si kila mtu anaweza kuubiri injiri takatifu,Mtu yeyote anaweza kubeba Biblia na hata kuisoma mpaka akapata Phd,lakini si kila mtu ana uwezo wa kubeba Biblia takatifu,na kuisoma.Hata sadaka wanazotumia kujenga na kununua magari ya kifaari na ndege,si kwamba wanatumia sadaka takatifu kwa sababu mtu yeyote ana uwezo wa kutoa sadaka awe ameua,awe ameeiba wao wanachukua tu,ila si kila mtu ana uwezo wa kutoa sadaka takatifu na hata kuitumia sadaka takatifu utaongozwa na roho mtakatifu.Si kwamba yesu Kristu waumini waliokuwa wanamfuata walikuwa hawatoi sadaka za kumfanya awe tajiri kimwili,bali alizigeuza na kuwa sadaka takatifu kwa kuimiza Upendo kwa walio masikini na wenye shida.
ni kweli usemayo na ndio maana sijasema watumishi wote ni feki...ila wengi wao ndio wanachafua wenzao mifano mizuri wakiwemo hao tajwa hapo juu.


Neno mwenyewe alisema watu wake tunapotea kwa kukosa maarifa. haya yote yasingekuwepo kama watu wangeshika Neno.
 
Back
Top Bottom