Wataalamu wa Maabara watoa dukuduku lao, kuhusu sakata la utoaji majibu yasiyo sahihi katika Vituo vya Afya

Mdeke_Pileme

JF-Expert Member
Aug 24, 2013
1,563
2,126
Baada ya jukwa la JamiiForums kuchapisha nakala kwenye mitandao ya kijamii inayosema :-

Bodi ya Maabara Binafsi za Afya ambayo ipo chini ya Wizara ya Afya imesema inayafanyia kazi madai kuwa baadhi ya Maabara zinatoa majibu ya uongo ili Zahanati ziuze Dawa, ikiwa ni ufafanuzi uliotolewa baada ya Mdau wa JamiiForums.com kuibua hoja hiyo.

Soma:

Bodi hiyo imesema kwa kushirikiana na Bodi ya Ushauri wa Hospitali Binafsi imeanza ufuatiliaji na itachukua hatua kwa wote watakaobainika kufanya vitendo hivyo

Bodi imetoa wito kwa Wananchi kutoa taarifa za vitendo vya aina hiyo ya Wataalam wanaotoa majibu yenye mashaka au ya uongo ili waweze kuuza Dawa kwa kupiga simu ya bure na 199 na kutoa taarifa.

MAELEZO YA WATAALAMU WA MAABARA YALIYO TOLEWA KUPITIA UKURASA WAO WA INSTAGRAM :-
KWA HESHIMA KUBWA.
• Tunapenda kuwasilisha ushauri kuhusu suala la uchache wa wataalamu wa maabara kazini katika vituo vya afya, na athari zake kwa huduma za afya. Hali hii inahitaji kuchukuliwa hatua madhubuti ili kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana kwa wananchi.

• Athari za Vipimo Kupimwa na Wasio Wataalamu wa Maabara au watu ambao hawana mafunzo sahihi ya maabara, kuna hatari kubwa ya matokeo potofu au ya uongo kutolewa. Hii inaweza kusababisha kutopata tiba sahihi au matibabu yasiyo na ufanisi, hii ni pamoja na kutokuajili wataalam wa maabara wa kutosha katika vituo vya afya, Hali hii inaleta athari mbaya kwa utoaji wa huduma za afya. Kutokana na hali hii, tunapendekeza serikali ichukue hatua zifuatazo:

1• kufuta Sheria ya mwaka 2007 inayo ruhusu wasiokuwa wataalam wa maabara kufanya vipimo vya mkojo na damu katika vituo vya afya, zahanat pamoja na hospital, kwa sababu wataalam wa maabara wapo wa kutosha na bado wapo mitaani bila ajira.

2• Tunapendekeza serikali iweke mikakati ya kuacha kuwapa vipaumbele watu ambao si wataalamu wa maabara [ NON LAB TESTERS ] katika vituo vya afya serikalini pamoja vituo vya afya binafsi . Hii itahakikisha matokeo sahihi ya vipimo na ubora wa huduma za afya. Njia za kufikia lengo hili ni pamoja na kuimarisha mchakato wa ajira kwa kutoa kipaumbele kwa wataalamu wa maabara wenye sifa sahihi, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi ikiwemo semina kwa wataalamu wa maabara , pamoja na kuweka masharti ya kisheria ya kuajiri wataalamu wa maabara.

3• Kuunda sera na mipango ya kuhamashisha wataalamu wa maabara kufanya kazi katika vituo vya afya, ikiwa ni pamoja na kuweka mishahara stahiki.

4• Kuweka mifumo imara ya udhibiti wa ubora ili kuhakikisha vipimo vinapimwa na wataalamu wa maabara wenye ujuzi na matokeo yanatolewa kwa usahihi.

KWA HESHIMA,
• Tafadhali tunaomba Wizara ya Afya itoe kipaumbele katika kuajiri wataalamu wa maabara kwa kuzingatia ripoti iliyotayarishwa na wataalam wa maabara inayobainisha upungufu mkubwa wa wataalamu wa maabara katika vituo vya afya. Kufanya hivyo kutaimarisha huduma bora za afya na kukuza ustawi wa jamii.

TANZANIA MEDICAL LABORATORY ASSOCIATION- TMLA
[ EMAIL : TMLA@secretary.net ]
 
Makanjanja wanapopewa dhamana ya kuangamiza afya za watu kwa kigezo cha "sayansi", lazima hatua madhubuti zichukuliwe dhidi yao.

Hawa ni wale wenye D MBILI waliosoma Kairuki University na BUGANDOOH.

Kwa lugha yetu ya kikerewe BUGANDOOH maana yake ni uji mzito wa mtama. Unaweza ukaona ni jinsi gani hawa wazee wa BUGANDOOH wenye D MBILI wamesheheni uji mzito kwenye vichwa vyao.

Katika vitu vyote, mimi BICHWA BIN KOMWE, kitu ninachoweza kukifanya kama chaguo la mwisho ni kupeleka komwe langu kwa hawa makanjanja wa TIK TOK ERA.

Aione DR Mambo Jambo
 
Makanjanja wanapopewa dhamana ya kuangamiza afya za watu kwa kigezo cha "sayansi", lazima hatua madhubuti zichukuliwe dhidi yao.

Hawa ni wale wenye D MBILI waliosoma Kairuki University na BUGANDOOH.

Kwa lugha yetu ya kikerewe BUGANDOOH maana yake ni uji mzito wa mtama. Unaweza ukaona ni jinsi gani hawa wazee wa BUGANDOOH wenye D MBILI wamesheheni uji mzito kwenye vichwa vyao.

Katika vitu vyote, mimi BICHWA BIN KOMWE, kitu ninachoweza kukifanya kama chaguo la mwisho ni kupeleka komwe langu kwa hawa makanjanja wa TIK TOK ERA.

Aione DR Mambo Jambo
🤣🤣🤣🤣
 
Makanjanja wanapopewa dhamana ya kuangamiza afya za watu kwa kigezo cha "sayansi", lazima hatua madhubuti zichukuliwe dhidi yao.

Hawa ni wale wenye D MBILI waliosoma Kairuki University na BUGANDOOH.

Kwa lugha yetu ya kikerewe BUGANDOOH maana yake ni uji mzito wa mtama. Unaweza ukaona ni jinsi gani hawa wazee wa BUGANDOOH wenye D MBILI wamesheheni uji mzito kwenye vichwa vyao.

Katika vitu vyote, mimi BICHWA BIN KOMWE, kitu ninachoweza kukifanya kama chaguo la mwisho ni kupeleka komwe langu kwa hawa makanjanja wa TIK TOK ERA.

Aione DR Mambo Jambo
😀😀😀😀
Kumbe we ni mkerewe...
Mkerewe wa Wapi Mlitunguru au Nansio au Mkasika 😀😀
 
Makanjanja wanapopewa dhamana ya kuangamiza afya za watu kwa kigezo cha "sayansi", lazima hatua madhubuti zichukuliwe dhidi yao.

Hawa ni wale wenye D MBILI waliosoma Kairuki University na BUGANDOOH.

Kwa lugha yetu ya kikerewe BUGANDOOH maana yake ni uji mzito wa mtama. Unaweza ukaona ni jinsi gani hawa wazee wa BUGANDOOH wenye D MBILI wamesheheni uji mzito kwenye vichwa vyao.

Katika vitu vyote, mimi BICHWA BIN KOMWE, kitu ninachoweza kukifanya kama chaguo la mwisho ni kupeleka komwe langu kwa hawa makanjanja wa TIK TOK ERA.

Aione DR Mambo Jambo
Umeangalia qualifications zao,?? Sifa za kujiunga na Laboratory, Clinical officer and pharmacy ni zote zinafana mkuu...
 
Wenyewe wanasema, hawatoi hayo majibu, Bali vipimo vinapimwa na watu ambao hawana mafunzo sahihi, Mfano nurse, CO na medical attendant ndo wamevamia fan yao.
Hili nikweli kabisa unamkuta mtu professional yake ni nurse,co au yeyote ilimuladi kaelekezwa namna kutumia kipimo basi yeye nikutumia Tu , principle ya kipimo hajui aandaeje huo mkojo au dama ili pate majibu sahii hajui yy nikuwekatu itakavyo soma ivo ivo anakutupia majibu yakoo hili swala nipana Sana 🙏
 
Kuna siku nilichanganya fanta na mkojo niliambiwa na UTI iliyofikia kiwango cha juu.🙂🙄 nilijiuliza hata harufu ya soda nayo kashindwa kufahamu
😀😀, dah aise mambo ni ovyo sana mkuu,, au walivyo sema wenyewe kuwa kuna vijakazi, siyo wataalam ndo maana mambo yapo ovyo.
 
Duh, Ivi serikali hajui haya mambo, au bora liende, Malaria, UTI, minyoo, daa wanagawa sana... Kama unapewa karanga

Wizara ya Afya, bila shaka mpo humu kwenye jukwa Wizara ya Afya Tanzania , Toeni angalau kuhusu haya malalamiko 🤝🤝
 
Hili nikweli kabisa unamkuta mtu professional yake ni nurse,co au yeyote ilimuladi kaelekezwa namna kutumia kipimo basi yeye nikutumia Tu , principle ya kipimo hajui aandaeje huo mkojo au dama ili pate majibu sahii hajui yy nikuwekatu itakavyo soma ivo ivo anakutupia majibu yakoo hili swala nipana Sana 🙏
BICHWA KOMWE -, amesema ufaulu au vigezo vya kujiunga na Maabara kwamba ni D mbili 😁😁, je ni sahihi...
 
Back
Top Bottom