Wewe ulitumia vigezo gani kuwapa kazi hao jamaa? Nadhani wewe ndo unatatizo, na zero kabisaNaandika kwa uchungu sana. Nilipewa instructions ya kutafuta kampuni ya IT hapa Tz kudisign app na web kwa ajili ya masuala fulani fulani. Nikawacheck jamaa fulani ni IT wazuri tu (kwa mjibu wao na ka kampuni kao uchwara) na mmoja kasoma US mwingine China. Nikawapa 15,000,000/= waanze kazi. Hii ni baadhi ya malipo ya awali.
Miezi mi4 hakuna feedback. Tukasema tusubiri labda jamaa wako kazini. Miezi 6 hola. Miezi 12 hola. Huku na huku nikapigiwa simu kazi tayari. Nikasema poa. So nilikuwa mbali. Nikamtafuta software engineer ni mkenya afanye testing. Aisee jamaa alicheka sana. Ikasema hao vijana wamegoogle templates wameedit na kupachika na ni bogus development.
Idea ilikuwa kuwa na software inayotrace magari ya kumpuni, yako wapi, yametembea kilo ngapi and other staffs-Real time data.
Wakaishia kutengeneza utopolo tu. I guess wako humu pia. Ilibidi tulipe upya tukapeleka project Rwanda. Vijana wamedesign from scratch na within 4 month wamekabidhi kazi.
Sasa naelewa kwa nini watu hawataki kuwekeza kwenye IT Bongo. Ujinga mtupu. Hawa vijana wetu wafuge tu kuku kwa kweli. Hivi nyie ndo mtaweza hata kushindana na Bolt+uber?.
Anyway sijui CS/IT mnafundishwa nn huko vyuoni. Natamani kujua mitaala yenu.
100% disappointed.