Wassira: CHADEMA kufa ni Ngumu

Wassira: CHADEMA kufa ni Ngumu

Kuna watu wengine wakiongea unaogopa hata kusikiliza, sawa na sur.............yake
 
Amekwisha huyo, hata wanaomsikiliza lazima wanakasoro kama zake
 
Hatimaye waziri wa Jk bwana Stephen Wasira kakili kuwa CHADEMA haiwezi kufa kirahisi na CCM wasibweteke na kudhani kitakufa kama walivyopanga huko nyuma na kuwaomba waangalie njia mbadala ikiwemo kumshawishi msajili wa vyama vya siasa kukifuta.

Source Gazeti Jamuhuri

Kumbe sasa akili zimeanza kuwaingia vichwani. Nadhani hii kauli imekuja baada ya kichapo cha 4-0 jijini Arusha ambako yeye (wasira) ni mlezi wa ccm mkoa wa Arusha na alipiga kambi huko lakini wameambulia aibu ya mwaka. Na atambue kwamba Chadema haitakufa pamoja na mipango yote miovu wanayoipangia hadi 2015 inachukua nchi na wao wanabaki kuwa watazamaji.
 
Huyu zee la nyani la Gombe si alisema kuwa CHADEMA itakuwa imekufa na kupotea katika miaka 2 ijayo?
Sasa baada ya mikakati yake akisaidiana na kina Mchembe,Polisiccm na Usalama wa Taifa wamegundua kuwa CHADEMA ni maji marefu.

Ifuatayo ni mikakati iliyoshindwa ya Wassira na Magamba wenzake:

  1. Wamejaribu kutengeneza video fake zimeshindwa
  2. Wametunga kesi za kubambikiza kwa Viongozi na Wanachadema zimekwama.
  3. Wamejaribu kufuta au kutengua Ubunge wa baadhi ya Wabunge wa CHADEMA wameshindwa.
  4. Wameteka waandishi wa Habari na Viongozi wa Madaktari wameshindwa.
  5. Wamemwua mwandishi wa Ch.10 Daudi Mwangosi wakashindwa.
  6. Wameua watu kwenye mikutano na maandamano ya CHADEMA bado wameshindwa.
  7. Wamechochea udini,ukabila na itikadi wameshindwa.
  8. Wametumia Bomu la Kivita la kutupa na mkono kwenye mkutano wa kampeni wa CHADEMA pale Soweto na kutaka kumwuua Mwenyekiti Taifa na Mbunge A Town bado wakashindwa.

Sasa wanataka kumtumia kiranja wao Mkuu John Tendwa aifute CHADEMA kwa sababu dhaifu kabisa ati ya kutaka kuanzisha vikundi vya ukakamazu na ulinzi shirikishi ndani ya CHADEMA. Vikundi kama hivi vipo hata ndani ya CCM na jamaa zao wa CUF lakini Tendwa amenyamaza kimya!!!

Nataka tu nimshauri Tendwa ushauri wa bure kabisa kuwa Watanzania ni wapole sana na waungwana sana.Watanzania ni wavumilivu na wastahimivu sana. Watanzania ni wapenda amani. Lakini kwa namna Serikali ya CCM inavyotawala(siyo kuongoza) kwa sasa Watanzania hawahawa wenye sifa nilizozitaja hapo mwanzo wanabadilika kidogokidogo! Kama Tendwa ana macho ya kutazama na aone sasa, kama Tendwa ana masikio ya kusikia na asikie sasa. Kwamba Watanzania wameshachoka na siasa za CCM za kutaka kuwaburuza Watanzania kama vile hawana akili.

Namsihi Tendwa akae,atafakari na aone kama ana macho kile kilichotukia Arusha kwenye Bomu la Soweto na mrejesho wa hisia za Wana Arusha kwenye matokeo ya Chaguzi za Kata 4 za Udiwani hapo Arusha. Kama ana macho ya kuona na aone sasa.

Lakini pia namsihi Tendwa akae na atafakuri kile kilichotokea Mtwara kuhusu Gesi asilia na kinachoendelea kufukuta chini kwa chini hukohuko Mtwara kwa sasa.Bila shaka amesikia na kama hajaona basi afike Mtwara ajionee mwenyewe uhalisia na mambo asingoje kusimuliwa.

Akisha tafakari yote haya sasa ndipo apime na aone kama itakuwa ni busara kwake kuifuta CHADEMA kwenye daftari lake la kuandikisha vyama. Kama hana akili na busara za kutafakuri basi aendelee na mpango wake na hao magamba wenzake kuifuta CHADEMA ambao bila shaka kwao ni mpango PLAN B au C. Tendwa atangaze hata kukifuta leo halafu aone nini kitafanyika nchi nzima.Kama ana simu ya Mohamed Morsi wa Misri ampigie amwulize nini walichofanya Wamisri kwa serikali yake!

Na ndipo Tendwa atakapojua kwamba hupashwi kuchezea nguvu ya Wananchi(Umma) kwa namna yoyote ile.

Mmmh mkuu umeongea points tupu ila maccm yamevaa miwani ya mbao, pia tendwa anatumika kama remote control. Sasa ni kweli wajaribu kuifuta chadema waone kazi..nchi haitatawalika kama alivyosema dr slaa...japo maccm yanajifanya hayaelewi dr.slaa alimaabisha nini kusema nchi haitatawalika..nikutokana na upuuuzi wao mfano wanavyotishia kuifuta chadema hebu wajaribu waone tutakachowafanya..ohooo chezea nguvu ya umma wewe!
 
Sifa za Wasira ni adhimu miongoni mwa Wagombea urais kupitia CCM na hata Dr.Slaa anajua kibarua kitakuwa kigumu kwa upande wa CHADEMA.
Wewe ni nani kuliko Lowasa anaeogopa?
We ni nani kuliko Dr.Slaa anayehofia ?

weka mezani hizo unazoita 'sifa za wassira' ili tuzipime na kuona kweli zina mashiko tukilinganisha na potential candidates wengine ndani na nje ya ccm
 
ccm itakufa kwa kujaribu kukiua chadema, take it from me

Uko sahihi kabisa. Niliwahi kusema na nitaendelea kusema...tafsiri ya demokrasia ya vyama vingi vya siasa kwa ccm ni 'kudhibiti' au 'kuua' vyama vya upinzani kwa nguvu zake zote. Mzee Mkapa alifanikiwa sana katika hili na kilichofuata ni ccm kubweteka na kuendelea kuamini kuwa njia hiyo ndiyo njia pekee ya kuifanya ccm iendelee kushika hatamu za uongozi. Tulitegemea ziara ya sekretariati ya CCM kule China itakuwa imepata fursa ya kijifunza mbinu mpya, lakini mwenendo wa kampeni za hivi karibuni za ARS na kwingineko ulikofanyika uchaguzi wa madiwani hazijaonyesha mabadiliko yoyote. Ni mbinu zile zile ambazo wananchi wameshazichoka!

Matokeo yake sasa hakuna juhudi za makusudi zinafanywa na ccm kueneza itikadi na sera zake na kuingiza wanachama wapya hasa vijana.Ukifuatilia mkutano wa ndani au wa nje wowote wa ccm, press conference, press release n.k. utashangaa kuona vyama vya upinzani hususani CDM kimetajwa mara nyingi na viongozi wa ccm kuliko CCM yenyewe. Na pale ambapo wamejaribu kufanya, wameishia ama kuvisema vyama vya upinzani na sio kueleza sera za ccm na namna ambavyo zinasaidia kutatua kero za wananchi. Waliviita kuwa ni 'vyama vya msimu' uchaguzi ukiisha vitatoweka, sasa ni karibu miaka 3 tangu uchaguzi mkuu ufanyike, lakini bado viko ulingoni na vinawanyanyasa kweli kweli.
 
labda waanzishe ccj inaweza kushindana na cdm lakin chama cha chukua chako mapema itakua ngumu
 
Uko sahihi kabisa. Niliwahi kusema na nitaendelea kusema...tafsiri ya demokrasia ya vyama vingi vya siasa kwa ccm ni 'kudhibiti' au 'kuua' vyama vya upinzani kwa nguvu zake zote. Mzee Mkapa alifanikiwa sana katika hili na kilichofuata ni ccm kubweteka na kuendelea kuamini kuwa njia hiyo ndiyo njia pekee ya kuifanya ccm iendelee kushika hatamu za uongozi. Tulitegemea ziara ya sekretariati ya CCM kule China itakuwa imepata fursa ya kijifunza mbinu mpya, lakini mwenendo wa kampeni za hivi karibuni za ARS na kwingineko ulikofanyika uchaguzi wa madiwani hazijaonyesha mabadiliko yoyote. Ni mbinu zile zile ambazo wananchi wameshazichoka!

Matokeo yake sasa hakuna juhudi za makusudi zinafanywa na ccm kueneza itikadi na sera zake na kuingiza wanachama wapya hasa vijana.Ukifuatilia mkutano wa ndani au wa nje wowote wa ccm, press conference, press release n.k. utashangaa kuona vyama vya upinzani hususani CDM kimetajwa mara nyingi na viongozi wa ccm kuliko CCM yenyewe. Na pale ambapo wamejaribu kufanya, wameishia ama kuvisema vyama vya upinzani na sio kueleza sera za ccm na namna ambavyo zinasaidia kutatua kero za wananchi. Waliviita kuwa ni 'vyama vya msimu' uchaguzi ukiisha vitatoweka, sasa ni karibu miaka 3 tangu uchaguzi mkuu ufanyike, lakini bado viko ulingoni na vinawanyanyasa kweli kweli.

Kimsingi ccm hawajaweza kujifunza kitu kimoja kwamba '' huwezi kutumia mabavu siku zote ukahimili moto wa mabadiliko uliopo kwenye mioyo ya watu''

Unaweza kutawala watu kwa ufanisi kama mioyo yao inakubaliana kwa asilimia kubwa na mfumo wako. Mapinduzi ya nchi huanzishwa na uchovu wa mabavu ulioendeshwa kwa muda mrefu. Psychology ya watu ni kwamba huwa wana limits za kuhimili upuuzi, na kama ukitake it for granted kwamba hiyo tabia ni endelevu, utajishtukia siku moto unawaka na huwezi kuuzima maana ulikuwa unachochewa chini kwa chini kwa muda mrefu.

CCm kuweni makini, kama watu wamewapa ustaarabu kwa muda wote huo mliowatawala jaribuni kuwaheshimu otherwise msije kujutia yaliyowakuta kina Charles Tyler.
 
Hatimaye waziri wa Jk bwana Stephen Wasira kakili kuwa CHADEMA haiwezi kufa kirahisi na CCM wasibweteke na kudhani kitakufa kama walivyopanga huko nyuma na kuwaomba waangalie njia mbadala ikiwemo kumshawishi msajili wa vyama vya siasa kukifuta.

Source Gazeti Jamuhuri

Hivi wakikifuta hakiwezi kuanzishwa kingine? Watatumia ule mtindo wa NBC ilipokabidhiwa kwa wanunuzi from S. Africa. Ofisi zote pamoja na uongozi wa CHADEMA itakayofutwa utaamia chama hicho kipya....Tena nashauri kiitwe CHADEMA 2.0
 

The Invincible,Robot na Mods wote ushauri wangu uliwafikia au mnafurahia hali hii.
Pata picha angewekwa Slaa kafananishwa na Nguruwe, hapa jukwaani Thread hiyo ingekuwa Hai?
Vp kuhusu Ban, angepona mtu huyo?
JF is a CDM wing.
 
Back
Top Bottom