Wassira: CHADEMA kufa ni Ngumu

Wassira: CHADEMA kufa ni Ngumu

Hatimaye waziri wa Jk bwana Stephen Wasira kakili kuwa CHADEMA haiwezi kufa kirahisi na CCM wasibweteke na kudhani kitakufa kama walivyopanga huko nyuma na kuwaomba waangalie njia mbadala ikiwemo kumshawishi msajili wa vyama vya siasa kukifuta.

Source Gazeti Jamuhuri
Ha ha ha hahahahahahahaa,kama ni kweli nimecheka sana.
 
Akili za tope, mawazo na ushauri kama tope.

Wasira na watawala wenzake bado wanaamini Tanzania ni yao na ccm ndiyo yenye HATI-MILIKI ya taifa hili. Ni kwa kuwa hakuna utawala wa sharia na maadili ya viongozi yanaendeshwa kama JAA LA TAKA; kwa kauli zao za hovyo, akina wasira na wenzake ilitakiwa wakamatwe na kushtakiwa kwa uchochezi na kuvuruga amani ya Tanzania.
 
Hadithi ya fisi na mkono wa binadamu kusubiri mkono udondoke.

Cc: CHAMVIGA @fweero
 
Last edited by a moderator:
Wasira anawakilisha mawazo ya viongozi wengi walio ccm, wao wanadhani chama chenye haki ya kutawala nchi hii ni ccm pekee! Mawazo mufilisi kabisa.
 
Si mlikubali mfumo wa vyama vingi, (japo shingo upande). So mzee Wassira vumilia ushindani wa kisasa toka CDM na sio hizo dua za kuku. Kufikiria kukifuta chama ndio mnaharibu zaidi! don't think about it.
 
Nitaendelea kusisitiza kuwa ndani ya magamba hakuna anayejua kuwa ni kwa nini chama chao kinafanya blanda, Hivi demokrasia ni kufuta vyama vya upinzani, siasa za hawa majamaa bwana.
 
VIVA CHADEMA.muombee adui yako ili aishi cku nyingi ili unapofanikiwa ajionee kwa macho.eeh,mungu baba wa mbinguni naomba usimchukue mapema steven wassira ili aone chadema inavyoingia ikulu "AMEN"
 
Hivi demokrasia ni kuviua vyama vya upinzani au kutangaza sera madhubuti....
watu8 hebu fikiria hivi....ili Barcelona iwe bingwa inabidi izihujumu timu zingine.

Kwa mazingira hayo Barcelona ni bingwa kwa vile ni timu bora au bingwa kwa vile timu pinzani zinahujumiwa...

CCM is like a HEAVY weight boxer always wanting to stage a fight against feather weight amateur boxers!!
 
Last edited by a moderator:
Ritz, Simiyu yetu, HAMY-D, bungeni. Nadhani mmepata taarifa kwamba mzee wenu amekiri kwamba haiwezekani kukisambaratisha CHADEMA hivyo tafuteni namna mpya ya kufanya siasa lakini kwa mfumo huu wa siasa zenu uchwara mnakiangamiza Chama Cha Mapinduzi.
Kama tulivyowapa muda na sasa kuanza kukiri hadharani kwamba chama dume hawakiwezi kukiua, basi tuendelee kuwapa muda hivyo hivyo kwani si muda mrefu watakuja wenyewe kukiri kwamba 2015, Ikulu ni itakuwa ikiongozwa na Akili kubwa
 
Huyu zee la nyani la Gombe si alisema kuwa CHADEMA itakuwa imekufa na kupotea katika miaka 2 ijayo?
Sasa baada ya mikakati yake akisaidiana na kina Mchembe,Polisiccm na Usalama wa Taifa wamegundua kuwa CHADEMA ni maji marefu.

Ifuatayo ni mikakati iliyoshindwa ya Wassira na Magamba wenzake:

  1. Wamejaribu kutengeneza video fake zimeshindwa
  2. Wametunga kesi za kubambikiza kwa Viongozi na Wanachadema zimekwama.
  3. Wamejaribu kufuta au kutengua Ubunge wa baadhi ya Wabunge wa CHADEMA wameshindwa.
  4. Wameteka waandishi wa Habari na Viongozi wa Madaktari wameshindwa.
  5. Wamemwua mwandishi wa Ch.10 Daudi Mwangosi wakashindwa.
  6. Wameua watu kwenye mikutano na maandamano ya CHADEMA bado wameshindwa.
  7. Wamechochea udini,ukabila na itikadi wameshindwa.
  8. Wametumia Bomu la Kivita la kutupa na mkono kwenye mkutano wa kampeni wa CHADEMA pale Soweto na kutaka kumwuua Mwenyekiti Taifa na Mbunge A Town bado wakashindwa.

Sasa wanataka kumtumia kiranja wao Mkuu John Tendwa aifute CHADEMA kwa sababu dhaifu kabisa ati ya kutaka kuanzisha vikundi vya ukakamazu na ulinzi shirikishi ndani ya CHADEMA. Vikundi kama hivi vipo hata ndani ya CCM na jamaa zao wa CUF lakini Tendwa amenyamaza kimya!!!

Nataka tu nimshauri Tendwa ushauri wa bure kabisa kuwa Watanzania ni wapole sana na waungwana sana.Watanzania ni wavumilivu na wastahimivu sana. Watanzania ni wapenda amani. Lakini kwa namna Serikali ya CCM inavyotawala(siyo kuongoza) kwa sasa Watanzania hawahawa wenye sifa nilizozitaja hapo mwanzo wanabadilika kidogokidogo! Kama Tendwa ana macho ya kutazama na aone sasa, kama Tendwa ana masikio ya kusikia na asikie sasa. Kwamba Watanzania wameshachoka na siasa za CCM za kutaka kuwaburuza Watanzania kama vile hawana akili.

Namsihi Tendwa akae,atafakari na aone kama ana macho kile kilichotukia Arusha kwenye Bomu la Soweto na mrejesho wa hisia za Wana Arusha kwenye matokeo ya Chaguzi za Kata 4 za Udiwani hapo Arusha. Kama ana macho ya kuona na aone sasa.

Lakini pia namsihi Tendwa akae na atafakuri kile kilichotokea Mtwara kuhusu Gesi asilia na kinachoendelea kufukuta chini kwa chini hukohuko Mtwara kwa sasa.Bila shaka amesikia na kama hajaona basi afike Mtwara ajionee mwenyewe uhalisia na mambo asingoje kusimuliwa.

Akisha tafakari yote haya sasa ndipo apime na aone kama itakuwa ni busara kwake kuifuta CHADEMA kwenye daftari lake la kuandikisha vyama. Kama hana akili na busara za kutafakuri basi aendelee na mpango wake na hao magamba wenzake kuifuta CHADEMA ambao bila shaka kwao ni mpango PLAN B au C. Tendwa atangaze hata kukifuta leo halafu aone nini kitafanyika nchi nzima.Kama ana simu ya Mohamed Morsi wa Misri ampigie amwulize nini walichofanya Wamisri kwa serikali yake!

Na ndipo Tendwa atakapojua kwamba hupashwi kuchezea nguvu ya Wananchi(Umma) kwa namna yoyote ile.
 
kama siasa ya vyama vingi haikuhitajika Tanzania,ilikuwaje waliikubali? tuwaache wanachi waendeee kufanya maamuzi na kuchagua wakitakacho/wakipendacho.
 
Na bado mpaka watakubali tu kama chadema siyo chama cha mchezo mchozo na mzaha mzaha
 
Hatimaye waziri wa Jk bwana Stephen Wasira kakili kuwa CHADEMA haiwezi kufa kirahisi na CCM wasibweteke na kudhani kitakufa kama walivyopanga huko nyuma na kuwaomba waangalie njia mbadala ikiwemo kumshawishi msajili wa vyama vya siasa kukifuta.

Source Gazeti Jamuhuri


Hizi ni fikra za Watawala ,nnaisikitikia nchi yangu na viongozi tulio nao kwa kauli zao za kipumbav....u kabisa.
 
Back
Top Bottom