Tumezoea kusikia matamko kutoka kwa mabinti kama vike
kazi ndiyo mume wangu,
mume si lazima ninaweza kuzaa nikalea mwenyewe,
kuolewa siyo lazima,
kuishi single ndo maisha niliyoamua, n.k
Mi nafikiri wasichana wengi hudanganywa na umri kwamba walivyo wataendelea kuwa on demand ya wanaume na hivyo wakihitaji mume watampata. Ya nini kuwa chini ya mtu mwingine.Kumbe hawajui umri unavyosogea waliokuwa wakikupapatikia nao wanaendelea kupungua.
Wengine wameamua kuzaa aidha kwa bahati mbaya au kwa sababu nilizoeleza hapo awali. Lakini kauli ya "mwanaume nini bwana" imekuwa ikisikika sana vinywani mwao. Sasa sijui hutoa kauli za namna hiyo kwasababu ya kukosa, kuumizwa au kiukweli kutoka rohoni. Na wakishazalishwa watoto pengine zaidi ya mmoja utasikia wanatafuta mwanaume aliye BORA wakililia upweke.
Kilichonifanya niandike huu uzi ni case ya Snura ambayo iko kwenye gazeti la jana la Risasi. Nimeimbatanisha na uzi huu. Hili tatizo ni la Snura lakini naamini kwamba mawazo yake yanawakilisha wanawake walio wengi ambao wako kweny hali aliyo nayo. Swali ni je wanawake huwa wanajua kwamba haya matamko ni ya ujana? Je wanajua consequnces ya kuwa single mother pamoja na kwamba utakuwa unajiweza kiuchumi? Nimeleta hii labda inaweza kubadili mitizamo ya mabinti wengi wanaodanganywa na wakati bila kuona mbele wanapokwenda.
Unaweza kuwa na mawazo ya kutoolewa. Swali je hutakuwa na mwanaume wa kukutimizia haja zako? Kama unamhitaji utapandwa na wangapi? Maana itafika wakati kila mwanaume anayetaka anakuja kwako kama kipozeo.
Nimeiweka humu kwa maoni yenu wana jf ili isaide kupanua mawazo jinsi mahusiano tunavyoyachukulia.karibuni.
View attachment 440211