P Didy Wa Tanzania
JF-Expert Member
- May 6, 2022
- 2,376
- 3,891
Kila mtu anajua leo hii kuwa Wasafi Tv na Wasafi FM ndiyo media ambayo zimepata nguvu ya kushabikiwa kwa muda mfupi na kupata watazamaji na wasikilizaji wengi.
Huenda labda ushawishi huo umekuja kwa sababu ya bosi wao Diamond platnumz kuipiga chapuo media hiyo lakini kuna kitu naona kabisa kimepungu pale Wasafi Media, na kama kila siku hii Wasafi Media itatagemea chapuo kwa kumuongelea Diamond platnumz na Zuchu kila siku.
Basi ipo siku hii media itaenda kufa na nafasi yake itachukuliwa na media nyingine kama media hii haitobadilika.
Wasafi Media inamuitaji mtu wenye ubunifu kama Jonijoo, walitakiwa kutumia nguvu ya kila namna kumzuia Jonijoo asiondoke ili kutengeneza vijana sahihi ambao walitakiwa kupata madini kutoka kwa Jonijoo. Kama wanavyofanya East Africa Radio kwa Dulla Planet na wale wadada.
Lakini kuondoka kwa Jonijoo na kumleta Lil Ommy naona kwangu haijakaa sawa. Jonijoo mmoja alikuwa anasimama kwenye The Bar Tender na msanii wake mmoja tu anafanya naye mahojiano wewe mtazamaji huku hautamani kipindi kiishe, hamlazimishi mtu kujibu maswali ila amamuuliza mtu maswali ambayo siyo mtazamaji wala siyo msanii ambaye alitegemea ataulizwa hilo swali.
Lakini leo hii kwenye wasafi TV kwenye Big Sunday Live Show unakutana na Lil Ommy, Ray Mshana na Ammy girl, wasanii zaidi ya watatu lakini kinachoendelea kwenye kipindi hakieleweki na wala hakina mvuto.
Raia tulikuwa tunafurahia mahojiano na Jonijoo pale Block 89, Jonijoo, Liyaah Naa mtu imara, tulikuwa tunafurahia kuwasikiliza. Unaweza ukawapotezea XXL B Dozen, Adam Mchomvu na Mamy Baby kule Clouds, leo hii Wasafi FM hakuna linaloeleweka, kelele tu na umarekani mwingi.
Kipindi The Story Book kinaanza watu tulikuwa tunafurahia maandiko ya Jamal April na masimulizi ya Mtiga Abdallah, lakini leo hii kipindi hakina mvuto kivile, naona kazi mbili kapewa mtu mmoja. Anayeandika ndiyo huyo huyo na anasimulia kwa njia ya sauti ni huyo huyo.
Ujumbe kwa Wasafi Media, inatakiwa kuwa makini sana, watu wanalalamika Wasafi haina maudhui kabisa zaidi ya umbea na kuongelea ngono kwa sana basi, ndiyo maana kila siku wanapigwa na rungu la TCRA.
Wanaopewa 'headlines' ni wale ambao hawana ubunifu kabisa.
Sasa Wasafi FM na Wasafi Tv kuweni makini msije mkampoteza Edo Kumwembe na George Ambagile.
Huenda labda ushawishi huo umekuja kwa sababu ya bosi wao Diamond platnumz kuipiga chapuo media hiyo lakini kuna kitu naona kabisa kimepungu pale Wasafi Media, na kama kila siku hii Wasafi Media itatagemea chapuo kwa kumuongelea Diamond platnumz na Zuchu kila siku.
Basi ipo siku hii media itaenda kufa na nafasi yake itachukuliwa na media nyingine kama media hii haitobadilika.
Wasafi Media inamuitaji mtu wenye ubunifu kama Jonijoo, walitakiwa kutumia nguvu ya kila namna kumzuia Jonijoo asiondoke ili kutengeneza vijana sahihi ambao walitakiwa kupata madini kutoka kwa Jonijoo. Kama wanavyofanya East Africa Radio kwa Dulla Planet na wale wadada.
Lakini kuondoka kwa Jonijoo na kumleta Lil Ommy naona kwangu haijakaa sawa. Jonijoo mmoja alikuwa anasimama kwenye The Bar Tender na msanii wake mmoja tu anafanya naye mahojiano wewe mtazamaji huku hautamani kipindi kiishe, hamlazimishi mtu kujibu maswali ila amamuuliza mtu maswali ambayo siyo mtazamaji wala siyo msanii ambaye alitegemea ataulizwa hilo swali.
Lakini leo hii kwenye wasafi TV kwenye Big Sunday Live Show unakutana na Lil Ommy, Ray Mshana na Ammy girl, wasanii zaidi ya watatu lakini kinachoendelea kwenye kipindi hakieleweki na wala hakina mvuto.
Raia tulikuwa tunafurahia mahojiano na Jonijoo pale Block 89, Jonijoo, Liyaah Naa mtu imara, tulikuwa tunafurahia kuwasikiliza. Unaweza ukawapotezea XXL B Dozen, Adam Mchomvu na Mamy Baby kule Clouds, leo hii Wasafi FM hakuna linaloeleweka, kelele tu na umarekani mwingi.
Kipindi The Story Book kinaanza watu tulikuwa tunafurahia maandiko ya Jamal April na masimulizi ya Mtiga Abdallah, lakini leo hii kipindi hakina mvuto kivile, naona kazi mbili kapewa mtu mmoja. Anayeandika ndiyo huyo huyo na anasimulia kwa njia ya sauti ni huyo huyo.
Ujumbe kwa Wasafi Media, inatakiwa kuwa makini sana, watu wanalalamika Wasafi haina maudhui kabisa zaidi ya umbea na kuongelea ngono kwa sana basi, ndiyo maana kila siku wanapigwa na rungu la TCRA.
Wanaopewa 'headlines' ni wale ambao hawana ubunifu kabisa.
Sasa Wasafi FM na Wasafi Tv kuweni makini msije mkampoteza Edo Kumwembe na George Ambagile.