Warioba: Mimi na Salim urais basi

Warioba: Mimi na Salim urais basi

Atuongoze bila kututawala, inawezekana, mbona hili la katiba ametuongoza bila kuwa rais??? hazina za taifa ni mtu kama warioba, malecela, lowasa ni deni la taifa
 
Ndugu zangu Kusema Kweli, huyu Mzee Jaji Joseph Warioba ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Mpya, ametokea Kuwa Kiongozi wa tatu Baada ya Dr.Slaa na Mhe.Mbowe, Kunivutia sana hasa Kwa Misimamo yao ya Kiutendaji pale Wanaposimamia Kile Wanachokiamini Kwa niaba ya wengi. Jaji Warioba licha ya Kuwa Kada na Mwanachama wa CCM, ameuonyesha Dhahiri Ukomavu wake wa Kisiasa Katika Kujenga, Kutetea na Kusimamia hoja zake zenye Maslahi Kwa Taifa letu Kwa Ujumla bila Kuelemea Upande wowote.

Jaji Warioba pamoja na Kukumbana na Shinikizo Kubwa Kutoka Upande wa Chama Chake, tena Shinikizo linaloambatana na Matusi, Kebehi, Dharau, Udharirishwaji n.k, Lakini Jaji Warioba anaendelea Kuwa Jasiri Kila Kukicha Katika Kutetea hoja za Wanyonge wa Taifa hili na Kubeba Mzigo wa Lawama zote Inazotupiwa Tume anayoiongoza, Ilimradi Kile anachoamini Kimeelezwa na Watanzania, Kiwasilishwe Bungeni. Mzee Warioba ni Mtu wa Pili baada ya Dr.Slaa, anayeweza Kugombea Urais 2015 Kwa Sababu ya Hekima, na Busara zake Kama za Mwl.Nyerere.
rais 2015 ambae watanzania twamuhitaji ni Prof. Ann Tibaijuka tu
 
HOngera kamanda Francis, mi ninadhani kwa suala la Katiba Jaji Warioba amefanya vizuri sana. lakini sina uhakika kama anaweza kufanya vizuri kufanya kazi katika Utawala wa juu. Binafsi namkubali sana Sinde Warioba Joseph, lakini bado nashindwa kumpa kura zangu zote hasa unapomshindanisha na mtu kama DR. SLAA hivi. BIG UP KAMANDA FRANCIS yangu kwa SLAA THEN YA PILI KWA WARIOBA
 
KWA UJUMLA CHAMA CHOCHOTE KITAKACHOMSIMAMISHA JAJI JOSEPH WARIOBA KINAWEZA KISISHINDE UCHAGUZI LAKINI NINA UHAKIKA KITAPATA KURA NYINGI SANA ZA KUTOSHA KUKIKENDESHA KWA MIAKA MITANO BILA SHIDA
warioba, Makamau wake ni aliyekuwa mwanasheria mkuu wa Zanzibar Othman Masoud Othman, timu hiyo inaweza kuzoa kura nyingi sana bara na visiwani.alafu waziri mkuu mteuliwa awe Zito kabwe. itakuwa Serikali inayofahamikama kwa kiasi kikubwa kuwahi kushika madaraka katika nchi hii. ACT MPOOOOOO!!!!!!!!!!!!!!
 
Ukiwa pro Chadema akili yako inawaza matukio tu.Sasa Warioba karne hii atamchagua nani? au katika utumishi wake wa uwaziri mkuu alifanya jema lipi la kumkumbuka?
 
Ukiwa pro Chadema akili yako inawaza matukio tu.Sasa Warioba karne hii atamchagua nani? au katika utumishi wake wa uwaziri mkuu alifanya jema lipi la kumkumbuka?
Alikuwa mmoja wapo wa wahunzi wakuu wa katiba tunayoitumia sasa,Aliwahi kuwa mwenyekiti wa Taasisi ya Kimataifa iliyopo chini ya UN inayojihusisha na masuala ya kikatiba na kisheria kwa nchi wanachama.Tupatie wasifu wa Chenge na Sitta.
 
Alikuwa mmoja wapo wa wahunzi wakuu wa katiba tunayoitumia sasa,Aliwahi kuwa mwenyekiti wa Taasisi ya Kimataifa iliyopo chini ya UN inayojihusisha na masuala ya kikatiba na kisheria kwa nchi wanachama.Tupatie wasifu wa Chenge na Sitta.

Huu si wakati wake
 
Inakubalika kabisa iwapo mikakati na mipango itawekwa barabara. Ila haya nina hakika nayo kwa zaidi ya 1500%, kwamba;


  1. Ataondoka na kundi kubwa sana la wana CCM ambao ni waadilifu na wanaoitaka na kuipenda Tanganyika yao (kwa sababu ndani ya CCM siyo wote waovu na kuwa wameoza)...............Hili litakuwa pigo la pili kwa CCM baada ya pigo la kwanza la kutupa Rasimu ya pili ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba (iliyotokana na maoni ya wananchi wenyewe ambao ndiyo wenye Katiba) iliyoongozwa na Jaji huyu, Joseph Sinde Warioba
  2. Wataendesha kampeni yao kwa matusi na kashfa dhidi ya mzee huyu (kama tu walivyomtusi kwa kila aina ya tusi na kashfa katika mkutano wao mkuu wa Dodoma waliokaa kwa kisingizio cha eti wako kisheria na wanatengeneza Katiba) na hili ndilo litakuwa pigo la tatu na la mwisho la kuilaza kaburini CCM hii maskini!!

Honestly, nikubaliane na wewe kuwa wakicheza vizuri karata zao na wakati huohuo kujifunza kwa makosa ya wakati ule kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 1995 pale Mrema Augustino Lyatonga alipochomoka kutoka CCM na kuingia Upinzani, alitikisa na asingekuwa Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pamoja na ujinga, woga na matumizi makubwa ya nguvu za dola + uchanga wa siasa za upinzani wakati huo, wallahi tena Mkapa Benjamini William asingekuwa Rais wa Tanzania wakati ule, sembuse leo na miaka hii ya kizazi hiki cha dot.com, kilichozibuka na kuzifahamu haki zao na mamlaka waliyonayo juu ya uendeshaji wa nchi yao!!????.................Oooh, I really don't get it!!

Pia ni lazima tujue kuwa inawezekana kuwa ule utabiri wa Marehemu baba wa Taifa Mwl J.K. Nyerere "kuwa upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM" na kuupa nguvu upinzani wa sasa chini ya kina Mbowe, Mbatia, Lipumba, Rev. Mtikila na wengine wale halisi (na si kina Cheyo, Mrema, Dovutwa Fahmi & their Co) sasa ni wakati wake kujidhihiri. And personally, I am very optimistic kuwa anaweza asiwe hata Jaji Joseph Warioba..............kwani kwa sakata hili la Katiba ya kisanii iliyoasisiwa na Masanii Jakaya Kikwete, litakuja na maajabu tusiyo yatarajia!!
 
Nakumbuka alikuwa waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais pekee niliyesalimiana naye kwa kushikana mikono.
 
warioba hana sifa hata moja ya kuwa rais wa taifa hili kutokana na unafika na ubinafsi alionao pia ni ambaye sio result oriented mi naona kama mnataka awe rais naomba mmshauri aende TFF akagombee urais huko maana kule kuna migogoro ya akina malinzi na ndumbaru
 
warioba hana sifa hata moja ya kuwa rais wa taifa hili kutokana na unafika na ubinafsi alionao pia ni ambaye sio result oriented mi naona kama mnataka awe rais naomba mmshauri aende TFF akagombee urais huko maana kule kuna migogoro ya akina malinzi na ndumbaru

1413650096932.jpg
 
Huyu mzee anastahili kuwa rais kutokana na kutetea madlsji ya wananchi. Tatizo naliliona mi umri wake kwa sasa ni mkubwa. Nafikiri atakuwa mshauri mxuri wa Slaa pindi CHADEMA ikitupatia uhuru wetu.
 
Nchi yenye watu corrupt kama hii anayeiweza ni mtu asiyeogopa nyuso za watu kama Mwigulu, na chama kinachoweza ni ccm kama inaweza kuacha ufisadi, dhuruma kwa wananchi kwa kisingizio cha maabara, ulafi na wizi mfano posho za bunge la katiba, u-Vasco da Gama, rushwa hasa kipindi cha uchaguzi, ubabe, ulaghai au u-Karl Peters, na uozo mwingine mwingi.
 
Utakuwa umenunua vyeti,ndio maana hujiamini mpaka ujisifie mwemyewe eti umesoma.Matendo na tabia ndio hutoa picha kamili ya msomi.Uchangiaji wako umedhihirisha kuwa wewe huna hicho ulichoingia nacho humu

Binafsi sina tatizo na kazi nzuri aliyoyafanya jaji Warioba katika mchakato wa katiba mpya japo Kama zilivyo kazi zingine za wanadamu mapungufu hayakosekani.

Ila nikimlinganisha na majaji wengine waliyowahi kuongoza Tume za mabadiliko ya katiba Kama jaji Nyalali na Kisanga nagundua tofauti za msingi. Huwenda tofauti hizi zinatokana na ukweli kwamba waliomtangulia hawakuwa politicians .

Utaona kwamba japo maendekezo mengi ya msingi katika repoti zao ambayo yamechukua nafasi kubwa pia katika ripoti ya Warioba hayakuzingatiwa katika mabadiliko ya katiba lakini sikuwasikia hata siku moja wakipaza Sauti kulalamika kwa nini yaliachwa. Bila Shaka wailiwaachia wananchi wenye wenye mawazo yao kuzungumza.
 
Back
Top Bottom