Warioba: Mimi na Salim urais basi

Warioba: Mimi na Salim urais basi

Binafsi sina tatizo na kazi nzuri aliyoyafanya jaji Warioba katika mchakato wa katiba mpya japo Kama zilivyo kazi zingine za wanadamu mapungufu hayakosekani.

Ila nikimlinganisha na majaji wengine waliyowahi kuongoza Tume za mabadiliko ya katiba Kama jaji Nyalali na Kisanga nagundua tofauti za msingi. Huwenda tofauti hizi zinatokana na ukweli kwamba waliomtangulia hawakuwa politicians .

Utaona kwamba japo maendekezo mengi ya msingi katika repoti zao ambayo yamechukua nafasi kubwa pia katika ripoti ya Warioba hayakuzingatiwa katika mabadiliko ya katiba lakini sikuwasikia hata siku moja wakipaza Sauti kulalamika kwa nini yaliachwa. Bila Shaka wailiwaachia wananchi wenye wenye mawazo yao kuzungumza.
Kati ya hao kuna hata mmoja aliyetumwa kuandika rasimu ya Katiba ya nchi kama Jaji Warioba?
 
Binafsi sina tatizo na kazi nzuri aliyoyafanya jaji Warioba katika mchakato wa katiba mpya japo Kama zilivyo kazi zingine za wanadamu mapungufu hayakosekani.

Ila nikimlinganisha na majaji wengine waliyowahi kuongoza Tume za mabadiliko ya katiba Kama jaji Nyalali na Kisanga nagundua tofauti za msingi. Huwenda tofauti hizi zinatokana na ukweli kwamba waliomtangulia hawakuwa politicians .

Utaona kwamba japo maendekezo mengi ya msingi katika repoti zao ambayo yamechukua nafasi kubwa pia katika ripoti ya Warioba hayakuzingatiwa katika mabadiliko ya katiba lakini sikuwasikia hata siku moja wakipaza Sauti kulalamika kwa nini yaliachwa. Bila Shaka wailiwaachia wananchi wenye wenye mawazo yao kuzungumza.

So u wanted mtu ambaye atakaa kimya tu hata kama ukweli utakuwa unapindishwa siyo? To me this Mzee is my hero! Hakutaka kuwa mnafiki,amesimamia kile anachokiona kuwa ndio ukweli.
 
Mimi ni msomi tena sana katika maswala ya science. Nimebahatika kupata Kazi nzuri kiasi kuniwezesha kuwa na DSTV.

Vipindi ni vingi ila napenda habari za nje ya nchi.

Nimefuatilia sana Katiba ya Kenya pia nchi mbalimbali, muungano wetu ni mzuri sana na una maadui wengi ila serikali tatu ni kuvunja Muungano. Je Warioba ana hila gani na hii nchi?

Rasimu ya Katiba ilapaswa kubadilishwa kuendana na mahitaji ya kisiasa ya sasa waryoba alitaka wabunge wafanyeje?

Najua CCM haijawahi kumpitisha waziri Mkuu yoyote Kugombea Urais.

Je atagombea upinzani?

Dah,haya kama ni swala la Dstv na mimi nina Exprola decoder,lakini huu ujinga wa CCM ni big No! Nyie vipi mbona hamkubaliani na mawanzo kinzani?
 
Nimekuwa nikiona yanayoendelea katika nchi hii yanatokea kama kiini macho, mazingaombwe au songombingo. Lakini jana baada ya hotuba ile pale Ubungo plaza nimeamini tunaweza kupata rais makini mwaka 2015. Kwanini tunaendelea kuwajadili hawa: Lowassa, Mwigulu, Makamba Pinda na hata Kigwangala? huenda wanaweza kuwa rais!!!. Kuna list nyingine ya watu makini pia, nao tuwajadili huenda hatujachelewa. Unajua hata Kikwete alianza kitambo..enzi za mwalimu! akaambiwa asubiri hatimaye tukazoea kumsikia mwishowe akawa rais na sasa anamaliza muda wake. Kama mtaendelea kuficha majina ya wagombea makini basi hii nchi itakuja kuangukia mikononi mwa wahuni ambao Mwalimu Nyerere aliwataja. Kama mti wenye matunda mazuri haushi kurushiwa mawe basi ona hii:
View attachment 198678
 
Laiti ingekuwa ukiingia kwenye thread unalipia ningedai kurudishiwa pesa yangu.Huu ni upuuzi
 
Mingoi wewe uliwahi kutoa thread ya maana lini japo tulipie hata shilingi 10?
 
Last edited by a moderator:
Mh. Jaji sinde wariba




Tukiwa tumebakisha miaka takribani mmoja, taifa
letu liingie tena katika mchakato wa uchaguzi wa
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na
Uchaguzi wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar; nafikiri ni wakati muuafaka sasa wa
kuanza kufikiri viongozi wa namna gani
wanahitajika katika taifa letu hasa wakati huu
ambapo nchi yetu ipo katika mawimbi ya
mabadiliko ya fikra hasa kutoka mabadiliko
makubwa ya Katiba katika historia ya Taifa letu.
Ni matarajio yetu kuwa uchaguzi wa mwaka 2015
pengine utakuwa na historaia ya pekee; upekee
wa uchaguzi huu ni matarajio ya wananchi wengi
kuwa uchaguzi huu utafanyika katika kipindi
ambacho taifa litakuwa limekwisha pata Katiba
yake mpya;
swali ambalo tuanalojiuliza sasa ni je Katiba hiyo
itakuwa imekizi matakwa ya Taifa ambalo linataka
kusonga mbele kimaendeleo?
Kama taifa litakuwa limefanikiwa kupata Katiba
bora basi hatuna budi tupate viongozi ambao kwa
kweli nao watakuwa bora katika kuongoza Taifa
letu kuelekea kwenye maisha bora kwa kila
mtanzania. Ni ukweli ambao haupindiki kuwa
Katiba bora ni msingi wa maendeleo ya nchi
kwani ni msaafa wa sheria na kanuni sahihi
kufuatwa na itamlazimisha kiongozi kuongoza
kwa uwajibikaji; kuonyesha uzalendo na kuwa
mfano bora kwa viongozi wengine.
Pengine katika msingi huu tutahitaji kiongozi
ambaye anauelewa mpana wa kuielewa Katiba ili
aweze kuisimamia kwa dhati kabisa; tutahitaji
viongozi wenye UWEZO wa kufikiri kwa usahihi,
kuamua kwa usahihi na kutenda kwa usahihi
wakitambua dhamana ya uongozi ambao taifa
linawapa. Kwa hivyo tutahitaji RAIS pamoja na
mambo mengine awe na UWEZO kuongoza kwa
usahihi.
Vile vile tunahitaji viongozi wajao katika serikali
zetu mbili wawe ni watu wa WATU; viongozi
ambao wataweza kuona matatizo ya wananchi
wao ni yao na yanawakera wanawanyima usingizi,
yana wafanya waongeze nguvu ya uwajibikaji wa
kusimamia rasilimali za Taifa. Nasi kama
wananchi tuwe na uwezo wa kuwapima kwa
watakacho kifanya wakiwa madarakani.
Pengine tutahitaji kidogo aina ya viongozi wetu
wawe wakali japo sio sahihi katika nchi ya
kidemokrasia kutumia msemo huu lakini wakati
mwingine ile tuweze kupiga hatua ya maendeleo
tutahitaji viongozi wenye mawazo ya kidikteta ili
tuweze kubadilisha kidogo maadili ya utendaji
kwa Watanzania hasa viongozi wetu katika
mawizara na idara zake:Tunahitaji Maraisi katika
serikali zetu mbili ambao wanaweza
kuwawajibisha mara moja watendaji wake ambao
wanashindwa kuwajibika, tuwapate viongozi
ambao wanaweka pembeni huruma na urafiki
ambao hauna faida kwa Taifa;
Nafikiri itakuwa ni jambo la busara kama sisi
kama watanzania na wapiga kura tukiweza
kuepuka tabia ya kuwachagua viongozi wetu kwa
Mazoea, Mkumbo na kwa kutumia Hisia na
mapenzi binafsi juu ya wagombea. Nafikiri umefika
wakati tuwachagua viongozi wetu kwa upeo wao
wa kuona mambo mbalimbali nauwezo wao wa
uongozi hapa nazungumzia uzoefu wa kiongozi
kabla ya kuchaguliwa kuwa rais je amefanikiwa
kwa kiasi gani katika idara ambayo amewahi
kuongoza?
kama taifa tunafahamu kuwa taifa letu bado
linaogelea sana katika tope nzito la matumizi
mabaya ya rasilimali ya Taifa Rushwa na Ufisadi
basi tunahitaji Rais ambaye analiona hili kuwa
Lazima tukubali kuwa mabadiliko yoyote ya
kisiasa, kijamii na kiuchumi yenye kulenga
kuletea faida wananchi walio wengi hayawezi
kufanikiwa bila ya kutokomeza rushwa na ufisadi.
Kiongozi wetu aweze kuliona hili na kuwa tayari
kupambana nalo akiamini kuwa Tanzania yetu
tatizo la rushwa limeshaota mizizi:Watanzania
wengi kwa mamilioni wamepoteza matumaini na
hali zao za maisha lakini Maraisi wetu wapya
watakuwa tayari kulitatua tatizo hili na
kuwachukulia sheria wale wote ambao
wamehusika katika uchafu huu,
Tunahitaji vile vile kiongozi ambaye ataweza
kuyatekeleza kwa vitendo manemo haya ya
Mheshimiwa Yusuph Makamba "maendeleo ya
Watanzania yataletwa na wao wenyewe, kwa
kufanya kazi. Watanzania wamekuwa wavivu wa
kufanya kazi na kwamba kila kitu wanategemea
kitafanywa na serikali … Watanzania wataendelea
kulia umaskini kwa kuwa hatuna tabia ya
kushirikiana na kufanya kazi," . Kauli hii ni nzito
kiongozi wetu anayetaka kuongoza taifa hili
lazima awe kuwahamasisha wananchi bila
kuogopa kwa kuwaeleza ukweli huu bila kuogopa
kukosa kura katika kipindi kingine cha uchaguzi.
Daima tunapofikiria kuwachagua viongozi wa juu
wa Taifa letu tunayakumbuka maneno ya Baba wa
Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi sema kuwa kazi
ya urais ni ngumu na inahitaji busara na kuchukua
maamuzi magumu, ili kuweza kutimiza haki
wananchi wanyonge " walala hoi "; aliendelea
kushauri kuwa "Ole wale wanaokimbilia Ikulu,
wanakimbilia nini, Ikulu hakuna biashara ya
kufanya, Ikulu ni mahali patakatifu na kama kuna
mtu anadhani kuwa kukaa Ikulu ni raha basi
angeniuliza mimi katika kipindi cha miaka 21
niliyokaa Ikulu nimefanya biashara gani,Ikulu ni
mzigo mzito"
Mwandishi Nyenyembe aliwahi andika kuwa "Kwa
maana hiyo mtu anapoamua kuulilia urais,urais sio
pambo la nchi,urais ni jalala, urais ni chumba cha
kuhifadhia maiti,urais ni njaa,urais ni
magonjwa,urais ni bakuli la kukingia machozi ya
watu wanyonge wanaolia kila siku wakihitaji
msaada na kama hawapati anayetazamwa hapo ni
rais"
 

POSTED BY TANZANIA CLASSIC ON 12:31 AM |

dk_24d53.jpg


Dar es Salaam. Waziri Mkuu mstaafu, Dk Salim Ahmed Salim amesema hana mpango na hafikirii tena kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili nyumbani kwake Masaki, Dar es Salaam jana, Dk Salim alisema alipowania nafasi hiyo mwaka 2005, hakuwa na ufahamu mzuri kuhusu mchakato huo lakini baadaye alibaini kwamba, mbali na rekodi ya utendaji, kuna mambo mengine yanayohitajika katika kinyang'anyiro hicho na kwamba hata watu wanaomfikiria na kutaja jina lake miongoni mwa wanaoweza kuwania tena nafasi hiyo, wanakosea.

"Sifikirii tena, hii ni zamu ya kizazi kingine. Ila nitaendelea kuisaidia nchi yangu katika nyanja mbalimbali kadri ya uwezo wangu," alisema.

Dk Salim ambaye mbali na uwaziri mkuu amewahi kushika nafasi nyingine mbalimbali kitaifa na kimataifa, alisema uzoefu alioupata katika kinyang'anyiro cha urais unatosha.(E.L).


Alipoulizwa kama uzoefu huo ni mbaya au mzuri kwake, alisema ni mchanganyiko.
Dk Salim aliwahi kugombea nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) na kushindwa kutokana na kura ya veto ya Marekani, pia aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), sasa Umoja wa Afrika (AU). Pia aliwahi kuwa Rais wa Bunge Kuu la UN mwaka 1979 na 1980.

Licha ya kujitokeza mara moja kuomba uteuzi wa CCM kuwania urais 2005, nyota yake katika nafasi hiyo ilianza kuwaka tangu mwaka 1985 akiwa Waziri Mkuu pale aliposhindanishwa katika Kamati Kuu ya CCM na aliyekuwa Waziri Mkuu, Rashidi Kawawa pamoja aliyekuwa Makamu wa Rais wakati huo, Ali Hassan Mwinyi ambaye alipitishwa kiitifaki na kushinda kiti hicho.

Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM, Pius Msekwa alisimulia jinsi Mwinyi alivyopita, kwa sababu alikuwa Makamu wa Rais, hivyo wajumbe wa Kamati Kuu walikosa hoja na sababu za kumwacha na kumchukua Waziri Mkuu aliyekuwa chini yake kiitifaki.

"Makamu wa Rais ukimruka maana yake hatoshi, wakaona hawana maelezo hayo, ikabidi wamteue Mwinyi," alisema Msekwa.

Sifa za viongozi

Katika hatua nyingine, Dk Salim alisema kuna umuhimu mkubwa wa kuandaa viongozi hasa mtu anayekwenda kushika nafasi ya urais atakayekwenda sambamba na mahitaji ya kizazi cha sasa alichokiita cha 'dot com'.

"Hapa sizungumzii viongozi wa CCM au wa Chadema au chama kingine, nazungumzia viongozi wa nchi watakaoweza kufanyia kazi matatizo ya Watanzania.

"Ni vizuri viongozi wakaandaliwa, isiwe mtu anaibuka tu anagawa hela halafu anashinda. Anatakiwa mtu atakayeweza kushughulikia matatizo hayo. Watanzania ni wapole na wavumilivu lakini wanazungumza. Hivyo anahitajika kiongozi atakayesikiliza mahitaji yao na kutoa suluhisho, si kutoa ahadi za uongo," alisema. Dk Salim alisema katika kipindi hiki, anahitajika kiongozi atakayekuwa juu ya tofauti za kisiasa, kidini, asili.

"Unajua hapa nchini kama ilivyo mahali pengine, ukiingiza mgawanyiko wa kidini wakati familia nyingi zina watu wa dini tofauti, wote wataathirika."
Viongozi na rushwa

Akizungumzia tatizo la rushwa, Dk Salim alisema ni kubwa na kadri linavyoongezeka, linakuwa adui wa uwajibikaji, demokrasia.

Alisema katika enzi za utumishi wake nje ya nchi, alikuwa akiona rushwa ilivyokithiri katika nchi mbalimbali, lakini hapa nyumbani pakiwa salama hadi akawa anasema Tanzania ina bahati, kauli ambayo hawezi kuisema sasa.

Dk Salim alibainisha kuwa uongozi unaoingia madarakani kwa rushwa hauwezi kuwa mzuri kwa nchi na athari zake zinaonekana hadi ngazi ya chini katika huduma za jamii kama mahakamani, polisi na hospitalini.













 
Salim na Warioba ndio waliobaki wasafi ndani ya CCM lakini umri hauwaruhusu tena! Rais wa awamu ya 5 ni Dr Slaa, wengine wote waliobaki ni makapi tu!
 
Kwa imani yangu binafsi sioni kiongozi yeyote ambaye anaweza kuirudisha nchi katika msitari zaidi ya huyu.

my take;-
*ataweza kukemea uovu kwa 100%
*ataweza kudhibiti uizi na utoroshaji wa fedha zetu nje ya nchi
*atarudisha nidhamu na uadilifu ambao umeshapotea
*atarudisha nyumba za umma walizojigawia
*atarudisha heshima ya mashirika ya umma kama ttcl na mengineyo
 
Wewe IKULU hawaendi wagonjwa na wazee.

Angalia picha ya wakati Kikwete anapewa nchi na alivyo sasa.Alikuwa kijana Akamaliza mzee.

Sasa niambia hao wengine wakipewa Miaka kumi ni wanaingia wazee wanatoka Vikongwe.
 
wewe inaonesha wa siku hizi, hukumuona alivokuwa waziri mkuu ilikuwa ni sheeda
 
Salim na Warioba ndio waliobaki wasafi ndani ya CCM lakini umri hauwaruhusu tena! Rais wa awamu ya 5 ni Dr Slaa, wengine wote waliobaki ni makapi tu!

Kupenda kweli ugonjwa. Salim ana miaka 73 umri haumruhusu lakini Slaa mwenye 67 ni kijana hiyo reasoning ya wapi .Warioba ana miaka 74 . Tofauti ya umri kati yao ni miaka 6-7.Nipe sababu nyingine hiyo ya umri nashindwa kumesa. Naona wote wazee.Lowassa ana miaka 61 kwa reasoning hiyo ya umri anafaa kuliko Slaa?
 
Back
Top Bottom