Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,933
Hapo kwenye nyekundu naona hujamtendea haki Dr. Salim na sisi wanajamvi, maana sijaona mahali mwandishi kamtuhumu kwa vile ni mwislamu. Kwangu hoja ingekuwa hivi akina Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Slaa, Lipumba, Cheo, nk waliogombea na wengine wakashinda kuwa maraisi walikuwa na CV kubwa kuliko ya Salim? Labda tumtoe Nyerere kwa kwenda UN na kueleza kuwa tunahitaji kujitawala nchi ikiwa na wenye degree wasiofika kumi labda huu ulikuwa ujasiri. Lakini wengine hawa, sijaona kilichowafanya wawe wagombea tofauti na yeye Salim. Sidhani kama kuwa karibu na wananchi ni kigezo cha kuwa kiongozi bora hata kama kuwa karibu nao kunamaanisha kuwaibia na kuwachomolea hata mia tano waliyoweka mifukoni mwao. Pia mimi mbona naona ana ukaribu sana na Nyerere Foundation kama mwenyekiti amekosaje kuwa karibu na wananchi?
Akigombea na kupitishwa na CCM au akihamia chama chochote mi binafsi nitampa kura yangu si kwa sababu ya dini yake, au sura yake (maana mambo ya sura za watu tunaona yalikotufikisha) bali kwa sababu ya weledi wake wa masuala ya kimataifa na kitaifa.
Ningefurahi kuwasaidia kupata uelewa wa hoja yako wachangiaji kama ungezipangua hoja zangu zote hapo juu kujenga utetezi wa kumpa Kura Salim Ahmed Salim. Sijaona hoja ulizojengea utetezi wako, mleta mada ameanika hoja na madhaifu ambayo anaona Salim si hastahili tu bali hafai kuwa rais wa Tanzania.