Warioba: Mimi na Salim urais basi

Warioba: Mimi na Salim urais basi

Babu kazeeka anaitaji kulea wajuku tz tnaitaji rais mwenye nguvu na kijana
 
warioba hajawahi shindwa kesi ya ubunge mahakamani. yeye ndo alimshinda wassira ambaye alikuwa ameshinda uchaguzi wa bunda mwaka 1995 akiwa chama cha nccr mageuzi. mahakama ilimkuta wassira ana hatia ya kutoa rushwa ktk uchaguzi huo na uchaguzi ukatengeuliwa na wassira akazuiwa kugombea ubunge kwa muda wa miaka mitano. jamaa baada ya hapo akajisalimisha ccm. hivyo usichanganye story. warioba is really a man of integrity.

Mzee mchakachuaji wa maoni ya wananchi!
 
Kwa ukweli itakuwa ngumu sana;
Acheni tu apumzike ameshaitumikia TZ vya kutosha.
 
Ni ushabiki wa kipumbavu kwani kuwa mwenyekiti wa kamati lazima uwerais
 
Ni mtu pekee wa ngazi ya juu niliyeshikana naye mkono akiwa waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais
 
[h=2]
icon1.png
Re: Warioba Raisi 2015[/h]Mimi naunga mkono warioba kugombea uraisi lakini si kwa tiketi ya CCM ,kwani mafisadi hawa hawata mpa nafasi.
Ukawa -waseme neno kubwa kuhusu Uraisi,wamshauri warioba ajiunge na chama cha JAHAZI ASILIi,au NLD halafu ukawa wamuunge mkono na awe raisi wa ukawa.
 
Alivuliwa Ubunge na Mahakama kwa Kosa la Rushwa Kesi ilifunguliwa na Wassira, Warioba akiwa Mbunge wa Bunda


Wewe unaonekana hujui hata mambo yaliyotokea jana kuhusu nchi hii.
Nyie ndo mabingwa wa kuharibu historia za watu wema duniani. Hii ni laana kubwa kwa taifa hili.

Unajua enzi za mwalimu Usalama wa taifa walikua wanafanya kazi kikamilifu kwa manufaa makubwa ya taifa.
Mtu kuteuliwa kuwa JAJI halikua ni jambo la kisiasa wala upendelea wa kujaza nafasi tu. Lilikua ni suala zima la uwezo na uadilifu.

Ni ujinga wa hali ya juu na uongo usiokuwa na faida kusema kwamba Jaji Warioba alitoa rushwa kwenye uchaguzi. Labda ni ujinga wa kutokujua au ni maelekezo ya kina Nape na Paul Makonda ambao kipindi hicho walikua hata hawajafikisha umri wa kupiga kura.Enzi zile mtu alikua anaombwa na wananchi na pia Chama ili agombee nafasi ya uongozi.Uongozi halikua suala la fedha na ndivyo anavyoamini Jaji Warioba. Na haamini hivyo kwa sababu ya kutafuta umaarufu bali ni kwa sababu huo ndio ukweli na msingi wa haki katika demokrasia ya kupata viongozi bora.

Serikali mbili au tatu zisiwe ndo mwisho wa kufikiri na kuliangamiza taifa.
Wewe kama unataka umjue Wassira ni nani jaribu kugombea naye kwenye jimbo lake.
 
Waryoba akae apumzike amezeeka awaachie wengine nyadhifa alizopitia alifanya nini? Je, Bunda aliifanyia nini kama wilaya yake? Je, kwao Nyamuswa kuna maendeleo gani aliyowaletea wananchi kwa kipindi chote cha NYERERE, MWINYI, MKAPA na KIKWETE?
 
alifanya kipi cha kukumbukwa wkt alipokuwa prime minister na makamu wa rais.kama alishindwa wkt ule ataweza leo


Kwani Kikwete, Mkapa, Mwinyi na Nyerere wamefanya nini cha maana zaidi yakuiba mali za uma na kukingiana kifua?
 
naomba ukawa wazungumze nae na akikubali tu basi huo ndio utakua mwisho wa laana za ccm
 
Historia inaonesha Warioba amejituma sana kufanya kazi kwa ajili ya taifa hili. Mosi kamati ya raisi aliyoiongoza mwanzoni mwa utawala wa Mkapa kuhusiana na rushwa ilikuwa nzuri sana. Hata hivyo kazi yake ilitupiliwa mbali na hakuna jambo la maana lilifanyiwa kazi. Pia kazi aliyoifanya kwenye kamati ya katiba imetukuka. Amefanya kazi kwa uaminifu na ametoa na kutoa suluhisho litakaloiletea Tanganyika na Tanzania kwa ujumla ustawi mwema. Hata hivyo kazi yake inaonekana kudharauliwa. Hii inanisukuma nione kwamba kuna haja huyu mzee kuwa raisi wa nchi hii ili aweke misingi imara ya nchi yetu.

Raisi wa wasafi
 
Nakubaliana nawe. Warioba ni raisi wa wasafi. Jambo hili likiwezekana ni neema kwetu.
 
Rais 2015 anafaa kuwa Prof. Lipumba .Waziri mkuu ni Dr.Slaa.Makamu wa Rais Duni haji Duni. Rais wa Znz Maalim Seif Sharif.
Wabunge wengi watatoka vyama vya upinzani na CCM itakuwa imekufa kifo cha asili.
 
Back
Top Bottom