Warioba: Mimi na Salim urais basi

Warioba: Mimi na Salim urais basi

Nadhani busara zake zimeonekana katika rasimu aliyoisimamia..

Anakubalika na watu wengi kutokana na mitazamo yake..

Ana uzoefu kiutawala na katika nafasi mbalimbali kitaifa...

Ni hazina tosha kwa taifa..kutokana na uzoefu wake..

Mimi napendekeza achukue fomu kugombea.....nafasi ya Urais , 2015.
 
Anafaa zaidi kuwa mshauri kwani umri umesogea sana. Japo una wazo zuri.
 
Itabidi tuwe wazalendo kwelikweli Warioba gombea uraisi tuokoe wanyonge ww ndie dira thabiti
 
Kwa tiketi ya UKAWA?


Zoezi la kuandika katiba tupende tusipende ni lazima lianze upya na kusimamiwa na viongozi ambao watahakikisha kuwa tunapata katiba itakayokubalika na wananchi waliowengi. Hapa tulipofika sasa ni lazima tutakwenda kwenye uchaguzi mwaka kesho na kutumia katiba ya mwaka 1977 ambayo itakuwa imefanyiwa marekebisho ikiwamo kuruhusu INDEPENDENT CANDIDATES. Kutokana na kuruhusiwa hawa Independent Candidates ndio wangeshauriwa viongozi waadilfu kutoka Bara na visiwani kuchuka form na kugombea URAIS kwa dhumuni la kushinda na baadae kuingia mkataba kuwa wataongoza kwa kipindi cha miaka miwili tu ili kufanikisha uandikishwaji wa KATIBA. Ningependekeza kama utaratibu huu ukiungwa mkono basi tumshawishi Jaji Warioba kutoka bara na Ahmed Salim kutoka visiwani wagombee kiti cha URAIS. Nawasilisha.
 
Mimi ni msomi tena sana katika maswala ya science. Nimebahatika kupata Kazi nzuri kiasi kuniwezesha kuwa na DSTV.

Vipindi ni vingi ila napenda habari za nje ya nchi.

Nimefuatilia sana Katiba ya Kenya pia nchi mbalimbali, muungano wetu ni mzuri sana na una maadui wengi ila serikali tatu ni kuvunja Muungano. Je Warioba ana hila gani na hii nchi?

Rasimu ya Katiba ilapaswa kubadilishwa kuendana na mahitaji ya kisiasa ya sasa waryoba alitaka wabunge wafanyeje?

Najua CCM haijawahi kumpitisha waziri Mkuu yoyote Kugombea Urais.

Je atagombea upinzani?
 
Wewe si msomi, au hujaelimika. Ccm imetokana na Tanu na asp. Nyerere alichaguliwa kuwa rais kutokea kwenye uwaziri mkuu kasome tena historia ya Tanganyika tunayoiomba wananchi (si warioba).
Pia usijifunge kimawazo eti kila anayeipinga rasimu ya ccm anataka urais, au utuambie kama ni vibaya mtu kutaka urais.
Nao wote wanaopinga si viongozi tu, hata wananchi maana imekiuka maoni yetu ikaweka mipango yao ya kutawala zaidi
 
Wewe si msomi, au hujaelimika. Ccm imetokana na Tanu na asp. Nyerere alichaguliwa kuwa rais kutokea kwenye uwaziri mkuu kasome tena historia ya Tanganyika tunayoiomba wananchi (si warioba).
Pia usijifunge kimawazo eti kila anayeipinga rasimu ya ccm anataka urais, au utuambie kama ni vibaya mtu kutaka urais.
Nao wote wanaopinga si viongozi tu, hata wananchi maana imekiuka maoni yetu ikaweka mipango yao ya kutawala zaidi

Niambie baada ya Nyerere Nani amekuwa rais??
 
Back
Top Bottom