Money Maker
Senior Member
- Jul 11, 2011
- 146
- 31
Nafikiri mzee sitta ameona spidi ya EL ni kubwa hivyo anajikomba walau aendelee kupata mkate wake wa kila siku.
Kwani kasema uongo? Ni kweli wabunge wa CDM ni wanafiki.
Akitolea ufafanuzi kombora lililorushwa na David Kafulila, Waziri wa Uhusiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta ameikejeli kambi ya Upinzani kuwa ni wanafiki na waliojaa kauli nyepesi na za Ujanja ujanja na kazi waliyotumwa bungeni ni kufanya wanachokifanya sasa, hivyo wabunge wa CCM wawapuuze na kuwatazama kama walivyo kwani wananchi wanatazama na wataamua kwa wanayoyafanya.
Inashangaza kuona Sitta anaobuka na kauli hizi huku maji yakiwa shingoni kwa upande wake katika uwanja wa siasa. Akizungumza kwa mbwembwe huku akizomewa pia na baadhi ya Wabunge pale aliponukuu mfano wa hoja ya Posho
Sitta amesikika dhahiri akijikinga katika mwavuli huu kwa kuhoji inakuwaje leo wabunge wa Upinzani ambao wengine walikuwapo miaka kadhaa iliyopita bungeni na wamekuwa wakilipwa posho hizo kwa miaka mitano iliyopita leo wanziona si halali, warudishe posho zote ndio waseme kauli zao hizo za kinafiki alisisitiza Sitta.
Awali kigwangala nae aliangukia pua baada ya kuataka kuota muongozo kwa Mbunge wa Viti maalum CDM aliyeponda utitiri wa Vihiyo waliojaa MSD kuwa ndio kiini cha tatizo la upungufu mkubwa wa madawa kwa sasa Nchi.
Busara imehama tayari, tulimtegemea sana huyu mzee atuvushe kidogo kutoka makucha ya CCM ingawa kuyakemea, sasa looooo, mvi za bure. Yeye kwa busara????? zake tulitegemea awajenge wapinzania ili waikosoe serikali na kuisukuma iwatumikie watu, sasa anaukandia upinzani. Hajui kuwa kama sio kuwa na vyama vingi asingelikuwa na wzo la kuunda CCJ. SHAME UP ON YOU MZEE WETU
Jana nilimshangaa sana samweli sita kwa kweli kauli alizotoa bungeni juu ya swala la kafulila ukweli alapaswa afikiri kabla ya kuongea maneno yale. kwanza ameingia kwenye orodha ya viongozi wanaotetea posho jamani sita toka aanze kula pesa za walipa kodi toka awamu ya kwaza mpaka leo bado anazitolea macho huyu ni kiongozi hatari anayetoa kauli akiwa na jazba na ufinyu wa mawazo kwa kauli ya jana amejimaliza kisiasa