GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
Akitolea ufafanuzi kombora lililorushwa na David Kafulila, Waziri wa Uhusiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta ameikejeli kambi ya Upinzani kuwa ni wanafiki na waliojaa kauli nyepesi na za Ujanja ujanja na kazi waliyotumwa bungeni ni kufanya wanachokifanya sasa, hivyo wabunge wa CCM wawapuuze na kuwatazama kama walivyo kwani wananchi wanatazama na wataamua kwa wanayoyafanya.
Inashangaza kuona Sitta anaobuka na kauli hizi huku maji yakiwa shingoni kwa upande wake katika uwanja wa siasa. Akizungumza kwa mbwembwe huku akizomewa pia na baadhi ya Wabunge pale aliponukuu mfano wa hoja ya Posho
Sitta amesikika dhahiri akijikinga katika mwavuli huu kwa kuhoji inakuwaje leo wabunge wa Upinzani ambao wengine walikuwapo miaka kadhaa iliyopita bungeni na wamekuwa wakilipwa posho hizo kwa miaka mitano iliyopita leo wanziona si halali, warudishe posho zote ndio waseme kauli zao hizo za kinafiki alisisitiza Sitta.
Awali kigwangala nae aliangukia pua baada ya kuataka kuota muongozo kwa Mbunge wa Viti maalum CDM aliyeponda utitiri wa Vihiyo waliojaa MSD kuwa ndio kiini cha tatizo la upungufu mkubwa wa madawa kwa sasa Nchi.
Inashangaza kuona Sitta anaobuka na kauli hizi huku maji yakiwa shingoni kwa upande wake katika uwanja wa siasa. Akizungumza kwa mbwembwe huku akizomewa pia na baadhi ya Wabunge pale aliponukuu mfano wa hoja ya Posho
Sitta amesikika dhahiri akijikinga katika mwavuli huu kwa kuhoji inakuwaje leo wabunge wa Upinzani ambao wengine walikuwapo miaka kadhaa iliyopita bungeni na wamekuwa wakilipwa posho hizo kwa miaka mitano iliyopita leo wanziona si halali, warudishe posho zote ndio waseme kauli zao hizo za kinafiki alisisitiza Sitta.
Awali kigwangala nae aliangukia pua baada ya kuataka kuota muongozo kwa Mbunge wa Viti maalum CDM aliyeponda utitiri wa Vihiyo waliojaa MSD kuwa ndio kiini cha tatizo la upungufu mkubwa wa madawa kwa sasa Nchi.