Wanene kuongezewa marupurupu

Wanene kuongezewa marupurupu

Hivi Mzee Es umesoma shutuma za mswahili unayempongeza ama?

Embu tulia uzisome halafu ndio uje kumlazimisha zitto "aje kurudiha heshima ya forum"

Mwenzio nafikiria kuchukua likizo katika hii forum maana naona karibuni na mimi nitashindwa kujicontrol nikawa hovyohovyo kuanza kutoa shutuma za ajabu kwa watu na familia zao humu. Believe me nina mengi......na sio shutuma maana ninauhakika nayo kwani nayaona kwa macho yangu na kuyasikia kwa masikio yangu.

Tanzanianjema
 
Mzee TZnjema,

Sidhani kama nimemtaja Mswahili, nimempongeza Mtanzania na Masatu, hebu soma tena mkuuu na ninarudia tena kuwapongeza kwa kusimamia heshima ya forum kwanza kuliko wananchama!
 
Hapana mzee huu usanii wa mchana mchana kama vile watoto wadogo, WHY? Yaaani watu wazima na akili zao unaweza kuwarushia huu ujinga ninauona kwenye hii mada, badala ya kujibu kashfa?

Na kwale wanaomjibia ninasema kuwa hamuna tofauti yoyote na Malinzi, msemaji wa Ridhiwani, yale yale, usanii at best!
 
okee sasa nakuelewa.....

Lakini ukifuatilia huu mjadala tangie uanze unadhani Zitto akisema tofauti na kuwa "alikula uroda" kuna atakayeamini kati ya wale ambao tayari wameshamhukumu?

Na akisema amekula kuna kipi ambacho unadhani forum itafaidika nacho ama yeye binafsi atafaidika kisiasa ukichukulia manani hata kama ameonyesha mambo kadhaa tofauti na wengine lakini mwishowe yeye ni mwanasiasa tu....

Na jee kati ya jamboforum na wanajimbo wake ni nani mwenye haki ya kuambiwa huwo "ukweli" anaoshurutishwa hapa......mimi ningemshauri kama ana jipya kuhusiana na sakata hilo akalitolee kwa wapiga kura wake kwanza na ndio aje huku ambako ukweli ni wachache wanaomtakia mema....kama ambavyo tusivyowatakia mema wanasiasa wengine na wakati mwengine huwa najiuliza kama tunalitakia mema taifa letu pia.

Mwishowe unadhani kuwa katika mazingira kama haya ya kumsulubu ama "kuwasha hell" kama unavyoita wewe kwa kile kinachodaiwa kutokea, waheshimiwa wengine hapa watakuja wazi kama hawa jamaa na kutupa issue kama anazotupa Zitto? Kuwasha hell on issue sawa lakini sio personalities na familia zao kama principles za siasa nchini mwetu zinavyosema...

Ukweli ni kwamba ukitowa kuwa Zitto ni mtu wa karibu kwangu na niko proud na mazuri yake na kuumizwa na mapungufu yake, kinachofanyika hapa kinafanya nijiulize kama it worthy kutumia muda ninaotumia kupitia na kuchangia katika forum hii.

Zaidi inaniuma kuwa nimejiharibia kuwakaribisha watu wengi ninaowaheshimu katika forum hii na kufikia kushuhudia haya.....nashukuru mungu jana niliacha kumshauri mtu mmoja muhimu sana ambaye hata kama asingejitokeza humu kusoma tu kinachojiri humu kingemsaidia yeye na pengine taifa letu..


Tanzanianjema
 
Je viongozi wakisema ndio walikula pesa kwenye Richmond na Radar, je itageuza nini kwani hela si zimeshaliwa anyway? Then kama that is the case tunakuja hapa kufanya nini kwenye hii forum?

Kwa hiyo unasema kuwa viongozi wa CCM kama wakiamua kuwa wananchama hapa basi hatutawasulubu tena maana sasa ni wananchama hapa forum?

With all the heshima kwa Mheshimiwa Zitto, lakini haifaanyii haki hii forum kwa kutojibu kwa ufasaha kuhusu kasha iliyomkumba, kama kiongozi wa taifa letu na hasa sisi wananchi wa hii forum, forget huko jimboni kwake, ninaongelea hapa forum ambako yeye ni respected member, I have nothing personal na Zitto, kwa sababu ninajua kuwa huwezi kuwa kiongozi zubavu halafu ukapewa nafasi na kuwa mjumbe wa bodi ya Ujerumani na rais wa nchi hiyo kama yeye alivyo,

lakini on this ninasema kuwa hapana, tena mnachokifanya ni sawa na serikali kuyatishia magazeti ya Tanzania Daima na Mwananchi, kutaka kutufunga midomo kwa visingizio vya kuwa mjumbe hapa na the rst of the story, ninasema kuwa hadithi zenu hazi-hold water so far, Zitto aliamua mwenyewe kwa hiari yake kuingia kwa jina lake kamili, sasa pamoja na sifa zote alizopewa na anazopata hapa forum, pia kuna responsibility zake, na mojawapo ndio hii ya yeye kusimama tall than all of us!

The time is now!
 
Mzee ES said:
Ndio maana ninasema kuwa sisi wananchi hatuna vision wala busara, na pia ni wasanii wa kutupwa?

Sisi wanachi wote hatuna vision wala busara kweli? Kwa sababu ya mjadala wa Zitto na Amina hapa kwenye forum?

Je ina-include Mzee ES na Kichuguu? Duh!! Hah!!! hah!!! hah!!! hah!!!,

Itabidi nitatafute taputapu la kugwida ili niweze kutafakari zaidi namna ya kutafuta busara na vision zaidi.
 
Hakuna kashfa hapa! nimeeleza maisha aliyokulia zitto ndio sababu ya kufanya uovu wake.

BI Sent 50.

tuwekee picha ya harusi ya wazazi wake zitto. hilo litadhibitisha uongo wangu.

Malezi kwa watoto ni muhimu sana. ukiyakosa unaweza kuwa kauzu ukubwani.
aliyetukana ni Samvulachole kwa kumwita kipanya Zitto. lakini hamja muonya samvula kwa kumfananisha mbunge na panya, mko na mswahili tu,

mteteni na suzan mzee kadhalilishwa sana kwenye mada ya Malecela London. hapo mtakuwa mmeapply gender issue ila kumtetea mbunge ambaye hajatukanwa ni unafiki.

nilikubali kunyamaza lakini wametokea viuje wanaona sina data. nachelea kuweka mengi ya zitto mtaona kinyaa kukaa nae.
 
Busara na vision zinakuwaje ndani ya bunge ambalo, kuna walioiba hela za hela za wananchi kwenye Richmond, na wanaoiba wake za wananchi, ndani ya bunge hilo hilo?

Yes ni ukosaji wa busara na vision kufikiri mbunge kwamba aliyeiba mke wa mwananchi(kama kweli), atashindwa kuiba hela za wananchi akipewa nafasi!

Heshima ya forum haijengwi na kumtetea Zittto, wakati yeye mwenyewe yupo hapa hapa, isipokuwa inashuka na kuwa kama Mtandao na wapambe!
 
Mzee ES,

Tanzanainjema ameweka mambo haya bayana sana, na Mzee ES nawe unajua vizuri sana kusoma between the lines. Jibu la kwanza lililotyolewa na Zitto halikuwa zuri na wale waliomwuliuza zaidi walikuwa na haki. Hata hivyo baada ya kuwa amejibu na kuafirm yale yalikuwa yametangzawa magazetini huko nyuma, kulikuwa hakuna haja ya kumwandama tena, in fact alijibu swali sawa kabisa na jinsi ulivyomwuliza. Maswali ya follow up cross-examination type yangesaidia sana lakini badala yake watu walianza kumwandama kama vile tayari wana uhakika kuwa kweli alifanya mambo yale. Nina imani kabisa hata wewe unaona ubovu uliojitokeza katika maswali aliyoulizwa. Lazima tukubali kuwa hadi sasa hatujui ukweli wa jambo hili kwa vile hakuna aliyetoa details za kulithibitisha.

Yes ni ukosaji wa busara na vision kufikiri mbunge kwamba aliyeiba mke wa mwananchi(kama kweli), atashindwa kuiba hela za wananchi akipewa nafasi!

This is what I told Masatu kuwa hapa tuseme siyo busara (WISDOM) wakati yeye alidai kuwa LOGIC inatuma kuwa mtu akilala na mke wa mtu basi ataiba. Unfortunately LOGIC haisupport statement ile; kama unajua Logic Theory utakubalina nami.
 
hajawahi kufanya mkutano wowote kuweka wazi hili jambo.kichuguu acha kutupoteza. wapi na lini alifanya hivyo?
hata ukimkingia kifua. Zitto ananuka janaba la mke wa mtu. aje kujisafisha mwenyewe.
 
Mzee Kichuguuu,

Ninasema kuwa Mheshimiwa Zitto, aje hapa forum aseme ukweli na aulizwe maswali na wana-forum, that is all, the rest in mazungumzo baada ya habari kwangu na sipendi kabisaa huu utoto ninauona kwenye hii ishu ndogo na sasa inataka kukuzwa kuwa kubwa for nothing!

Mheshimiwa aje hapa aseme ukweli na kujibu maswali ya wananchi, kwa nini mnaleta maneno mengi?
 
Es.
Hujui anayeogopa polisi ni mhalifu?wewe kama hujaiba utaogopa polisi? Zitto anaogopa press conference na JF.
anaingia kwa majina mengine na haishi kunitumia PM kuwa ninyamaze.
 
Pamoja na yote Mzee Es naomba unijibu maswali yangu ili nami nielimike....

Tanzanianjema
 
Mswahili sikiliza,

Ni kweli hajawahi kuweka mkutano wa waandishi. Lakini nadhani alijibu kwa simu au kitu kama hicho na taarifa hiyo ikaandikwa magazetini. Cheki kule kwenye Vibweka, utakuta jibu hilo. Swali ambalo lilikuwa moyoni mwangu ni kuwa, jibu lile lilipotiwa na mwandishi wa habari tu, na wala haikuwa press conference kwa hiyo inawezekana walimisquote na vitu kama hivyo. Kwa hiyo alipofika hapa, wote tulikuwa na hamu kusikia jibu lake, a ngeweza kuwa na jibu tofauti na ilivyotangazwa. Mwishoni jibu lake lilrudia kuwa lile lile. Sijui kama lilikuwa ni jibu la kweli au la uwongo, tungejua zaidi kwa kumcross-examine. Ni wazi kuwa kama kweli alifanya, inawezekana asiseme hadi ashikishwe, na kumshikisha ilikuwa ni cross-examination. Tumeshindwa kufanya hivyo hadi akakimbia.

Mzee ES,

Unfortunately huwezi kumlazimisha kuja hapa na ndiyo failure iliyojitokeza. Sitegemei umwulize kwa matusi na kejeli halafu ajibu ndiyo nilitembea na mwanamke yule. Whether unayaona kuwa ni mazungumzo baada ya habari au unyaangalia seriously, that is the fact. Maswali yako ya kwanza yalikuwa ni mazuri na alitakiwa ayajibu na nadhani baadaye aliyajibu; maswali yasiyokuwa na msingi yaliyofuata yalivuruga kila kitu.
 
Wazee nimewasikia, haya sasa endeleeni kuwatukana viongozi wa CCM! maana ndio siku zote njia ya mkato, kumbe ikiwa Chadema tunakuwa mabubu?

Ninasema viongzi wa serikali hawawezi kuwa wasaniii bila ya wananchi kuwa the best wasaniii, na huu ndio mfano wenyewe kuwa sisi wananchi ni wasanii kama viongozi wetu, kule Malinzi ni msemaji wa Ridhiwani, na hapa Zitto ana wasemaji wake,

Ninasema hivi ninategemea Mheshimiwa Zitto, kuja hapa kujibu maswali ya wana-forum kwenye kashfa yake na Amina Chifupa, sina lingine wakuu, Mzee TZnjema, maswali anatakiwa kujibu Zitto, sio mimi, mimi ninan maswali tu kwake tena mengi sana, maana nina ushahidi mwingi kuhusiana na hiyo ishu, ndio maana nina maswali mengi na nina subiri, it does not matter what ninasema aje ajibu maswali hapa!
 
Nilishasema tangu mwanzo hakuna jibu litakaloridhisha na hakuna swali litakaloachwa kuulizwa! Mmemuuliza Zitto kawajibu. Haitoshi. Mmeyaleta ya mama yake haitoshi. Hamuwezi kukubali jibu lolote isipokuwa "ndiyo mimi na Amina tulikuwa na uhusiano wa kimapenzi na ulikuwa mzuri kweli". Akijibu hivyo haina maana itakuwa mwisho maswali yatakuja "kwanini uvunje ndoa ya watu, wewe kama kiongozi.. tukuamini vipi na wake zetu? vipi mabinti zetu na dada zetu, unawezaje kukaa Bungeni ilhali hivi na vile".

Kila mtu ana haki ya kuuliza lolote lile kwa mtu yeyote yule, lakini huwezi kumlazimisha mtu kujibu kama hataki. Haki ya uhuru wa kusema, inahusisha na uhuru wa kutotaka kusema! Ndio maana wenzetu wamarekani wanayo mabadiliko ya tano ya katiba!

Inapohusu mambo ya umma na yanayohusu maslahi ya TAifa kila kiongozi analazimika kutoa habari sahihi kwa wananchi. Hata hivyo hatuwezi kumlazimisha kiongozi kwa suala ambalo si la kisheria kutueleza habari za maisha yake binafsi? Hivi Malecela ana watoto wangapi? Je Kikwete amewahi kulala na wanawake wangapi? Mbona hatujawahi kumuona mke wa Lipumba? Vipi kuhusu Mrema na mke wake? Vipi kuhusu Freeman na mahusiano yake na kina dada? etc etc etc...

Mnaosema double standard, you have no idea what your setting up! Kama tunakubali (na ninaamini ndiyo hoja yenu) kuwa masuala ya chumbani na malezi ya familia za viongozi yanaweza kuchambuliwa hadharani. Basi tufungue mjadala huo na tusiishie kwa Zitto na viongozi wa Chadema tu, au viongozi wengine wa upinzani. Tuwazungumze wote kwa uhuru na uwazi.

Ninachosema na ninapenda kueleweka ni kuwa kama Zitto alikuwa anatuhumiwa kujihusisha na biashara fulani haramu, hilo linazungumzika; kama anatuhumiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mfanyakazi wake hilo linajadilika; kama Zitto angekuwa anatuhumiwa kuingiza jimbo lake kwenye mkataba wa ajabu ajabu hilo linazungumzika. Ni kutokana na mawazo hayo ndio maana tunauwezo na kila sababu ya kuhoji utendaji kazi wa viongozi wa serikali yetu, nia na matumizi yao.

Kuamua kutong'ang'ani kutaka kujua mambo ya undani ya chumbani ya mheshimiwa Zitto kwa vile tu yeye ni Mwakilishi wetu siyo unafiki! Sijawahi mahala popote kutaka kujua mambo ya chumbani ya Malecela, Kikwete, Kawawa, Lowassa, Nchimbi n.k SIyo kwa sababu hakuna madai dhidi yao au kwamba watu hawajui, ni kwa sababu tu kwamba jambo hilo linafungua sanduku ambalo hatuko tayari kulifungua. Mnapotetea kulazimisha Zitto awape undani wa kile "kilichotokea" hata kama keshakanusha hamtaki ukweli, bali mnataka ukweli kama ulivyoandikwa na nyinyi! Nilionya huko nyuma kuwa wanaotaka Zitto aseme hawawezi kuridhika hadi akiri kuwa na mahusiano ya kimapenzi na ni hicho ambayo baadhi ya ndugu zetu hapa wanataka. Chochote chini ya hapo, hakitakubalika.

Ninawaomba na tena nina wasihi kutoka ndani ya moyo wangu, msifungue sanduku hili la kujadili mambo ya chumbani ya viongozi au madhaifu ya kibinadamu ya viongozi wetu endapo mambo hayo hayahusiani moja kwa moja na nafasi zao, pesa za walipa kodi au maslahi yoyote yale ya kitaifa. Na msilazimishe kuwa kiongozi akienda msalani basi hilo ni jambo la kitaifa na mnataka details zake, kisa tu alionekana akienda msalani kwa jirani yake! Kipimo ambacho mnataka kukitumia kwa Zitto kikikubalika siyo kwamba kitaonesha umakini wa forum hii bali kutaishusha hadhi yake kuliko tunavyofikiria. Nawahakikishia kama mnafikiri mambo yanayojulikana ni ya Zitto peke yake fikirini tena. Wenye data za viongozi au wanaotaka kujua mambo ya viongozi siyo nyinyi peke yenu! Kuna watu wanajua viongozi wanaposafiri huja na kina nani, wanakaa wapi, na kina nani wanakutana nao. Tukikubali kuwa Zitto LAZIMA azungumze hapa (licha ya kuwa tayari amezungumza) na akiri (licha ya kuwa ameshakanusha) kuwa amefanya kitendo fulani (ambacho tayari amesema hakufanya) basi siyo kwamba tunataka kutenda haki bali kufurahisha tu udadisi wetu wa kibinadamu. Nawasihi tena, kama kweli ninyi mnaitetea forum hii, basi heshimuni mambo ya binafsi ya viongozi na hilo litumiwe kwa viongozi wote.

Hata hivyo endapo mambo yale ya binafsi yanahusiana na nafasi, vyeo, au yanaweza kuwa ni matendo ya kihalifu (criminal acts) basi hilo halina mjadala kwani hakuna mtu yeyote aliyejuu ya bodi au juu ya wanachama. Wote wako chini ya ukweli, ukweli mtupu, na si kingine bali ukweli.

Hata hivyo, sitarajii kuwa mtakubali ushauri huu kwani tayari mmeshanipa chama kuwa miye Chadema na ninamtetea Zitto. Na hii ni mara ya mwisho kuweka jambo hili sawa, mimi SIYO mwanachama wa CHADEMA ila ni mfuasi madhubuti wa mafundisho ya Mwalimu na mpenzi wa classical ideas za CCM. Kwa vile ninaandikia Tanzania Daima basi baadhi ya watu wamedhani mimi ni Chadema. Sasa hivi ninaandikia Kulikoni pia na sijui hilo linaendana na chama gani, na muda si mrefu (inshallah) nitaanza kuandikia magazeti ya serikali.

Mapenzi yangu ya kwanza na ya pekee yako mahali pamoja tu na hapo pekee ndipo ninaposimamia hoja. Napo ni Tanzania na Tanzania peke yake. Hakuna Chama, kiongozi, au mtu yeyote ambaye ni juu ya nchi yetu.

Narudia tena, siyo kwa jazba ya ujana bali kwa hekima ya uzee; TUSIFUNGULIE na TUKATAE kuendeleza mjadala huu wa masuala ya chumbani ya Zitto na Amina. Amina hataki/kazuiwa kusema tusimlazimishe; akitaka kusema ni haki yake na asizuiwe. Zitto ameshasema, tusimlazimishe aseme kitu ambacho hayuko tayari au hana tutakuwa tunafanya cyber bulling ili kutishia watu. Nawasihii tena, chonde chonde. Zitto keshazungumza, tukubali amefanya haki yake, zaidi ya hapo ni kujitafutia umaarufu usio wa lazima kwa mgongo wa kiongozi wa kitaifa! Hakuna cha kumkoma nyani geledi wala nini, ni kukomoana kinyama kwa kupigana mijeledi!

Na hii ni post yangu ya mwisho kwenye suala hili.
 
Kichuguu.

aliogopa nini kufanya press? mbona alikuwa na spidi kumkanusha rais kwa kuita mkutano wakati huo huo.? hili la ugoni ndio anaomba apewe muda.

umesema magazeti yaliandika. si kweli sema liliandika gazeti la chadema tu-Tanzania Daima, tena baada ya mwezi mzima. utapata picha kamili kuwa Tanzania Daima ni gazeti la kukampenia Chadema possible kabisa ile story ilipikwa. kwanini achaguwe kuongea na gazeti moja tu tena la chama chake?

ni sawa na kuomba kazi halafu unaulizwa reference unaleta toka kwa mkeo au mumeo. ilitakiwa taarifa itoke kwenye independent gazeti. si Tanzania Daima wala Uhuru. Tanzania Daima lilisema tumeongea nae kwenye simu tu kwanini hakwenda ITV,TVT,Majira.mwananchi n.k?

nilisema huko nyuma kuwa siri ya ugoni ni uoga na kuchanganyikiwa hadi urudi kuwa normal inachukua hadi miezi mitatu. ndio sasa anakuja kupitia mlango wa nyuma.

nakupa kisa cha mhalifu ndiye mara nyingi anaogopa na kuchukia vyombo vya sheria au polisi. mtu kama si mhalifu utaogopaje polisi? Kwanini ZItto aogope ukumbi wa habari-maelezo?kwanini asiyapeleke mahakamani magazeti na watu waliochafua jina lake? kwanini amvalishe koti mke wa mtu na hili hadi gazeti la chadema liliandika. jee kuna uhalali gani wa yeye kuvaliana nguo na mke wa mtu?

kichuguu,Zitto,Bi sent 50, TN na wana chadema wote nasema I CAN'T BUY YOUR STORY!
 
"We must forever conduct our struggle on the high plane of dignity and discipline"

Tanzanianjema
 
nina ushahidi mwingi kuhusiana na hiyo ishu,.....

Kumbe una ushahidi bwana. Kwa nini usiutoe kutusaidia sisi kuelewa jambo hili vizuri. Muda wote tunaongea kufuatia taarifa za magazetini ambazo zote siyo conclusive. Nimeuliza mara nyingi sana mwenye ushahidi zaidi ya taarifa za magazetini atufahamishe lakini hujawahi kutoa; matokeo yake tunajadiliana swala moja kutoka domain mbili tofauti: wasio na ushahidi na nyie wenye ushahidi, kwa hiyo no way tukafikia compromise.

Kama ulivyowahi kutoa ushahidi wote uliokuwa nao kuhusu Richmond, kwa nini hukutoa ushahidi huu wa Zitto/Chifupa pale tulipokuwa tunajadili stori hii. Huenda sasa hivi tusingekuwa tunavutana hapa kuhusu jambo hili
 
Back
Top Bottom