Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

Mwenzenu yamenikuta na kusema za ukweli nashindwa kabisa kuelewa namna ya kutoka hapa na kusonga mbele.

Ni mume nilompenda sana sana sana. Mungu katujaalia two beautifull kids na mengine ambayo am greatfull for. Tuliishi kwa upendo,furaha na amani hadi miezi 8 ilopita nilipogundua kuwa nilivyomdhania mume wangu sivyo alivyo.

Kwakuwa nampenda na kumfahamu sana mume wangu, kuna kitu nilikuwa tu nakihisi hakiko sawa kwa muda. Baadae nikagundua he was cheating. Yaani sitaki kuelezea mstuko niloupata na jinsi ninaumia jamani. Japo aliomba sana msamaha and all that ila moyo wangu umekufa ganzi wapendwa.

Mume nilompenda sana kwasasa namuona kama jirani yangu tu, hata hamu nae sina kabisa na hata tendo la ndoa ni kama ananibaka tu. Tushaongea sana, tushakwenda hadi vacation sie wawili tu ila sioni kinachobadilika. Akisafiri kikazi au mimi nikisafiri najisikia amani zaidi and i dont miss him kabisa.

Kuna wakati nilimuomba some alone time nifikirie kuhusu mustakabali wa hii ndoa, alinipa huo muda na kwa kipindi hicho cha wiki moja kichwani mwangu nilishangaa kunazunguka watoto wetu tu na sio mume wangu. Sijamueleza mtu yeyote kuhusu hili hata mama yangu wala mshenga wetu ila linanitafuna hatari.

Wenzangu mnawezaje kusamehe wanaume wanaowacheat na kurudi katika hali zenu za kawaida? Maana mie kwasasa mume wangu namuonaje sijui, nae naona hali hii inamtesa ila ndio hivyo tena[emoji134]
Sijisikii kumpenda wala kumheshimu tena, naona kama hadeserve kwa kutokuithamini na kuivuruga ndoa yetu.
Kwenye mahusiano huombi ushauri unatakiwa ufanye maamuzi yatayokufurahisha wewe. Kila mtu atakupa ushauri kulingana na safari yake mapenzi na siyo yako.
 
Duu pole sana, nilichelewa kuuona huu uzi,ila nakupà pole sana, yaani kwa mtu uliyemwamini na kumpenda kwa dhati mmm maumivu yake daa, ila kusahau ni ngumu sana unaweza kusamehe na mkaendelea lakini hilo kovu ni kwa NEEMA ya Mungu
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Ina maana hujui maana ya hii picha?
You have special place in heaven my dia. View attachment 1522767

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hiyo nimeielewa, kiukweli nina uelewa wa mambo mengi yanayohusiana na mapenzi na ngono kutokana na asilimia kubwa ya marafiki nilionao.

Na ndiyo maana humu ninaandikaga vitu hadi watu wanadhani sijui nimeachika sijui single mother lakini kiuhalisia sijaexperience hata kimoja bali ni michango ya watu walionizunguka tu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hiyo nimeielewa, kiukweli nina uelewa wa mambo mengi yanayohusiana na mapenzi na ngono kutokana na asilimia kubwa ya marafiki nilionao.

Na ndiyo maana humu ninaandikaga vitu hadi watu wanadhani sijui nimeachika sijui single mother lakini kiuhalisia sijaexperience hata kimoja bali ni michango ya watu walionizunguka tu.
Umeielewa lakini hujaiexperience.
Lakini naelewa it goes with age.
Ukishajua utamu hautobania [emoji28]
 
Back
Top Bottom